Nilidhani ni mimi pekee nimesikia hii. Kama na ninyi mmesikia, inaonyesha kuna chembechembe za ukweli kwa kiasi fulani juu ya uwepo wajambo hili.
Naamini humu wapo ambao, either wameathiriwa na jambo hili, au kushuhudia na kupata maelezo ya kina juu ya jambo hili.
Imani hii ipo sana, mimi nimekuwa nikiisikia zaidi kwenye makabila ya wapare.
Tusubiri tusikie na wengine wanasemaje?
Nilishuhudia mke akiachwa, kwa madai ni mlango wa nane.
Nahisi kuna kitu kwenye hili. Ningependa nijifunze kuelewa hili jambo kwa mapana yake.
Hizi story nimekuwa nikizisikia, kuna watu kwenye maisha yaki wakiingia, utaandamwa na mikosi na hakuna ufanyalo ukafanikiwa. Kama ulikuwa na mali, basi utapukutika zote kiajabu kabisa.
Je umewahi isikia hii, unachochote tukajuzana zaidi juu ya hili.
Karibu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.