Recent content by Hechy Essy

  1. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Uķipita site nyingi, utakutana na hili tatizo la mkanda wa msingi kuwa na level moja nyumba nzima. Mkanda wa msingi unaopita sehemu ya kibaraza unatakiwa uwe chini kwa kozi moja mfano kama msingi wako umejenga kozi 7, basi sehemu ya kibaraza jenga kozi 6 tu. Ramani, Makadirio au Ushauri...
  2. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Kabla ya kupiga ripu kuta zako, hakikisha kwanza kuta zako kama zimenyooka au lah. Usije ukaweka tu plaster ya unene mmoja kutoka juu mpaka chini wakati kuta zako hazijanyooka, ukifanya hivyo maana yake na plaster nayo itakuwa haijanyooka. Kama kuta hazinyooka, unene wa plaster hauwezi...
  3. H

    Natafuta kifaa cha kutengeza hatch kama hii

    Kiongozi hapo tunatumiaga plywood na mbao tu, hakuna hicho kifaa (na hata ukipata unaweza ukakuta vipimo haviendani) Chukua plywood, kata vipande vinavyolingana na unene wa tofali ulizotumia uviloweke kwenye maji Laza ubao wa 1x6 au 1x5 usawa wa nguzo zinapoishia, ambapo chini yake utapigilia...
  4. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ulinzi wa nyumba kupitia madirisha unaimarishwa na pattern ya grill zako. Dirisha za aluminium (vioo) zinazuia tu baridi na vumbi, kwa sababu kama mtu amedhamiria kabisa kuiba anaweza akapasua kioo kwa nyundo au jiwe. Hakikisha pattern ya grill zako utakayochagua iwe ni complex kidogo, sio mtu...
  5. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Slope inayowekwa hapo ni ndogo mno kiasi kwamba huwezi kuiona kwa macho, hata wakati wa kuset inatakiwa ile bubble ya pima maji isitoke yote ktk chumba chake cha kati. Inatakiwa ivuke mstari kidogo sana Kama mlango mwanzo ulikuwa unafunguka vizuri bila shida, then baadae ndio ukawa unakwama...
  6. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ujenzi wa sakafu ya choo/bafu unatakiwa uzingatie drainage ya maji kwa maana hata ikitokea ukachukua ndoo ya maji ukamwaga mlangoni, maji yote yaende kudumbukia kwenye sink la choo bila kuacha vidimbwi pembeni. Hii itasaidia choo chako kuwa kikavu muda wote, na pia itakupunguzia kazi ya kufagia...
  7. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Mwisho wa siku uamuzi utabaki kwa mwenye nyumba, aweke ama asiweke. Hiyo sijasema kwamba inawekwa kwa ajili ya mafundi umeme, nilitolea mfano wa mtu wa kumuuliza hali ya joto iliyopo huko juu
  8. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Sio mzunguko wa hewa ndani ya nyumba, ni mzunguko wa hewa juu ya dari. Mafundi umeme wanaelewa vizuri joto lake wakiwa wanafanya marekebisho huko juu
  9. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ujenzi una hatua zake, na hatua zingine zinatakiwa zitangulie kabla ya zingine. Ukivuruga mpangilio ujue lazima utaingia gharama ya ziada huko mbeleni Mfano unakuta mtu ameanza kupigilia mbao za dari wakati bado hajapachika bomba za umeme ukutani, baadae akitaka kuweka hizo bomba anaanza...
  10. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Hapo safi, kazi imenyooka
  11. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    DPM haiwekwi juu ya nondo ndg, nondo zinalazwa juu ya DPM. Nondo unalaza juu ya DPM, kwa maana hata nondo pia zinatakiwa zilindwe na unyevu ili zisipate kutu ambapo hiyo kazi inafanywa DPM Kiufupi DPM inatenganisha tabaka la mawe (hardcore) na zege (jamvi)
  12. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Nyumba za paa la kuficha kupendeza kwake ni kule kupishana kwa kuta za juu ya mkanda. Changamoto iliyopo ni mafundi kulazimisha kuta zote zilingane urefu hata kama hakuna ulazima. Kule juu ya mkanda, kuna kuta zingine kazi yake ni kusimama kama kingo tu za mifereji ya maji kwa hivyo hakuna...
  13. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Kama unatamani kujenga nyumba ya paa la kuficha lakini unaogopa mambo ya paa kuvuja maji kipindi cha mvua, basi unaweza ukatumia mfumo wa mifereji ya nje (badala ya mifereji inayojengwa katika kuta za ndani) Katika mfumo huu, mifereji yote inayobeba maji inabebwa na kuta za nje na mapaa yake...
  14. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Kama kiwanja chako ni kidogo na unatamani siku za mbeleni uje uweke uzio (fence), basi ni vyema wakati wa kuset nyumba, nyumba yako ukaiset kwenye kona moja wapo ya kiwanja ili ubaki na eneo upande wa mbele na pembeni tu badala ya kuwa na eneo pande zote nne za nyumba (kwa maana ya kuset nyumba...
  15. H

    Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Nondo kavu Ukienda hardware kununua nondo, kuwa makini...fanya field test hapo hapo kabla ya kulipia na kuondoka na mzigo (mchukue fundi abebe na bender yake, uongozane nae hardware). Nondo kavu ukiikunja huwa inakatika, ni kama mti uliokauka sana. Nondo inayofaa katika ujenzi haitakiwi...
Back
Top Bottom