Jaji Mkuu: Tusijifananishe na Kenya, Mahakama zetu zipo huru zaidi

Jaji Mkuu: Tusijifananishe na Kenya, Mahakama zetu zipo huru zaidi

Kaanza huyu nae divai limeanza kumkolea kama yule mwenzie bondia...[emoji15] [emoji15]
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Jaji mkuu wa Tanzania Ibrahim Juma amaesema sio sahihi kufananisha mahakama zetu na mahakama za Kenya na kusema mahakama zetu zipo huru zaidi


Hivi alikuwa anajisikia kweli kipindi anatamka hayo maneno?!
 
Jaji anaitisha Press!!

Tanzania tuna mhimili mmoja tu.. Bunge naj mahakama tayari kapuni
 
Ni kawaida yenu ata yule mrangi alisema hana cha kujifunza Kenya,
 
Nakala ya barua yake kutoka london ameipata?

Au albadir inamnyevua?
Tuliambiwa mpango mzima ulifanyikia nyumba kuu!
 
Inategemea jaji Mkuu alimaanisha uhuru gani. labda alimaanisha uhuru wa kutafsiri sheria au wa uhuru wa kupanga mda wa kusikiliza kesi (kalenda) au uhuru wa kuajiri watumishi wa mahakama. Lakini kiukweli uhuru wa mahakama kwa tanzania ni neno la kusadikika.

Ni bora kabisa mahakama za mwanzo na mahakama za wilaya zina chembe chembe ya uhuru wa mahakama. Lakini ukifikia Mahakama za Mahakimu wakazi, Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa uhuru wa mahakama haupo. Ndio kuna kesi mahakimu na majaji wanaamua kwa utashi wao, tena bila kuhofia chochote. Lakini kuna kesi mahakimu na majaji wanaamua si kwa utashi wao wala si kwa kufuata misingi ya kisheria, bali wanaamua kwa misingi ya matakwa ya Serikali kuu (executive).

Kuna kesi nyingi sana tu (sitazitaja hapa kwa makusudi maalumu) mahakama ilitoa maamuzi hata kabla ya kusikiliza kesi hizo, kilichofanyika ni kutekeleza utaratibu tu ili kuonesha utaratibu umefuatwa. Nina mifano kibao ya kesi ambayo majaji (zilizokuwa mahakama kuu) na mahakimu (kwa kesi za mahakama za wilaya na mkoa) walifuatwa faragha na kuambiwa waharakishe kusikiliza kesi hizo, au zile walizoambiwa wacheleweshe usikilizwaji wa kesi hizo kwa makusudi, na zingine waliambiwa wafanye wafanyalo lakini uamuzi wa mwisho uwe na muelekeo fulani.

Hivi kuna anaejua kuwa hakuna kesi ambayo serikali (executive) ina interest nayo ambayo hupangiwa kusikilizwa na jaji au hakimu wa hovyo au wasiuyempenda? Ni utaratibu uliopo majaji hupangiwa kesi kulingana na yeye alivyo na mtizamo wake kwenye serikali, na mahakimu wanapangiwa kesi kulingana na kesi yenyewe.
Baada ya kuukosa ujaji mkuu unaanza kujielewa bado dikteta atakushika saburi ndio uanze kubwatuka vizuri
 
Jaji mkuu wetu kaanza vibaya.
Kenya ina sifika kwa sababu katiba yao inaruhusu matokeo ya kiti cha urais kupingwa mahakamani.Na hili jambo limefanya Kenya iwe na amani.Pia Mzee Msekwa amenukuliwa akisema kuwa na sisi tunahitaji kuwa na kitu kama hicho.Haya maneno ya jaji mkuu yanaonekana kama ni jitihada ya kufanya chaguzi zetu ziendelee kuwa sio za huru na haki.
 
Uhuru wa kupokea amri za magufuli ??? Na kwanini jaji uanze kuongea haya yote saa hizi ? Inaonyesha unavyo msafisha aliyekuteua ! Siusubiri kesi zije mbele yako? Au kuna kesi kwenye vyombo vya habari na mitandaoni !!! tukifananisha si sisi wewe unalinda nini ktk ufananishaji huo,ili kisijulikane ?kwanini ujitetee sana,sisi sindio tunapima na kuona Kenya na sisi tofauti iko wapi ? Hapo unawatafuta walio ongelea Nairobi,ili uwafunge ! Ikiwa mwanasheria mkuu wa serikali alizuia mazishi /msiba wa Mawazo,tutakosa kulinganisha Kenya na Tanzania,msiba tu wampizani unakua issue ya kitaifa,badala ya kusaka walio muuwa sheria iwahukumu,mnamnyanyasa marehemu,Lisa tu wauwaji ni ccm na marehemu ni Chadema !!! Tena na jipoliccm kubwa la mwanza na migwanda yake nalo,Linasambaratisha waombolezaji,huu kama sio ujuha ni nini ?alafu kabisa mzee jaji,unatoa kauli yenye ugwadu kama hii ??? Mzee jilindie heshima yako,kabla hujafika mbali.utadharaulika sasahivi ! Magufuli ni msiasa wewe ni jaji atakuchafulia heshima yako.ni ushauri tu bila shuruti.usinitumie policcm bure, niletwe na wilibaro kisutu !!
 
Back
Top Bottom