Kwa kulisaidia Taifa naomba kushauri kwamba hawa viongozi wetu wanaposafiri kwenda nje ya nchi watumie Economy Class badala ya kutumia Business class, na hapa nyumbani usafiri wa Ma-vx tuwabadilishie na kuwapa Suzuki Vitara ambazo hazina bei mbaya.
Uchaguzi hata ukirudiwa mara 10000000 bado CCM itashinda, na sababu kubwa ni kwamba hatuna tume huru ya uchaguzi hapa Tanzania. Tume iliyopo itafanya madudu yaleyale iliyoyafanya kwenye uchaguzi feki uliopita.
Davis Mosha ni kijana mwema sana, alikuwa na mipango mizuri sana na moshi mjini. Alitaka kuijenga Moshi iwe kama Dubai, lakini bahati mbaya wapiga kura hawakumuelewa na wameamua kumuweka pembeni.
Mimi na Nape tunatofautiana kiitikadi kwa kiasi kikubwa sana, lakini nimesikitishwa kusikia amepata ajali. Ninampa pole na ninamuomba Mungu Baba amponye haraka pale alipoumia ili aweze kuyakabili majukumu yake ya kila siku.
Kwa bajeti uliyonayo kupata mashine nzuri ni ngumu sana. Ninafanya biashara hiyo ya kununua mashine za kilimo na kujengea barabara hapa UK na kuzileta Tanzania. Kwa msaada zaidi ni PM
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.