Habarini,
Nina imani hamjambo, leo ninataka kushika mkono watu kadhaa ambao nitavutiwa na kile ambacho wanakifanya.
Kama unaamini kazi/shughuli unayofanya ina upekee na jamii itapata kujifunza kupitia kazi yako unayofanya basi naomba uelezee kwa ufupi aina ya kazi unayofanya (huenda usiwe wewe...
Mara nyingi sana nimekuwa katika mgogoro na majirani zangu humu ndani, nimekuwa nawadhihaki na kuwasulubu kwa maneno mabaya sana hawa majirani ila yote haya ni kutokana na mienendo yao mibaya ambayo mara nyingine hukera na mtu akashindwa kuvumilia.
Miaka 4 niliyopita nilipata kiwanja sehemu...
Takriban miezi 6 sasa natumia Telegram kwa ajili ya masuala fulani ila baada ya kujiunga nilitumiwa link na mshikaji wangu nami nikajiunga kwenye group moja la [emoji725] najua mnaelewa.
Sasa nikawa napata material ya lile group (videos na pictures) ila wiki moja sasa imepita nimeona picha...
Kwanza nimejikuta nachukia sana barakoa baada ya watu kukataa kuwa mtu niliyepiga naye picha siyo Diamond. Jana nilikuwa namsikiliza redioni asubuhi na akasema anaenda kuonesha watu hotel yake aliyonunua nikajiandaa kufika maeneo yale aliyokuwa anaenda ili nikapige naye picha kwani mimi ni...
Kipindi fulani nilikuwa ni mwajiriwa wa kampuni moja kama mlinzi wa mali wa zile kampuni hakika nilifanya kadi nzuri na mwisho nikawa mfanyakazi bora wa kampuni kwa namna ambavyo wengi hawakutegemea.
Nilikuwa naingia lindo saa 11 jioni na kutoka saa 12 asubuhi kila siku, ofisini kulikuwa na...
Kipindi fulani nikiwa kijijini nilikuwa nimebuni kitoweo ambacho kwa kweli kulikuwa kinanipa sana nyama ila kupatikana kwake haikuwa kazi ndogo.
Nilikuwa nakata ndimi za ng'ombe na kunywa supu bila wenye ng'ombe kujua kama wanyama wao hawana ndimi. Siku moja nikiwa nimekaa wazo likaniijia namna...
Tumeambiwa tusisogeleane na kukaa katika mikusanyiko kuepusha kuenea kwa Corona ila huku kijijini wazee wamekuwa hawasikii kila siku jioni wakaa kwenye mti mkubwa hapa kijijini na kucheza bao na wengi wanakuwa hawajavaa barakoa na gloves.
Niliwafuata nikawapa elimu ya maambukizi ya Corona na...
Baada ya kuzuka kwa gonjwa la Corona tuliletewa vikinga pua na mdomo (barakoa) na gloves za kuvaa mikononi hivyo vitu alitutumia mjomba mimi na mama na ndugu wengine.
Mama yeye anasema akivaa barakoa hapumui vizuri na wengine pia wanasema hivyohivyo ila mimi nimevaa naona kawaida na sema kweli...
Kipindi fulani nilikuwa na uhitaji wa hela sana nilitafuta njia mbalimbali za kupata kiasi kile cha pesa ila haikuwezekana ila alikuwepo jamaa mmoja alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu huko Dodoma akaniambia kwanini nisiende bodi ya mikopo kuomba mkopo nione kama nitafanikisha.
Kweli nilipata...
Wakati kazi imekosekana Dar nipo nipo tu mjomba wangu hanipi sapoti licha ya kuwa vizuri kiuchumi nakumbuka alinipa mtaji wa kuuza vitumbua ila yeye akachangia biashara yangu pia kufa.
Baada ya mihangaiko ya kusaka kazi kuwa mingi na isiyo na matunda, siku moja mjomba ameniambia kesho nijiandae...
Bibi yangu aliyekuwa rafiki yangu mkubwa na mshauri ulipotangulia mbele za haki na akaniacha na maumivu makubwa sana. Ukiwa uliisha ila chuki yangu na mjomba imekuwa kubwa mara baada ya msiba wake.
Bibi alipofariki mjomba alikuwa Dar, yeye ndiye kijana mkubwa wa kiume kwa bibi ila mama ndiye...
Habari mabibi mabwana,
Lengo la huu uzi siyo kuonesha udhaifu wa mifumo yetu ya ulinzi ila pia kusaidia mifumo yetu ya ulinzi hasa polisi kupambana na wahalifu waliojizatiti kimbinu na kiakili.
Siku mtu anaokoka huamua kusema mengi kuhusu yale yote aliyofanya kipindi cha nyuma, kutoa siri ni...
Baada ya ubatizo niliendelea kuwa muumini mwenye nidhamu kanisani na nikawa nafanya kazi zote za kikanisa hasa masuala yanayohusu vijana pia na mambo yote ya ndani na nje ya kanisani.
Takribani mwezi mmoja kiongozi wetu wa kwaya alikuwa anaumwa sana, baada ya kulazwa kwa wiki 3 mfululizo...
Nilipata nafasi ya kuendesha gari ya raia mmoja wa Asia aliyekuwa hapa nchini kibiashara, alikuwa na gari la abiria lililokuwa linafanya shughuli zake huko jijini Dar es Salaam.
Wakati naanza kazi tulikuwa wawili, mimi na kondakta ambaye baadae tulikosana kwa sababu ambazo niliona ananionea na...
Kipindi maisha yamenivuruga sina kazi wala makazi ni Bibi pekee aliyekuwa msaada mkubwa kwangu katika nyakati zote ngumu nilizokuwa napitia kipindi kile.
Kabla sijaanza kulima ulezi baada ya kutoka Dar kwa mjomba nilikuwa katika msongo mkubwa sana wa mawazo hata ulaji ukawa shida licha ya kuwa...
Rafiki yangu wa damu tangu tukiwa watoto hadi utu uzima naomba niwie radhi sana.
Leo nimeona niwape kisa ambacho kilipelekea urafiki wangu na yeye kufika tamati. Siku moja nilikuwa nyumbani nimefua nguo zangu na matandiko nikaweka safi majira ya mchana nguo zilikuwa zimekauka nikaanza kukunja...
Mwaka 2010 Mama alienda kwa kaka yake (yule mjomba wangu ambaye hadi leo tuna uhasama) mama alikaa miezi 6 Dar na siku anarudi alikuja na Sahani ambazo zilileta uadui na jirani hadi ikafikia hatua tukatumia nguvu za giza kupambana nae.
Mama alikuja na sahani 6 za mfupa ambazo alipewa na kaka...
Kule nyumbani tulikuwa na mgogoro wa ardhi kati ya kijiji chetu na kijiji jirani sasa jitihada zilifanyika kumaliza ule mgogoro ila ikashindikana ikabidi aje mkuu wa wilaya kutoa suluhu ya ule mgogoro.
Baada ya kufika ikagongwa kengele na tukakusanyika wote chini ya mti mmoja mkubwa pale...
Mwaka fulani kijiji kulitokea msiba wa mzee mmoja hivi mkubwa na aliyekuwa na mali nyingi hasa mifugo, nyumba na viwanja. Sasa vijana tukaitwa siku moja kabla ya msiba ili tujiandae na tuwe tayari kwa lolote, tukapewa majukumu ya kuhakikisha usafi umefanyika mazingira yote na maji yapo ya...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.