Naomba serikali itukumbuke na kutuzingatia. Ni mwalimu wa kujitolea nafundisha shule ya sekondari. Huu ni mwaka wa Tano naingia tangu nilipoanza kufundisha kwa kujitolea.
Natembea kilometa 10 natumia masaa mawili kwenda na mawili kurudi Kila siku. Nafanya hivyo kwa kuwa naipenda kazi yangu...
Waomba ajira huumia sana wakati majina ya waliopata ajira yanapotoka. Unakuta tangazo la ajira lilikuwa linataka wanaotakiwa kutuma maombi waliomaliza kuanzia 2012 had 2019 lakini utakuta baadhi ya waliopata ajira wamehitimu 2020 had 2021 na waliomaliza ndani ya miaka husika wamekosa.
Serikali ingefanya mpango wa kuwapa boom la mtaji kwa wanohitimu vyuo vikuu. Baada ya graduation graduates wote wapewe boom la kwenda kuwasaidia kuanzia maisha mtaani.
Hii ingesaidia kujiajiri kwa vijana punde baada ya kurudi mtaani.
Serikali imejenga shule nyingi mpya. Ambacho hakijanipendeza ni kuona inawapa nafasi walimu waajiriwa kwenye hizo shule lihali walimu tusiokuwa na ajira na tunajitolea mwaka watatu sasa hatupewi fursa. Ushauri wangu serikali itutazame kwa jicho la tatu tunaojitolea maana moyo wa kujitolea...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.