ali kibao

Alikuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Kamati Kuu ya CHADEMA

Mhanga wa Utekaji na Mauaji: Alitekwa nyara na watu wenye silaha akiwa kwenye basi la abiria mnamo Septemba 2024 akitokea Dar es Salaam kwenda Tanga.

Siku chache baadaye, mwili wake ulipatikana ukiwa umetupwa eneo la Ununio, Dar es Salaam, ukiwa na majeraha mabaya ya kuteswa (ikiwemo kumwagiwa tindikali).

Tukio lake lilizua hofu na mjadala mkubwa sana kitaifa kuhusu usalama wa raia, wanasiasa, na wimbi la utekaji nchini
  1. Erythrocyte

    JamiiForums Tanzania Mabasi mengi ya kisasa yana kamera, tunaamini waliomteka Hayati Ali Kibao wanajulikana. Polisi waanzie hapa

    Huu ndio Ukweli wa hali ya mambo kwa sasa, Hakuna mtekaji anayeweza kujificha, Ni suala la Polisi tu kufanya kazi yao ama Waamue wenyewe kuwalinda. Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana Baada ya Katibu Mkuu wa Chadema kutoa taarifa ya kutekwa kwa...
  2. Msanii

    JamiiForums Tanzania Ni wakati sahihi wa IGP kujiuzulu ama Rais achukue hatua

    Hakuna kinachozuia IGP kujiuzulu kwa haya yanayoendelea. Mauaji ya watu wasio na hatia tena mchana kweupe wanakwapuliwa kwenda kuuawa ni dhahiri polisi na usalama wanashirikiana kutekeleza hayo. TISS ipo chini ya ofisi ya Rais na aliitaka ikae chini yake kupitia mabadiliko ya sheria ya TISS...
  3. R

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Kwa hili la Ali Kibao hakuna yoyote ndani ya CHADEMA aliye salama!

    Hamko salama nyie nyote, Viongozi chukueni tahadhali, chukueni tahadhali na kaeni mtafakari kama chama nini kifanyike? Nini kifanyike? Usalama wenu ukoje be it Mbowe, Mnyika Heche, Lissu, Lema to mention but a few! Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa...
  4. Erythrocyte

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Kuuawa kwa Mzee Ali Kibao hakutafifisha jitihada za CHADEMA kuikomboa nchi

    Hili liwe angalizo kwa Watekaji na Wauaji na Viongozi wa Nchi ya Tanzania Wanaowatuma kuteka na kuua, Kwamba CHADEMA haitavunjika Moyo kutokana na Mauaji ya Mohamed Kibao, hizi mbinu za vitisho kwenye zama za sasa ni mbinu zilizopitwa na Wakati. Mzee Kibao alipokuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga...
  5. Chachu Ombara

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Polisi: Tunachunguza kubaini chanzo na watu waliohusika kumchukua Ali Kibao

    TAARIFA KWA UMMA Jana Septemba 6,2024 zilisambaa taarifa kwenye mitandao ya kijamii ikieleza kuwa jioni maeneo ya Tegeta Jijini Dar es Salaam, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ally Mohamed Kibao, akiwa safarini na basi la Tashrif alichukuliwa na kushushwa toka kwenye basi hilo na watu ambao...
  6. Chachu Ombara

    JamiiForums Tanzania CHADEMA: Mzee Ali Kibao ametekwa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama akiwa kwenye basi. Usalama wa Taifa waeleze alipo

    Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika akizungumza na wanahabari mchana wa siku ya Jumamosi Septemba 7, 2024 Makao Makuu ya CHADEMA, Dar es Salaam amesema kuwa... “Kwa aina ya bunduki walizokuwa nazo hao watu waliokuja kumchukua (Mzee Ally Mohamed Kibao ambaye ni...
  7. Erythrocyte

    JamiiForums Tanzania John Mnyika: Kiongozi wa CHADEMA Mzee Ali Mohamed Kibao, adaiwa kushushwa kwenye Basi na kuchukuliwa na watu wasiyojulikana

    Hii ndio Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu, John Mnyika kupitia ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X (Twitter) --- John Mnyika kupitia ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X (Twitter) anaripoti: Nimetaarifiwa usiku huu kuwa Mzee Ali Mohamed Kibao Mtaalamu katika Sekretariati CHADEMA amechukuliwa na...
Back
Top Bottom