Recent content by Mtoboa siri

  1. Mtoboa siri

    Ulishawahi kujilaumu kwa kufanya starehe ya muda mfupi yenye madhara makubwa kwako?

    Mkuu hii story yako nakumbuka pia uliiweka kwenye uzi wa "Mkasa upi ulikufanya ujute sana" Nilicheka sana nilipoisoma na leo nimeikuta hapa ni kama umenitonesha kwa kicheko..
  2. Mtoboa siri

    Benki ya Ethiopia yawataka waliochota fedha ATM baada ya mtandao kuharibika warudishe

    Iliwahi kutokea kwenye benki moja hapa Tanzania ambapo na mimi nilikuwa mmoja wa wanufaika mwaka 2017. Nilikuwa na shughuli za ujenzi nikamaliza hela yote kwenye account, nashangaa naulizia salio linasema kuna Milioni 8. Nikaona bahati ilioje hii, nikatoa milioni moja nyingine nikaziacha kwa...
  3. Mtoboa siri

    FBI walivyomdaka Thomas Lyimo 1998. Hata kama huwapendi wamarekani, basi tuwaheshimu tu

    Naomba ui-tag hapa hiyo thread nyingine inayofanana na hii.
  4. Mtoboa siri

    Tuishi na wanyama vizuri: paka wangu kaua nyoka jioni ya leo, bila yeye nyoka angekuwa ndani ya nyumba na lolote lingeweza kutokea

    Ilikuwa kijijini kipindi cha njaa, mwenyenyumba alienda shamba kurudi akakuta paka amekula mboga alioitegemea na hakukuwa na mboga nyingine.
  5. Mtoboa siri

    Tuishi na wanyama vizuri: paka wangu kaua nyoka jioni ya leo, bila yeye nyoka angekuwa ndani ya nyumba na lolote lingeweza kutokea

    Nilisimuliwa na mtu ninaemuamini, ila muhusika hakufa lakini alijeruhiwa sana usoni. Na pia nilisoma sifa za paka. Ni kiumbe hatari anapotaka kujihami kutokana na hatari iliopo mbele yake.
  6. Mtoboa siri

    Tuishi na wanyama vizuri: paka wangu kaua nyoka jioni ya leo, bila yeye nyoka angekuwa ndani ya nyumba na lolote lingeweza kutokea

    Paka anaweza kukuua hata wewe mkuu, kama unabisha funga mlango na madirisha yaani kusiwe na mahali pa yeye kutoka halafu mkate mkia.
  7. Mtoboa siri

    Sultan Tamba na Mussa Banzi Chukueni maua yenu japo bado tunawadai muendelezo wa baadhi ya filamu. Kanumba alichangia kuua soko la filamu

    Sultani Tamba movies zake ziliegemea vitisho zaidi ila Mussa Banzi alikuwa anapiga kotekote mapenzi na vitisho. Kuna movie ya Sultan Tamba inaitwa Wasiwasi, wanaume wawili wanagonga mlango usiku wa manane, mlango ulipofanguliwa wanauliza wapi kuna msiba. Aliefungua mlango anashangaa na kusema...
  8. Mtoboa siri

    Taarab: Special thread

    "Wanaume tumepewa daraja kubwa kwa Mungu, mashababi tumekuwa na kila aina ya mizungu" Wimbo V.I.P- Jahazi (Mzee Yusuph)
  9. Mtoboa siri

    Taarab: Special thread

    Uswazi enzi hizo kwenye sherehe za kukesha na muziki tuliita vigodoro nyimbo za taarab zilichukua nafasi kubwa sana. Ndio zilizomtoa Msagasumu. Na ndio nyimbo zilizozaa singeli kutokana na kuweka machombezo katika wimbo wanaita radha.
  10. Mtoboa siri

    Mtu hawezi kufa akafufuka, Stori za Watu waliokufa kuonekana ni uongo, na zinafanana kwa asilimia kubwa

    Mtaa wa Manzese Beston kuliwahi kutokea na mkasa kama huo, kuna kijana alikuwa mwizi alieshindikana. Ukapita muda mrefu bila kuonekana nyumbani kwao, zikaja taarifa kuwa ameuwawa kwenye tukio la wizi na mwili wake umehifadhiwa chuma cha maiti. Ndugu zake walivyokwenda hospital ili kuutambua...
  11. Mtoboa siri

    Nimepona bawasiri; Asante Mungu

    Ukiacha dawa za Hospital, dawa kubwa ya asili ni kuyakalia maji ya uvuguvugu yaliyo kwenye beseni yaliyochanganywa na chumvi nyingi kila siku kabla ya kulala kwa siku tano mfululizo. Unapona kabisa.
  12. Mtoboa siri

    Hivi mtu unafelije somo la hesabu? Zero brain kabisa wanafunzi wa siku hizi

    Ni muda mrefu zaidi ya miaka 25 toka nimalize darasa la saba ila nina uhakika hata leo hii ukinipa mtihani wa Taifa wa Hisabati darasa la saba napata A. Tena kwa mitihani ya miaka ya sasa majibu ya kuchagua na maswali mepesi ndio kabisa. Enzi zetu kipindi tunakutana Tuition na mitihani ya...
  13. Mtoboa siri

    Watu hukiri kwa vitendo: Kumfunga Simba ni kufunga dude kuubwa sana

    Kwa mtazamo wangu, Wanafanya sherehe sio kwa sababu wamemfunga Simba ila wamemfunga kwa idadi kubwa ya magoli ambapo ni nadra kutokea na huchukua zaidi ya miaka kumi kwa Simba na Yanga kufungana kwa idadi kubwa ya magoli. Kipindi cha nyuma Simba alishawahi kumfunga Yanga kwa magoli mengi na...
  14. Mtoboa siri

    Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?

    Habari wadau, kuna wimbo uliombwa na mdau muda kidogo nimeshindwa ku-tag comment yake ila wimbo nimeupata. Wimbo unaitwa maisha kigeugeu wa bendi ya MCA International wana MUNISANDESA. Ni wimbo wa dansi wa zamani nakumbuka ulitoka mwaka 1991. Kama mtakumbuka haya mashairi "kwani maisha ya sasa...
  15. Mtoboa siri

    Ushauri: Tunza MSG za Miamala ya Fedha, Ningelala Selo leo

    Hata kama ungefuta hizo meseji ungesumbuka tu kukaa polisi na ukapata dhamana. Upelelezi ungeonyesha pesa alipokea. Hata kesi ingepelekwa mahakamani ungeshinda asubuhi tu. Kilichokusaidia ni kuepuka usumbufu tu. Pesa ya kupewa ambayo unaweza kuikana ni ile ya mkono kwa mkono tu na si vinginevyo...
Back
Top Bottom