Wenzetu hawako kama unavyofikiria, wanajali ukweli wa kazi yao na sio anayewalipa, na hii ndiyo sifa inayowatambulisha na kufanya kazi yao iheshimike na kukubalika dunia nzima.
Viongozi wetu wanafanya kazi kubwa kuuaminisha umma pamoja na wasiojitambua, kuwa ukitoa hoja au maoni yako na yakakinzana na watawala wetu,wewe ni msaliti wa nchi. Tuliokwisha jitambua tumevuka mtego huo, japo nikiri wengi bado wamenaswa.
Ukishakuwa na Uongozi usiothamini demokrasia, haya siyo ya kushangaza. Tunaoelewa mambo haya, tunajua yapo makubwa zaidi njiani. Wazalendo wote jifungeni mikanda tuone kama tutavuka kipindi hiki cha mpito.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.