Ni kanuni, miongozo, Sheria dhaifu hakuna mantiki yeyote! Mbona akaunti za benki kila mmoja ana yake sijawahi kusikia ukishindwa kuiendesha wanaigawa. Tigo waligawa namba yangu kwa mtu, walinikera hadi Leo siwapendi. Wavivu wa kufikiri kuchanganya namba mbona vocha hazijirudii!
Mzungu ni balaa. Juzi Makamu wa rais kazindua uwashaji vifaa vya usikivu kwa watoto 14 (cochlear implant) Muhimbili, wameshasetiwa vifaa ktk sikio ila hakifanyi kazi had kiwashwe kwa mawimbi, mfumo unaowasha kifaa hicho ni ambao upo nje mtu ana u control, so mtengenezaji si anaweza akazima muda...
Labda kama kuna foleni ndio utatumia muda wote huo. Au uwe mgeni kwa wenyeji wanajua ikiwa kama ni wikiendi hamana foleni G'mboto to Posta haizidi dakika 15
Kwa kifupi kinachofanywa ni uhuni. Si waunde namba mpya wampe mteja, kwani lazima ambayo imeshatumika? Wakitaka kujua namba zipi zipo active si system inaonyesha? Wenzetu wapo ktk teknolojia ya AI sisi bado tunagombania cheap.
Bora waseme ni mateso makubwa kuishi mjini bila umeme. Umeme unakatwa kama dozi ya Panadol. Kila siku, bora mkate mwezi mrekebishe, baada ya hapo mridishe. Nimewatusi Leo...
Ila Tanesco, Mungu anawaona. Ukonga Dar es Salaam, wamewakosea nini? Kila siku usiku mnakata umeme? Ratiba ya mgao imeegemea huku tu? Shirika hili ni kero jamani, too much.
Upo sahihi kwa mangi, muha, mgosi mtaani ndio mwokozi. Yaani super market ni kama eneo la anasa bongo, vitu Bei juu wakati wao wananunua kwa jumla madukani makuu au viwandani. Nchi za Kusini mwa Afrika wananchi wao wote wamezoea supermarkets nenda tu hapo Tunduma Mpakani ukivuka duka unakuta ni...
Hivi Tanesco ni lini mtaona Raha mkifanya kazi kwa weledi? Ratiba ya mgao hamtoi mnakata umeme mnavyojisikia nyie. Kwa nini hamuwi wazalenda kwa kuitumikia nchi yenu ipasavyo? Kutoa tu taarifa ya ratiba ni issue,Kitengo cha taarifa kinafanya nini? Mfano wiki hii maeneo mengi ya Dar mmekata umeme...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.