Hakuna tusi hapo. Hivi zile Nyaraka za Dini zilizokuwa zinatoka siyo wao walikuwa wanazitoa? Nini kimebadilika kwenye siasa za Tanzania toka wakati ule na sasa?
Nilitegemea kuona watu wakiweka vifungu vya sheria inayowaruhusu Basata kufungia kazi za wasanii nje ya mipaka ya Tanzania. Badala yake naona watu wanaongea hisia tu. Nchi inaendeshwa kwa sheria na siyo mtizamo wa watu. Wenye uelewa wa sheria wasaidie hapa.
Chaguzi ndogo zikifanyika kwa uhuru huo ccm wangepata kioo cha kujitizamia. Kwa sasa hata wao hawana uhakika kama wanaungwa mkono na "viongozi" wanaojiuzulu au kuna wananchi ambao wako nyuma ya "viongozi" hao pia.
Uwepo wa Bunge hili hauna impact kwenye maisha ya Mtanzania. Hata lisipo kuwepo maisha yataenda hv hv tu. Bunge limepoteza uwezo wake wa kuisimamia serikali.
Kwa kauli hii ya Mh Waziri naamini kuwa Lugumi atakuwa alilipwa kwa thamani ya Vituo 32 alivyofunga na siyo 108. Hela ya kufunga vituo 76 bado ipo kwa ajili ya kukamilisha zoezi pale serikali itakapoweka vizuri mazingira ya kufunga.
Tofauti na hivyo bado kuna harufu ya wizi.
Etwege,
Nguvu kubwa inayotumika kwenye hizi chaguzi ndogo dhidi ya Upinzani kwa kutumia vyombo vya dola hususan Tume ya Uchaguzi na Jeshi la Polisi inadhihirisha kuwa Wanaounga Mkono Juhudi za Mh. Rais ni viongozi husika tu na siyo wananchi.
Kuondoa Fao la Kujitoa ni Dhuluma kwa Wafanyakazi. Hii ni Indirect Tax baada ya Paye (Double Taxation) kwa maoni yangu.
Serikali inatumia fedha nyingi za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kufanya shughuli za maendeleo na hatimae kushindwa kuwalipa mafao yao wastaafu. Sasa wanatumia sheria kuzuia...
Ni wazi serikali ilitaka kuwarudisha hao wafanyakazi baada ya kugundua walikurupuka hapo awali. Ili isionekane kuwa serikali inajichanganya ikabidi kutumia bunge kuhalalisha mpango wao.
Akili ndogo inapopewa nafasi tatizo linakuwa kubwa badala ya kuongezeka.
Ukuangalia list ya watu 10 waliotajwa na Musiba utagundua ni watu wa mtazamo flani. Hakuweza hata kuchanganya watu tofauti ili kuweka angalau legitimacy ya hoja yake.
Siku hizi kuna "Watu wasiojulikana" ambao tayari tumeona...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.