Shida ya ujinga, ukiwa nao huwa haujifichi. Umezunguka kote unachafua taasisi nzima kumbe lengo umharibie mwenzako anayehama? Unapata nini kwa kumchafua mtu bila ushahidi? Unanufaika nini? Mazingira yanaonesha una chuki binafsi na huyu mwalimu anayehama. Mlikosana nini? Kwa akili yako unadhani...
Kula kwenyewe hela. Umeingia humu kwa sababu una bundle (hela.) Tatizo ni kuthaminisha upendo na kiasi cha pesa anazopata mtu. Kumpenda mwanamke kwa vitendo ni kuonesha unamjali; kumfanya kipaumbele chako; kumheshimu; kumlinda na mambo kama hayo yasiyoweza kulinganishwa na fedha.
Nadhani kuna tatizo la wanaume kufikiri hitaji kuu la mwanamke ni fedha. Inawezekana wanawake nao wanachangia imani kama hii, lakini ukweli wanawake wanahitaji zaidi kupendwa kuliko chochote. Ukimpenda mwanamke kwa vitendo na ukamfanya ajisikie yuko kwenye mikono salama hawezi kuweka mbele fedha.
PICHA: Image Of 1Love
Katika kufanya kazi ya unasihi (counselling) na wanandoa wengi wenye mitafaruku ya ndoa, nimegundua mambo kadhaa. Kwanza, vijana wengi wanaingia kwenye ndoa wakiwa na maandalizi hafifu. Wengi wanatumia muda mrefu kujifunza mitindo ya ngono wakifikiri hicho ndicho...
UKIFUATILIA mazungumzo ya wa-Tanzania wengi kwenye mitandao ya kijamii, unaweza kuona namna watu wanavyojinasibu kujua. Mijadala mingi imejaa ‘ujuaji’ unaofanya watu wajigambe, wadhihaki wengine, watukane na wakati mwingine, kadri ya mamlaka yao, watake kulazimisha kile wanachokiona wao ndio...
PICHA: Verastic
Mwanamke, kwa asili yake, anajisikia vizuri kusema matatizo yake kwa mtu wake wa karibu anayemwamini –kama, mathalani, mume wake. Ile tu kujua kuna mwanaume yuko tayari kusikia yanayousibu moyo wake kunamfanya ajisikie salama.
Kutegemeana na aina ya tatizo, mara nyingi...
Tumezungukwa na watu wasio na tofauti sana na Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu. Akina Yuda wapo kila mahali. Wengine ni wafanyakazi wenzetu, marafiki zetu, waumini wenzetu, majirani tunaoishi nao na wengine ni jamaa zetu wa karibu. Pengine ni muhimu kujua namna ya kuwabaini ili uchukue hatua kabla...
Inakadiriwa kuwa kati ya watu 800,000 na 1,000,000 hapa nchini wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka. Hawa ni vijana wanaomaliza masomo yao kwa ngazi mbambali za elimu au wale wanaokosa nafasi ya kuendelea na masomo katika mfumo rasmi wa elimu.
Mfumo wetu wa elimu unachuja wanafunzi kwa...
Dorcas, msichana wa miaka 30 anayefanya kazi kama Afisa Mikopo kwenye benki moja mjini, hakuwahi kufikiri ingetokea siku moja ‘achepuke’ kimapenzi na Johnson ambaye ni mfanyakazi mwenzake. Miaka mitatu iliyopita wakati anaanza kazi kwenye benki hiyo, Dorcas alikuwa na msimamo thabiti na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.