Ni kweli. Ila huwa ni burudani sana ya roho pale unapojua kuwa kuna mtu anakuchukia na anajua wewe unajua halafu unaonesha upendo kwake. Nakuhakikishia baada ya muda fulani: 1. Atashangaa 2. Atakukubali 3. Atakuheshimu na 4. mwisho lililo bora mtakuwa marafiki.
Sawa. Ila ulionesha kuwa amekukera.Ukaendelea kuelezea hulka yake, na sasa bado unaielezea.Ulifanya vizuri kusaidia wahitaji wakati ukiwa tajiri.Ulifanya kitu kingine mbali na hili unalofanya sasa. Ulitenda wema. Sasa unaua. Umeambiwa usiue. Wewe unaua.Unaua nafsi. Unamtangaza vibaya huyu mama...
Unasema hujawahi kumdharau mtu kwa sababu hana.Kisha unasema huyo jamaa amekabidhiwa tu nyumba asimamie.Hauoni hiyo hali ya kukabidhiwa maana yake hana? Hivyo umemdharau kwa sababu hana. Naona umeanza kuwadharau watu baada ya kuwa masikini.
Ni kutokumsalimia.
Ajibu asijibu wewe mpe salamu.Timiza wajibu wako.Yeye akitenda ovu nawe unamlipa ovu?
Kuna dada mmoja mtaani kwetu mwanzoni nilikuwa kila nikimsalimia alikuwa hajibu.Mimi niliendelea kumsalimu.Nikimkuta namsalimu yeye, kisha nikikuta watu wengine nyumba inayofuata ninawasalimu...
Muda wa mwezi mmoja ninaona ni mfupi.Pia ni muhimu kuwa chini ya mwalimu maalumu.Kuna baadhi ya matamshi ya maneno yanafanana lakini maneno yanaandikwa tofauti na matamshi (mchangiaji mmoja ameeleza hapo juu). Napendekeza:1. asome kwa miezi mitatu, 2. Aende British Council kwa mafunzo hayo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.