Utafiti sahihi wa kukubalika ni kupitia sanduku la kura. Sasa nenda kwa hao wana CCM kawaambie wakubali uchaguzi huru na wa haki ili tuthibitishe hicho unachodai ni itafiti wako. Waambie polisi wakae mbali na masanduku ya kura tuthibitishe hicho unachokisema.
Rais Samia, umefeli sana sana sana, unajiwekea record mbaya sana, dalili zinaonyesha kuwa ukombozi wa Tanzania na hasa Tanganyika utakuja chini ya utawala wako. Huwezi ukaanza kufunga watu na kuwabambikizia kesi ukabaki salama, haiwezekani labda Mungu hayupo.
Huwezi kulinganisha siasa za Tanzania na Kenya. Tamaduni zetu ni tofauti Sana. Tulikuzwa kwenye ujamaa, wenzetu kwenye ubepari. Wananchi TZ walilishwa uoga toka mwanzo wa Taifa, hilo limekuwa tatizo kubwa. Mara ngapi wapinzani wametoa wito wa kuandamana na wananchi wakagoma kutoka. Ni watanzania...
Kilicho nishangaza ni kuwa Mbowe alitumia nguvu kubwa mno kujitetea na kuwananga wanakosea amelamba asali. Ilitosha kuzungumza hilo kwa dakika tano na ikatotosha, lakini hilo lilichukua sehemu kubwa ya hotuba. Hilo linatuambia kuwa kuna kitu hakipo sawa.
Katika Biblia kuna wakati Nabii Samwel alikuwa anamwombea mfalme Saul, Mungu akamtokea na kumwambia kuwa wala asipoteze muda wake kumwombea kwa kuwa Mungu ameshamkataa. Hivyo ndivyo ulivyokuwa ama ingekuwa kwa Magufuli kama watu wangemwombea. Mungu alikwisha mkataa, huwezi kukiuka haki za wana...
Jambo moja umesahau ama umefanya makusudi ni ukweli kuwa Mbeya mjini wakazi wake sio Wanyakyusa, lile ni eneo la Wasafa na Wanyakyusa wamefanya kukarinishwa tu. Huko Tukuyu na Kyela ndiko kwa Wanyakyusa. Kuhusu mgogoro hilo ni jambo la muda tu. Je ulifanikiwa kupima imani ya wananchi wa Mbeya...
Labda nikuulize swali, Afica ya Kusini walipofikia makubaliano ya kuutokomeza ubaguzi wa rangi baada ya miaka mingi ya mapambano, ndani ya bunge lao kulikuwa na wanachama wangapi wa ANC? Hoja za ACT ni kama za vibaraka wa wakati huo. Shauku yao ni kuwa na uwakilishi bungeni hata kama ni kwa haramu.
Aliogopa kutaja umuhimu wa katiba mpya kwani hizo njozi zikiwekwa kwenye katiba hapatakuwa na mtu mwenye akili timamu (sio kama hayati JPM ama Ndugai) wa kuzipindisha.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.