Hapana msihukumu mapema hivyo wacha CAG afanye kazi yake. Hakuna safi Tanzania hii hata huko mlipo ni taabu. Kutoa taarifa amabazo hujafanyia uchunguzi wa kina waweza kupata shida mwisho wa siku
Ndugu zangu siyo kweli mnachoamini hapo. Dkt. Mwakwembe anamaanisha hivyo anavyomaanisha. Kama amekataa kuhusu UDA, yawezekana siyo chombo ambacho kimo ndani ya wizara yake. Mbona Vyombo vingine vimeainishwa katika taarifa na bajeti ya wizara yake na kwa nini isiwe hiyo. Unajua watu...
Shareholder ni mtu yeyote yule anaweza kuwa ili mradi kuwe na "invitation to subscribe shares". Kama prospectus ilitangazwa publicly basi hata wewe ungeweza kununua na kuwa shareholder, so sioni kwani tukaze misuli kwa Ridhiwani, yeye mtu kama wewe. Pia pata nafasi ya kufuatilia kuhusu mpango...
Ndugu zangu tuwe wakweli daima wala tusiwe na mtazamu hasi wakati wote. Kama ulimsikiliza vizuri Dr. Mwakwembe kila mradi alioutaja ambao upo katika utekelezaji alionyesha timeframe yake. Pia, miradi mingi ya kufufua engine za treni na mabehewa imefanyika jambo ambalo halikuwepo kabla yake. Sasa...
Serikali gani tena hiyo ifanye hivyo wakati Dkt. Magufuli alishapiga marufuku kuweka mabango barabarani ila wananchi wakaandamana hadi kwa waziri mkuu na pia meya wa jiji (Silaa) naye akapiga kelele hadi mzee pombe akaishiwa nguvu. Mawaziri hawana meno na yakiota tu wananchi tunayang'oa kupitia...
Ajali ni jambo la kawaida katika maisha ya mwanadamu hasa ukizingatia mada kuhusu msaada kwa wanaopata ajali za barabarani. Kuondo ajali ni njambo gumu labda kupunguza lakini ujue kwa hata askari wa usalama barabarani wakifanya kazi kwa makini ndo madereva wanakuwa wa kwanza mara kugoma na...
Mheshimiwa hebu eleza cdm itafanya nini na siyo kuisema tu ccm. Hiyo ndiyo namna watu wanavyoikataa cdm. Mtaishia kusema kumbe kutenda hamjui. Hata wewe uliahidi ubungo pia ila bado kero kibao
Kila mtu anayo haki ya kuogombea uongozi ila mradi anazo sifa zinazomruhusu kufanya hivyo. Mbona hukusema kwa wengine Hussein Mwingi, Makongoro Nyerere, Kawawa, Kighoma Malima na hata kule USA unasemaje kuhusu George Bushi na hapo Kenya Uhuru Kenyatta. Hata wewe ukiingia katika uongozi haina...
Ni kweli LAPF ni mfuko bora kwa walimu. Ukokotoaji wa LAPF una unafuu kwa mtumishi kwani huchangia 5% kati ya 20% na mwajili wake huchangia 15%. Hivyo una mzigo mdogo kwa mtumishi ukizingatia mishahara ya walimu wetu
Ndugu zangu tusiwe na perception za aina hiyo. Kuwa na kikao ni jambo la kawaida kwa chama au hata kikundi. Yawezekana wakajadili jambo la kawaida tu na kwa manufaa ya taifa. Tusifike mbali kimawazo mara zote kuwaza jambo baya hata zuri pia tuwaze.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.