Umesema kweli kabisa yani ukiingia Dar cha kwanza ni harufu za hovyo za uchafu mitaro michagu imekua kero watu wanachuruzisha maji machafu yanayotuama kwa muda mrefu
Kwa kuongezea msipende kuomba msaada kwa mtu usiye mjua unapokua kwenye ATM Kama hakuna mtumishi wa benki bora ukaingia ndani kuomba kusaidiwa kama umekwama kutumia kadi yako matapeli wapo wengi kwenye ATM Wanavizia ujichanganye tu wanakupiga tukio
Wakati mwingine uchumi ni tatizo unataka umpe pesa ukicheki mfukoni unabalance ya mkate tu kwa mangi unaitoaje si kila anayendesha gari anaweza kuwa na akiba mfukoni.mbaya ni kumtukana na kumdhalilisha.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.