Sasa kumbe shida iko wapi, ifanye Mtwara nayo ikusanye mapato hata 40 percent, then inufaishe nchi nzima, iwe hivyo kwa dhahabu ya Geita, Kahama, Tanzanite ya Arusha, Kahawa ya Kilimanjaro , Mahindi ya rukwa, Mkonge wa Tanga, Nazi za Bagamoyo etc
Mkuu usitake kupotosha, suala la gas kwetu sisi wa Mtwara halijalishi vyama vya siasa, ni la kimaslahi kwa watu wa Mtwara bila kujali itikadi zao, unaweza kulichukulia juu juu kimtazamo wako wa kipropaganda ila wananchi wameamka na wana ari kubwa kutetea maslahi yao
Tunashukuru Jf kuonyesha maandamano haya, maana vyombo vyetu vingi vya habari wameyapotezea, labda ni kwa maelekezo maalum, ila waonyeshe wasionyeshe wananchi wamesema sasa bhaaas, gesi haitaondoka kirahisi kama walivyofikiria
The Big show nakupongeza kwa kuendesha harakati kwenye mtandao wa jamii, jitahidi kusambaza elimu hii iwafikie wananchi waliowengi huko, si rahisi kwako kuwafikia wote, ila unaweza kuwapata watu wachache wenye ushawishi wasambaze harakati hizi kwa wengine
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.