Ninasikitishwa sana na ukimya wa mamlaka kutotupa updates kama ilivyokuwa hapo awali. Hali hii ya 'covid-19 updates lockdown' ni hatari sana kuliko covid-19 yenyewe. Taarifa kwa wakati inafanya watu kuwa makini zaidi. Tafadhali mamlaka badilikeni. Tusiwe kama China au Korea kaskazini ambao...
Hivi, huyu anayejiita Mzee wa upako ana umri gani? Mbona anaonekana ni mtu mzima lakini anaongea kama vijana waliozaliwa '90 na kuendelea? Yaelekea hajui siasa na wanasiasa mwaka '95 ilikuwaje. Ndo maana hajui neno ukoma liliingiaje katika siasa mwaka huo. Kama angelijua asingezungumza upuuzi...
Asante sana. Kwa sababu hiyo ni haki kabisa ccm na watz kwa ujumla kumuenzi Mwl. JK kwa kumuogopa mtu huyu si kama ukoma bali kama Ebola kwani ndo tishio nyakati tulinazo.
Hivi huyu mzee wa upako mwaka '95 alikuwa na umri gani? Hayo anayosema ni kana kwamba alikuwa hajazaliwa au alikuwa...
Mtu anayeheshimika duniani, jabali la siasa Africa, mtu aliyerudisha heshima ya watanzania, Baba wa taifa, Mwl. J.K. NYERERE, mwaka 1995 alituasa watz kumwogopa kama ukoma mtu anayeitafuta Ikulu kwa kutumia fedha. Nani asiyejua uwekezaji wa EL katika kuutafuta urais?
Amewadanganya mkadanganyika. Gwajima hana hata leseni ya bajaj. Uendeshaji wa kilevilevi uliwafanya polisi wamhoji kwa masaa kadhaa baada kumkosakosa Kadinali Pengo, aliishia hospitali akiwa mgonjwa. Anawasema wengine kumbe yeye nae ni mlevi, mgonjwa na ameishaingia kwenye kumi nane ya uzee...
Siamini haya ni majibu ya Gwajima. Namfahamu Gwajima, haya ni majibu mepesi mno kutolewa na Gwajima. Kama ndiye, Gwajima ninayemfahamu, ameanza kupata akili, anaanza kuwa na adabu, ni mwoga. Chezea ccm.
Anza ufisadi. Fedha utakayopata changia harambee, wanunulie vijana bodaboda nk. Uwe na lengo na usiwe mchoyo. Nyota uitakayo itakuja juu yako. Ni rahisi.
Ni assests kwa maana ya kura kuongezeka kwa ccm endapo utajitokeza uchaguzi wowote ule. Pia sasa wamerudi ccm, bila shaka unafahamu kuwa wanachama na mashabiki ndo the most valuable assets ya chama chochote. Msindai na Mpendazoe karibuni sana ccm na pia mmemfahamu mpinzani vizuri na kwa undani...
Siasa si uadui. Cheyo na Mrema ni wanasiasa wapinzani wa kweli. Hao cdm ni wanasiasa wapinzani wenye uanaharakati, ndo maana wanazungumzia ukombozi wa taifa hili. Si ajabu BWM akawapasha.
Ingawa EL alisema wame graduate, mmmh bado, ana kazi ya kufanya. Havai gwanda wala hasemi neno kamanda, EL...
Lowassa si mwanaharakati, ni mwanasiasa. Hawezi vaa jezi hizo za uanaharakati. Alipo hapo anatamani wazivue hizo.jezi, alama ya uanaharakati na kuwa wanasiasa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.