umeanza vizuri kujenga hoja zako, hongera kwa hilo. Lakini unajaribu kutuaminisha Wamasai siyo watanzania ni wakenya hapa ndipo wasiwasi wangu unapoanzia. Tujengeni hoja zetu kwa namna yoyote ile lakini tusithubutu kuukana utanzania wao kwa kuhalisha hoja zetu
Kuwa wapenzi siyo utetezi wa kumuingilia mtu kinyume na maumbile. Hata kama angekuwa mke wake hairuhusiwi kisheria. Pia, kwa mjibu wa maelezo ya binti, Rc alimuingilia kinguvu (alibaka).
Kheri za mwaka mpya wanajukwaa!
Nimeona na mimi kama mtanzania niungane na CDF kutafakari kwa kina hali ya ulinzi na usalama nchini.
Naomba niingie moja kwa moja kwenye mada yangu kama inavyojieleza. Ulinzi na usalama wa taifa ni jambo la muhimu kuliko kingine chochote kwenye taifa letu, na...
Nakubaliana na wewe mkuu, kunafukuto lingine liko huko mkoa wa Simiyu, polisi wameua kijana mmoja lakini viongozi wanatumia nguvu kubwa kufunika mwanaharamu apite, ni wiki sasa ndugu nao hawataki kuzika mwili wa mpendwa wao.
Naomba niingie kwenye Mada moja kwa moja.
Kutokana na malalamiko ya wananchi kutendewa unyama na jeshi la polisi sehemu mbalimbali za nchi, kama vile raia kuuwawa vituo vya polisi, raia kubambikwa kesi n.k.
Napendekeza kiundwe chombo kingine cha kuchunguza jinai zinazofanywa na jeshi la polisi...
Tupunguze kujadili hoja kwa jazba hili ni taifa letu sote. Magufuri alikuwa rais wetu sote (Mungu ampumzishe salama) kuna mambo mengi mazuri alifanya, lakini kunavitu alifanya havikuwa na tija kwa taifa.
1. Uwekezaji alioufanya Chato ni mkubwa kuliko eneo lenyewe. Air port chato (wrong place...
Kahama ni sehemu nzuri sana kwa biashara!, siyo kweli kwamba uchumi wa Kahama unategemea Buzwagi. Kama ni mji ambao uchumi wake unategemea vitu mno. Lakini madini ndo yanaongoza, pia wachimbaji wadogo kutoka maeneo jirani ndo wanaukuza mji na siyo Buzwagi.
Kumshauri kiongozi mkuu ndo kazi ya waziri na kufanya hivyo siyo kumpinga. Mimi nadhani watanzani tunatakiwa kubadilika sana. Nidhamu ya uoga ndo chanzo cha matatizo yetu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.