Sijakuelewa ukimwita mtu padre ulifikiri sio udini bali ni nini? Kweli Dr. alikuwa padre sasa kumwita padre ni kutaka kusisitiza huo upadri kwani kwa sasa hafanyi kazi ya upadri. Na huo ni udini!
Kadi elfu nne kwa staili huwezi kuzipata! Sidhani kama hata thelasini zipo! Pia nimeona bendera kama nne hivi. Lakini huu ni mchezo wa kuigiza tu. Kwa njaa hii kila kitu kinawezekana!
Kauli mbiu yako ya "vua gamba, vua gwanda, vaa uzalendo" sio sanifu. Kwanza umeitohoa kutokana na ya Chadema ya "vua gamba, vaa gwanda"
Uzalendo ni kitu kisichoonekana bali matokeo yake ndio yanayoonekana. Uzalendo ni mawazo ambayo hujazwa kwa watu kupitia mafundisho ya mara kwa mara ya watu...
Hakika CCM haijatulia kabisa! Wamepoteza dira kama alivyosema Horace Kolimba (RIP). Sasa wanaendeshwa puta na Chadema!
Chadema wamekuja na M4C wakiwa na slogan " vua gamba, vaa gwanda". Juzi juzi Nape akaiga na kuanzisha "vua gamba, vua gwanda, vaa uzalendo". Hakuna ubunifu hapo bali uigaji...
Kumekuwa na wimbi la mawaziri na viongozi wa taasisi mbali mbali nchini kufanya maamuzi ya kukurupuka kwa lengo la kutaka kujipatia umaarufu na kujihakikishia nafasi za uongozi. Kila tasisi na wizara utasikia huyu na yule kasimamishwa kazi bila hata taaratibu za kazi kufuatwa. Jamani utawala...
Neville Meena hana kosa lolote kwani ameongea ukweli wake. Kimsingi yeye anaitambua Tanzania na sio Tanganyika.
Suala hili linavurugwa kabisa na katiba yenyewe ambayo haiitamki Tanganyika bali Tanzania Bara. Sasa Tanzania Bara ni nchi gani kihistoria?
Jeshi la Polisi nchini limekosa utaalamu wa namna ya kushughulikia mikusanyiko mikubwa na maandamano makubwa hapa nchini. Mara nyingi huibuka na hadithi ambazo haziingii kwenye akili ya mwananchi wa kawaida. Kuzuia maandamano, kwa upeo wangu, ni kukiri kushindwa hasa pale ambapo sababu...
Sikushangai ndugu yangu najua hayo ni matokeo ya "mental slavery" chini ya mfumo fulani wa uongozi kwa muda mrefu. Umepoteza uwezo wako wa kufikiri kwa kuwa umejazwa hofu na kutojiamini kwa muda mrefu. Pole sana.
Ila baadae ya utakuwa huru. Na fikra zako zitakuwa sawa!
Shirika la habari la Nation Media la Kenya nalikubali sana kwa weledi wake kwenye tasnia ya habari katika jumuiya ya Afrika Mashariki.
Ninachoshangaa ni kwa nini hatuna TV inayomilikiwa na shirika hilo hapa nchini kama Kenya na Uganda . Ombi maalum kwa Tido Mhando ni kutuhakikishia kuna kituo...
Mbona hii story imekaa kipropaganda zaidi ya ukweli?
Inataka kujenga hisia wanaovua gamba ni watu waliopangwa kufanya hivyo na CDM ijapokuwa ukweli unajulikana kwamba kwa sasa watu wameichoka SISIEM. Jambo linalonitia shaka ni idadi ya hao vijana. Kwa kuwa CDM wanataka kuuaminisha na...
Nimefuatilia kwa karibu mambo yanayojiri kati yako na BAVICHA baada ya kutoa tamko la kutaka kugombea urais kupitia Chadema katika kikao cha NEC ya CCM na kumuomba mh. Rais Kikwete awe mpiga debe wako wakati wa kampeni. Kwanza, hapa ninaona kuna UTANI na KEBEHI ya hali ya juu kuliko hoja. Lakini...
Sasa mbona unaanza umbea tena? Inaelekea wewe ni mwandishi wa hilo gazeti! Sijui gazeti gani hata hivyo! Kuna swali juu ya biashara ya madawa ya kulevya na akajibu hausiki na hiyo biashara.
Haya mambo ya nasikia nasikia yanatoka wapi? China kuna kuokolewa kwa issue ya dope? Labda wamekudanganya...
Hiyo ndio propaganda ya kila wakati wa uchaguzi ya kuviingiza vyama vya upinzani katika migogoro ili chama tawala kifaidike!
Ni kwa nini usipendekeze kwenye tume ya katiba kuwepo kwa serikali ya mseto ambapo vyama viwili ambavyo havijafikisha zaidi ya nusu ya kura viweze kuungana na kuunda...
Nape naomba unieleze kwa nini CCM hamtaki mjadala juu ya mfumo mzuri wa Muungano? Kwanini mnaelekeza tuwe na serikali 2 badala ya 3 huku mkitambua hili suala linabishaniwa tangu enzi za akina Aboud Jumbe? Je kwanini hamuoni hiyo haja? Au mpaka wapemba na watanganyika waanze kujitoa mhanga?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.