Huwa napata taabu kujua kama watu wanaelewa tatizo la tra Kwenye hili jambo. Tatizo sio tra kuweza kuona akaunti za watu/kampuni, tatizo ni kutangaza kilichopo huko. Kwa sababu hicho sio kilichowapeleka huko. kwa uelewa wangu walitakiwa kuishia walipo sema hawajaona akaunti yoyote anayomiliki...
Haya mambo ni kama ilivyo kwenye tafiti. Huwa tafiti zinapingwa kwa tafiti. Nilitegemea kama great thinkers tungemjibu prof Kwa maandiko kupinga maandiko aliyoyataja kwenye post yake kuliko kumshambulia bila msingi wa kimaandiko.
Wakati mwingine michango ya humu :( inatupa picha kubwa sana ya namna elimu yetu inavyotutayarisha kama mazuzu tusioweza kuhoji. Wakubwa wakisema jambo hata wanataaluma husika wanahangaika kulitetea hata kama ni la kijinga.
Nilisema mahali kwenye kesi hii kwamba there is something wrong somewhere kweye mifumo yetu utoaji haki. Haiwezekani kesi ya kijinga kama hii dhamana yake ikawa ni issue kwa muda wote huo.
Ni sawa umechangisha michango ya harusi inafika siku ya harusi unageuka na kusema nimegundua sina nyumba ya kuishi Kwa hiyo michango naenda kununulia kiwanja !!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.