Wiki iliyopita TRC ilirejesha safari za treni za mizigo kutoka Tanzania mpaka Kampala Uganda kupitia Tabora, Isaka, Mwanza na Ziwa Victoria kwa kutumia bandari ya Mwanza na Port Bell nchini Uganda.
Hatua hiyo imefanyika baada ya kusitishwa kwa usafiri huo kwa miaka 10, jambo ambalo kurejeshwa...
UJENZI wa ukuta kuzunguka Mgodi wa Tanzanite Merereni, mkoani Manyara wenye mzunguko wa kilomita 24.5 unaratajiwa kukamilika mwishoni mwa Aprili, mwaka huu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliliambia Bunge na Watanzania wote mjini Dodoma jana wakati akiahirisha Mkutano wa 10 kwamba, ujenzi wa...
RELI ya Kisasa (SGR) inayojengwa hapa nchini imeelezwa kuwa ni reli bora kuliko zote Afrika. Mradi huo unaotekelezwa na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (Rahco), ilianza awamu ya kwanza ya ujenzi Mei, 2017 na inajengwa na Kampuni ya Kituruki ya Yapi Merkezi kwa ubia na Kampuni ya Mota-Engil...
Naungana na Watanzania wote kutoa pole kwa familia ya Komredi Kingunge
Ngombale-Mwiru, kutokana na kifo cha mwamba huo wa siasa katika Taifa
letu. Mzee Kingunge atakumbukwa kwa umahiri wake wa kujenga hoja na weledi
aliojaaliwa na Mwenyezi Mungu, hata akaweza kuwa lulu na moja ya injini
muhimu...
RAIS mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, alipata kuzungumza huko nyuma kuhusu zama. Akizungumza kwa ujumla tu, lakini kwa maana pana, alisema kila zama zina kitabu chake. Msingi wa hoja yake hiyo ni kwamba, si sahihi kulinganisha zama mbili tofauti kwa kutumia muktadha mmoja.
Bila shaka, hizi ni zama...
JUMUIYA ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Meru mkoani Arusha, imesema ni marufuku wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari kwa wasichana kuvaa sketi fupi na wavulana kunyoa viduku, kuvaa suruali chini ya makalio ili kulinda na kutunza maadili ya Kitanzania.
Pia jumuiya hiyo...
UHALIFU umekuwa ni adui mkubwa wa maendeleo kwa mtu binafsi, familia na hata Taifa kwa ujumla. Pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama kukabiliana na uhalifu huo, lakini pia wahalifu nao wamekuwa wakibuni mbinu mbalimbali za kutekeleza uhalifu.
Utakubaliana...
IDADI ya madiwani wa Jimbo la Iringa Mjini waliochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inazidi kuputika baada ya diwani mwingine, Oscar Kafuka wa Kata ya Mkwawa kutangaza kujiuzulu juzi usiku.
Kafuka anakuwa diwani wa sita kubwaga...
MWISHONI mwa mwaka jana, Rais John Magufuli alizindua Hospitali ya Taaluma na Sayansi ya Tiba (MAMC) maarufu kama Kampasi ya Mloganzila, hatua iliyoashiria kuanza rasmi kutumika kwa hospitali hiyo.
Hii ni hospitali ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Muhimbili, (MUHAS) iliyopo katika...
MKUTANO wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), uliokuwa ufanyike Novemba mwaka jana, sasa umepangwa kufanyika Februari Kampala, Uganda.
Mkutano huo unatarajiwa kuwa na uzito wa kipekee kutokana na viongozi wa EAC kujadili masuala ya miundombinu ndani ya nchi sita za...
"Ni kama Ulaya" Ni kauli inayotolewa na watu wengi (niliokutana nao) waliofika katika Hospitali ya Taaluma na Tiba Mloganzila (MAMC) iliyopo mpakani mwa Kisarawe mkoani Pwani na Ubungo, Dar es Salaam.
Hii ni hospitali inayowakilisha mapinduzi makubwa nchini katika sekta ya afya kutokana na...
Serikali za Wanyama na ndege au Wadudu;
Ndani zina taadhima, kama kwamba maabudu;
Na watu wenye hekima, siku hizi hawamudu
Madaraka na heshima, heri mnyama na mdudu
Vinywa vimewaachama, tamu imekuwa ngwandu
Na heshima imehama baki taka na mashudu
Na madhara na dhuluma miungu ya kuabudu...
MAGARI ya kifahari yaliyokwama kwa muda mrefu Bandari ya Dar es Salaam kutokana na waagizaji kushindwa kulipa kodi mbalimbali kwa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), yameanza kupigwa mnada huku kukiwa na dosari zilizofanya mnada usimamishwe kwanza.
Hata hivyo, wakati magari hayo yakipigwa mnada na...
TANZANIA imetunukiwa tuzo ya kimataifa, kwa kufanya vizuri katika utekelezaji wa sera za mapambano dhidi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza kupitia taasisi za kiraia.
Tuzo hiyo iliyotolewa kwa Shirikisho la Vyama vya Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza Tanzania (Tancda), imetolewa na Shirikisho la...
TAIFA letu lina watu wachokozi. Watu wa aina hii wana hulka ya ugomvi, wana roho ngumu kama paka, hivyo ili kuishi nao ni lazima tuwe wakali. Wakituchokoza tuwaponde utosini kufifisha utukutu wao.
Sifa za watu wenye hulka ya ugomvi ni kupenda kuwachokonoa polisi na kukimbizana nao, ni kawaida...
RAIS Yoweri Museveni wa Uganda amewatembelea walinda amani wa Tanzania, waliojeruhiwa wakiwa kazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika shambulio, lililosababisha vifo vya wapiganaji 15 wa Tanzania na kujeruhi wengine 44 waliopo chini ya mwamvuli wa majeshi ya Umoja wa Mataifa...
MWENYEKITI wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni Shehe wa mkoa huo, Alhad Mussa Salum amewataka viongozi wa kidini kuacha siasa za chuki dhidi ya viongozi wa kitaifa katika majukwaa yao ya ibada.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Shehe Alhad alisema siku za hivi karibuni...
WASOMI na Wanasiasa maarufu nchini wamesema kuwa wanaridhishwa na hali ya kisiasa iliyopo nchini kwa kipindi chote cha mwaka 2017.
Kuridhishwa huko kumetokana na hali ya utulivu na utendaji makini wa Serikali ya Awamu ya Tano ambayo inajali watu wake. Makamu Mkuu mstaafu wa Chuo Kikuu cha...
SERIKALI imewataka walimu wapya 3,033 wa shule za msingi na sekondari, kuripoti katika vituo vya kazi kuanzia Desemba 27, mwaka huu hadi Januari 7.
Kati ya walimu hao, walimu 266 ni wa sekondari na walimu 2,767 ni shule za msingi. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa...
MFUMO wa Kukusanya Mapato Kielektroniki (eRCS) umeonesha mafanikio makubwa kwa miezi mitatu ya mwanzo ya Julai, Agosti na Septemba mwaka huu.
Hii ni baada ya makusanyo ya kodi kwaupande wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRB) kupitia eRCS kufikia Sh bilioni 7.2, ukilinganisha na Sh bilioni 3.5, ZRB...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.