Recent content by Hechy Essy

  1. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Kama kiwanja kiko flat, idadi itategemea na urefu wa msingi unaoutaka mfano mwingine anaweza akajenga kozi 7 (kozi 4 chini ya ardhi, kozi 3 juu ya ardhi) lakini mwingine anaweza akaweka zaidi ya kazi 7 ili msingi uwe juu zaidi Kama kiwanja kina slope, level ya juu ya kiwanja ndio itakayokupa...
  2. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ujirani mwema huwa unaanzia mbali Kama unajenga nyumba yako, na unaona pia kuna mwenzako pembeni nae anajenga nyumba yake, anzeni kuazimana vitu kama ngazi, sijui mpira wa maji n.k Inasaidia sana kuokoa gharama zisizo za lazima lakini pia inatengeneza ujirani mzuri baina yenu kabla hata...
  3. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
  4. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Hapo hapo kwenye usalama ndio ilikuwa dhamira yangu, na hizo taa za sensor zipo za aina tofauti. Kuna zile ambazo zinakuwa zinawaka mwanga mdogo ila ikitokea movement yoyote, mwanga unaongezeka na kuwa mkali zaidi kwa hivyo sio kwamba nyumba itakuwa kiza asilimia 100
  5. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Siku hizi watu wengi taa za nje wanaweka taa zenye motion sensor, kwa maana taa zinakuwa zinawaka tu pale kunapotokea movement yoyote. Kimahesabu inaweza ikawa sawa au ikapunguza matumizi ya umeme ukilinganisha na mtu aliyeweka taa ya watt 20 inayowaka kuanzia jioni mpaka asubuhi. Hizi taa...
  6. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Taa za nje hata kama zinatumia switch moja, usiziunge kwa kufatana (series) kwa sababu ikiungua taa moja basi taa zote pia hazitofanya kazi hata kama zenyewe zitakuwa bado ni nzima. Hata taa za kwenye dari pia ziunge in parallel, ili ikileta shida taa moja, zingine ziendelee kufanya kazi kama...
  7. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Central stablizer ni kifaa kinachofungwa katika mfumo wa umeme ili kuulinda huo mfumo dhidi ya kupanda ama kushuka kwa voltage. Vifaa vyingi vya majumbani vinafanya kazi kwa voltage ya 220V mpaka 240V, sasa mfano kwenye setting, high voltage ukiweka iwe labda 240V, stablizer yako itakuwa...
  8. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Hakikisha main switch yako inawekwa katika umbali ambao unaweza kuifikia ukiwa umesimama bila kutumia nyenzo yoyote kama vile stuli, meza n.k Lakini pia isiwe imefungiwa katika chumba kwa maana itakapotokea shida ya kuhitaji kuizima isimlazimu mtu kuanza kutafuta funguo ya mlango, ndio maana...
  9. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ukuta unaotenganisha uwazi mmoja na uwazi mwingine mfano kati ya dirisha na dirisha au kati ya dirisha na mlango
  10. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ndio inawezekana ndg ila design yako inabidi isiwe na viukuta vifupi, huwa vinasumbua katika kupigilia box za mkanda. Mara nyingi huwa vinakatika Juu ya lental beam, kawaida huwa ni kozi 3 ila kama paa lako lina slope ya kuzidi angle 40 na unataka overhang ya bati iwe kubwa basi ukiweka kozi 4...
  11. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Na kwenye slab nondo zake zimesukwaje? Kichanja kimoja au vichanja viwili?
  12. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Uwazi wa dirisha la choo/bafu unatakiwa uanze baada ya kozi ya saba au juu ya hapo kwa maana kama umejenga kozi 10 kutoka mkanda wa chini hadi mkanda wa juu basi dirisha litakuwa likae katika kozi ya 8, 9 na 10. Kama utahitaji kuweka dirisha refu zaidi, itabidi uongeze idadi ya kozi kutoka...
  13. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Ni ramani na makadirio ndg, ushauri huwa ni bure kabisa siku zote za wiki
  14. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Hapo inategemea na ujazo wa tank lenyewe lakini pia na ardhi yako jinsi ilivyo. Yote kwa yote hata kama utalaza tofali, ni muhimu pia ukaweka na nguzo kuongeza uimara maana tofali za siku hizi sio za kuziamini sana (zinatengenezwa kibiashara zaidi tofauti na tofali za miaka ya nyuma)
  15. H

    JamiiForums Tanzania Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

    Kama unaweka ukuta wa gable, zingatia yafuatayo kuhusu mkanda (beam) 1. Idadi ya nondo, katika usukaji wa nondo funga nondo nne (chini nondo mbili na juu nondo mbili) 2. Hakikisha mkanda wako wa juu una depth ya kutosha kubeba huo mzigo unaokaa juu yake (minimum isipungue nchi 8 sawa na 20cm)...
Back
Top Bottom