Usisahau kutaja ushiriki wa Lowassa katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji mwaka 2014 ambapo alipata ushindi wa kimbunga wa asilimia 99.9 Huu pia muwe mnautaja!!
Unaonekana kituko mbele ya weledi unaposema Lowassa alipofukuzwa chama hakikutikikisika. Mwaka 2005 CCM ilishinda kwa asilimia 81 kiti cha urais, ila mara baada ya kumtimua Lowassa 2008 ukafanyika uchaguzi mkuu tena mwaka 2010 CCM ilishinda kwa asilimia 61. Hauoni kukosekana kwa kiungo imara...
Unaposema Lowassa ni fisadi una ushahidi wa ufisadi alioufanya au unabwabwaja tu? Ama unazungumzia suala la Richmond ambalo wabunge na Bunge imethibitisha ya kuwa haikulipwa hata sh. 1 kwa kampuni. Jifunze kufikiri walau kidogo
Haya maneno ya ugonjwa kuzushiwa wagombea hayajaanza leo kwani hata JK aliambiwa ni mgonjwa na hana siku chache atakufa leo hii ni mwaka wa tisa anadundikq. Afya ya mtu aijuaye ni Mwenyezi Mungu tu. Ila ukweli Lowassa ni mzima wa afya tele na nimetoka kuzungumza naye muda si mrefu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.