Tafadhali naomba anayefahamu vigezo vya kujiunga na Kidato cha 5 atuwekee humu jamvini.
Tovuti ya wizara ya elimu inaonesha kuwa wameshatoa vigezo lakini ukifungua link husika unakuta ni Barua Na. 1 ya mwaka 2013 inayohusu ongezeko la gharama za ukaguzi.
Sijakuelewa una maana gani ukisema hawa ni sawa na 2012. Mwaka 2012 hapakuwa na B+ na Div I ilianzia pointi 3-9 lakini mwaka huu inaanzia 3-7, vitu vingi ni tofauti sasa huo usawa ni upi hapo. Unajitesa bure kutetea u....zi wakati kila aliye na akili timamu anaona kabisa kuwa NECTA...
Big results Now itatumaliza kabisa kwa staili iliyotumika kupanga motokeo mwaka huu ni vigumu kuyaamini. Hivi Prof Mukandala bado ni mwenyekiti wa NECTA?
Mkuu nimekuelewa kuwa zamani hata waliokuwa wanapata F zote walikuwa wanaenda A-Level isipokuwa kwa kundi hili walianza kuchukua wale wenye ufaulu wa kuanzia C tatu ndiyo maana wamefanya wonders!!!
Watu walikuwa hawamwelewi mama Joyce Ndalichako lakini kwa hali ilivyo sasa wameshaanza kumkumbuka kabla hata hajamaliza mwaka tangu alipong'oka pale NECTA. Ukweli kama una mapenzi mema na nchi hii huwezi kufurahia hata chembe kinachoendelea kwenye sekta ya elimu eti kwa kivuli cha BRN
Mkuu mama Joyce alikuwa na mchezo gani? Mie nilidhani kiwango kimepanda kwa sababu mwaka huu alama za madaraja yote kuanzia A mpaka D zimeshushwa sana na ndiyo maana hata idadi ya pointi za I hadi III zimebanwa sana maana kama I ingebaki pointi 3-9 basi waliopata I wangeweza kufika asilimia 50
Kwa nujibu wa gazeti la habari Leo la tarehe 26/6/2014 NECTA itakua inatumia alama za mithani ya Mock kama CA kwenye mitihani ya Kidato cha Nne na Sita.
Je, hii imeakaaje? Maandalizi ya MOCK yanafanyika katika mazingira ya kuaminika kiasi ambacho NECTA ichukue hizo alama na kuziunganisha na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.