Hu
Hiyo wala sio bahati mbaya ndio utaratibu wa AFL.
Mfano mzuri AS Far Rabat ya Morocco wanaongoza ligi na wapo na asilimia kubwa kuchukua ubingwa wa Morocco msimu huu ila hata hivyo hawatashiriki AFL badala yake ni Wydad Casablanca na RS Berkane ndio wenye points za kutosha Caf kushiriki...
Maana ya Champions league ni ligi ya mabingwa ila kwa sasa itakuwa ni kama shirikisho tu maana vigogo wote watakuwa AFL na hayo ni mabadiliko mapya ya Caf kama utakaa kubisha subiri msimu mpya wa Caf uanze ndio utaelewa
Kupenda wengi hatujapenda hata mm nikiwa mmoja wao ila nimeona Caf wametumia...
Kwa hali ilivyo msimu ujao Simba na Yanga zitashiriki AFL bila kujali ligi itaishaje tayari hizo timu mbili zina point za kutosha kuwafanya kuwepo miongoni mwa hizo timu 24
Azam na kati ya hawa Coastal union, KMC au Tanzania Prisons anaweza shiriki nao klabu bingwa barani Africa kwa msimamo wa...
AFL haingalii msimamo wa Ligi za ndani ukiwa na point za kutosha Caf unafuzu moja kwa moja kushiriki AFL.
Klabu bingwa itabaki kwa zile timu zilizokosa points za kushiriki AFL na kwa mantiki hiyo kuanzia mwakani usitegemee kuziona Al Ahly,Wydad,Mamelod,Raja AC au Simba kwenye Champions league...
Kwakweli mm kama mwanasimba siwezi kuacha kuizungumzia Yanga na nilifurahi na mpaka sasa nina furaha kubwa baada ya Uto kutolewa robo fainali klabu bingwa hatua ambayo hapo awali walidhani ni rahisi tu kufika na kupita cha ajabu wameishia kucheza mechi 2 dk 180 bila kufunga hata goli la offside...
Nadhani aibu muanze kuona nyinyi maana mlizani huku klabu bingwa ni shirikisho na mkadhani wanaoishia robo fainali ni wazembe au hawana timu ya kupambana, haya sasa kiko wapi sasa nyie wenye timu bora mmebaki kulilia kosakosa iwe goli kuficha aibu yenu ya kuishia robo
Yaani kwa sasa tumesahau kila kitu hata jina la kocha wetu tu hatukumbuki ila tunachokumbuka tu Yanga wametolewa robo fainali na Mamelod licha ya kuandika barua ya kujiliza na manung'uniko Caf plus kushinda kwenye page za Caf kutukana bado wananchi wameishia robo fainali
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.