Binaadamu tunajisahau sana kama sio kujitoa ufahamu. Twajiona tuko sawa ktk kila kitu. Busara kubwa kwa mwenye hekima ni kusikiliza na kumueleza anayekushauri kuwa hapa sikuwa na maana hiyo mliyoifikiri,nilikuwa na mtazamo huu. Unaweza ukamshawishi ata aliyekushutumu akabadili maono na kutengua...
Duuuuh,asante sana mkuu. I salute you. Najiona kama nipo ukumbini nawaona wakongwe wakifanya yao enzi hizo muziki umeshika hatamu. Kuna haja ya kuwa na jukwaa letu la kupeana mavitu ya enzi hizo kma haya.
Asante sana mkuu kwa kumbukizi muruwa kabisa. Inaelekea Madilu ni alikuwa anatembelea sana nyota ya Franco baada ya kifo chake maana naona karibu nyimbo kadhaa za Franco kazifanyia remix. Naomba baadae utuwekee uhusiano wa hawa jamaa wawili Madilu na Franco. Na vp kuhusu Tabu ley na Mbiliabel...
Nimekuelewa mkuu,lengo langu lilikuwa kukuonyesha ulipo-mark M kwenye jina la raisi wa kwanza siko. Ni sawa na kusema jina la Dr. J.P.Magufuli lina herufi D ndani yake. M niliyoitarajia kwenye hilo jina ni kutoka kwenye jina la kati la Kambarage na sio Mwalimu. Ila umeeleweka mkuu.
UDSM kwa sababu naamini ndio chuo kikongwe kilichoanza kutoa elimu ya siasa nchini. Ata mfumo wa vyama vingi ulipoingia nchini nilitaraji watuandalie wataalamu ambao wangeenda kutuelimisha ipasavyo nn maana ya huu mfumo ktk uendeshaji wa nchi. Zaidi ya hapo maelezo yako mengine nimeyakubali na...
Kwa hali inayoendelea sasa nchini nachelea kusema UDSM mna kila sababu ya kubeba lawama juu ya uelewa wa masuala ya siasa uliopo nchini.
Dhana inayojengwa ya kuwa ukiwa upande fulani wa sarafu wewe ni wa kuunga mkono na ukiwa upande mwingine unakuwa wa kupinga ni dhana mbaya kwenye mfumo wa...
Tena mkutano uliohudhuriwa na PM. Nadhani ilitosha kwa PM kumuwakilisha yy kama Amir Jeshi aje kutoa heshima na kuwapa neno la faraja majeruhi, familia na manusura wa mkasa huu mkubwa uliotupata.
Tukumbuke kuwa Mh. Raisi alitoa ahadi hadharani akisema mwezi huu anaanza kurudisha utaaratibu wa nyongeza ya mwaka ya mshahara. Watumishi tarehe zetu ndio hizi zinayoyoma vp huko kwenu kuna lolote jipya.
Ndio wajibu wake, watu wangeongea kama hasingeonekana tena safari hii. Ni wajibu wa katibu mkuu wa chama kuwepo kwenye vikao vya juu vya chama. Hasipoonekana kwa sababu zisizo na mashiko ndipo huzua maswali na hayo maneno unayoyasema.
Najitahidi kuwaza kwa sauti kuhusu yule Askari aliyepayuka kwa sauti na kufyatua risasi hewani akujua anatekeleza majukumu yake kama ambavyo alikuwa akisikika akisema "Kwa nini hauheshimu bendera, nimekunywa maji ya bendera mimi" na akaungwa mkono na kamanda wake kwa maana ya mkuu wa kazi na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.