Hili neno la uzima limetulia kweli kweli, isipokuwa tu haliko kwenye jamvi lake.
Sijui kama taratibu zimebadilika, lakini ilikuwa unawatumia wahusika ujumbe binafsi wakuwie ruksa kubandika mawaidha yako mawili matatu kwenye jukwa husika. Sio jamvi la siasa. Enenda na amani ya Bwana, na...
Mheshimiwa Dr. Slaa, wewe ni kiongozi, Mbunge wetu, huwezi kututamkia "Watanzania hawaelewi issues"!
Kisiasa inaonyesha hujali hata kutuonyesha unanyenyekea kwa tuliokupa taadhima ya kutuongoza, na ulivyo mwepesi kutumia lugha za kujumuisha watu jumla jumla na kuwashusha. Tafadhali Mheshimiwa...
Basi kama unakubali kwamba nadharia ya Taifa Teule ni hekaya, na kwamba kipaji chake hakitokani na Uyahudi wake, unapoona taarifa ya Myahudi mwenye kipaji acha kujikunja kinyumenyume kuimbia sifa weledi wa taaluma wa Wayahudi wa miaka elfu tano ulela. Toa muktadha wa uhusiano wa kipaji na...
Mheshimiwa Dr. Slaa ametuambia amepitia "Kumbukumbu Rasmi za Bunge" na "Schedule of Amendments" na kuhitimisha kwamba swala hili halikupitishwa na Bunge.
"Hansard" ni Kitabu cha Kumbukumbu ya Mazungumzo katika Bunge. Je pia rekodi rasmi ya kila kilichofanyika Bungeni? Vipi kama kipengele...
Elimu ya vinasaba na asili ya viumbe hai inafundisha kwamba hakuna kundi lolote la binadamu au Wamakonde, au Wayahudi au Mataifa, ambalo lina kipaji cha akili kuliko kundi lingine liwalo lote. Inatakiwa nirudie, hakuna!
Ulichoeleza kinasaidia kufasili ni kwa nini kuna Wayahudi wengi waliobobea...
Hizo ulizotoa ni taarifa za matokeo ya mitihani yote miwili, kidato cha nne na sita?
"Kama sikosei...sina hakika...kama nakumbuka...washashi nisahihisheni" zimesheheni kujengea msingi wa hoja ya kumwombea msamaha mtahiniwa ukitetea matokeo. "Kama nakumbuka vizuri," kama unakumbuka vibaya...
"Endapo wakijenga," kina nani wakijenga?
Usiniambie tukutanulie barabara ili siku "ukipata bahati" ya kwenda kwenu utanue.
Una jukumu, sio "ukipata bahati," una wajibu wa kwenda kujenga ardhimama yako!
Kipaumbele chetu cha kwanza sasa hivi sio kutanua upana wa barabara. Usiwe nje ya mguso...
Duu, ndugu mwandishi umetuchambulia na kututafsiria sheria na katiba kwa staili ya meza kama ilivyo, bila kutupa nukuu ya kipengele hata kimoja.
Sheria inakosea, sheria inasema, sheria inakataza... Sheria inasemaje?
Basi wanajamvi na "harakati za komputa" wazidi kuwa na nguvu, na wapongezwe, kama ndivyo.
Lakini wakati tunapima ufanisi na tija ya mchango wa JF, ingependeza tujue wana JF walifanya nini katika kuzuia majengo haya yasiendelee. Katika maandamano ya wakazi wa eneo hilo kulikuwa na bango la...
Sio baraza la mawaziri kwa ujumla wake ndio linaamua ubinafsishaji wa shirika kama NBC?
Kama mwenyekiti wa baraza la mawaziri kala hongo halafu kapigia chapuo kuuza kipande cha nchi na wajumbe wa kikao wamenyweshwa chai na chapati za Ikulu wakalala kikaoni hoja ikapita basi kosa la kuuza NBC...
Sio swala la "Wana Simba mmekereka," ni swala zaidi la kiufundi/kikazi kuhusu uandishi habari nchini:
Jana habari muhimu kuliko zote nchini kimichezo ilikuwa ni kuna timu imeshinda ubingwa, haijalishi ni ipi, kuna mechi iliyoamua klabu bingwa itakayoiwakilisha Tanzania kimataifa. Utaachaje...
"Waliosikiliza watasema" ndio kina nani hao? Wewe unatuambia umetumia "common sense" kujua alichokisema msemaji, nadhani tupate aliyesikiliza. Uganda na Burundi umezifichaficha kwenye mabano kwa nini, zilisemwa au ni makadirio sahihi yako wewe?
Tanzania "haikuwemo kwenye listi," sawa, taja...
Umeshukuru nini sasa Jaji?
Huyu kiongozi anaweza kuwa na nia nzuri lakini kauli zake - ambazo ni kielelezo kizuri cha upeo wake - zinatia shaka. Katika nasaha hizo hizo alidai: "Adhabu zinachangia msongamano, sio kila siku kutoa vifungu, unao uhuru wa kutoa adhabu mbadala,"
Anawaambia...
Na ndo maana hatuendelei; hata kwenye dirisha la kukusanya ada mbali mbali kama TRA, DAWASCO, mahakama, Luku, n.k. unakuta hakuna mtu dirishani. Ndio vyanzo vya mishahara yao halafu wanaringa kupokea.
Mtu anaomba contacts za kuchangia CHADEMA, anaambiwa lazima awe na simu ya Voda au Zain!
Itapendeza zaidi kama tukipitia upya mila na sheria zetu.
Mzizi wa fitina wa tatizo la tegemezi la kiuchumi la mwanamke kwa mwanamme umechimbiwa kwenye sheria:
It shall be the duty of every husband to maintain his wife or wives and to provide them with such accommodation, clothing and food...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.