Hii imekaa vizuri kabisa. Msajili ni mamlaka kamili ya kusimamia vyama na kama chama hakifuati sheria ana mamlaka ya kukirekebisha au kukataa maamuzi yaliyo kinyume cha sheria bila kujali sura ya mtu!
Kama Mungu ndiye aliyeumba mbingu na pia hii dunia, na kama Mungu siyo mmoja basi kila Mungu angekuwa amejiumbia dunia yake na mbingu yake na angekuwa na waumini wake katika dunia yake na mbingu yake.
Acha uvivu wa kufikiri. Serikali haishindwi kufanya vitu vingi kwa mara moja. Ina rasilimali nyingi ikiwemo rasilimali watu. Kwa mazoea ya serikali zilizopita kukosa utekelezaji basi unadhani kila kitu hakiwezekani hiyo siyo kweli na ni mtazamo wako tu hasi. Acha Bulldozer lifanye kazi na ole...
Kwani hekima ni nini? Inategemea na tafsiri ya kila mtu na mazingira aliyopo. Hekima kwa mwingine siyo lazima iwe hekima kwa kila mtu. Tusidanganyane. Ni mtazamo tu wa kila mtu na kila mtu yuko huru kufikiri atakavyo. Watu wanategemea wanyenyekewe hali wao hawana unyenyekevu wowote. Lazima...
Acha uongo kila mtu anajuaje CUF walishinda wakati kura hazikuhesabiwa zote na tume haikutangaza matokeo? Mtu kujitangazia kuwa ameshinda ndiyo unataka kuaminisha watu kiupotofu kuwa CUF ilishinda? Endelea kuota ndoto bandia ambazo hazitakuja kutimia.
kwani bendera ni ya jeshi peke yao? ni bendera ya taifa, hivyo desturi ya kuheshimu bendera yapasa kuwa kwa wananchi wote. Na kuheshimu bendera kunadhihirishwa kwa kufuata itifaki zilizowekwa kwa ajili hiyo na kukubalika katika taifa husika na kwa kufuata misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa...
Mbona hujaweka ushahidi wa kuonyesha kuwa serikali imelazimisha benki kukanusha? unapotosha kwa kuandika hisia zako binafsi na kutafuta ziwe ukweli kumbe ni uongo mkubwa!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.