Wacheni unafiki. Kwani kuna wakati ufisadi ndani ya ccm uliisha? Trilioni 1.5 zilizopigwa mpaka CAG akatimliwa ilikuwa awamu gani? Au kwa kuwa zilikuwa zinapigwa watu wamefungwa midomo na kuimbishwa mapambio ya kijinga ya kuunga mkono juhudi, ndo mnajitoa ufahamu kuwa wapigaji wamerudi kwani...
Isaya 34
16 Tafuteni katika kitabu cha Bwana mkasome; hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapana mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa changu kimeamuru, na roho yake imewakusanya.
Umechelewa kutoa maoni maana kanuni za uendeshaji wa ligi zimeshapita. Ungekuwa na akili inayoona mbele ungeliliona mapema na siyo kusubiri limeshatokea.
Kumbuka kuwa sheria inayotungwa kwa sababu ya tukio fulani huwa haitumiki kulihukumu tukio hilo, bali hutumika kwa matukio kama hayo...
Ujinga tunao tena si kidogo. Wewe uliona wapi mambo haya katika nchi zingine? Utozwe kodi ya mapato, utozwe kodi kwenye kila bidhaa unayonunua, kisha utozwe tozo kwenye miamala ya mitandao halafu wakufuate mpaka kwenye pesa ambayo waliikata kodi siku ulipolipwa mshahara, halafu wewe unakenua...
Utopolo hamnaga jema. Kutwa kucha kama wanga kushupalia ya wenzenu na kutia choncho kwa yasiyowahusu. Huo uwongo wako mimi naukanusha kwa kuwapa habari za kweli kwamba sababu ya jezi kuchelewa ni kuzirudisha kiwandani kubadilisha nembo ya mdhamini maana tangu mwanzo simba ilijua itamalizana na...
Imenichukua dakika kadhaa kufikiri kama mwandishi anaishi Tanzania. Baadaye nikagundua kuwa huenda anatafuta uteuzi ili kuganga njaa. Any way katika msafara wa mamba kenge hawakosekani twende tu hivyohivyo lakini tusisahau ule msemo wa wahenga kuwa kila mchuma janga hula na wa kwao.
Chama Cha Mumiani mabwege sana. Wanatamani kumpindua hata Muncu ili wao ndo waabudiwe na viumbe vyote. Hivi hawajatosheka na kununua madiwani na wabunge wa upinzani badala yake, hata TLS nayo inawatoa udenda???!!!
Swali hilo halijibiwi kiuanaume bali kiimani. Mwabadamu amepewa kuyatawala maumbile na siyo maumbile kumtawala. Kwa hiyo unapowaza kuwa na wake wengi kwa dharura, dharura hiyohiyo ifikirie kwa mke au wake zako. Hapo ndipo linapokuja swalia la kujitoa, kujikana nafsi na kuutiisha mwili.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.