Niliambiwa nikipatiwa good medication naweza kuishi hadi miezi nane. Lakini matibabu ni gharama kubwa na sihitaji msaada niko Kwenye critical stage na napata maumivu makali sana. Nahisi ni vema nife nipumzike.
Ripoti ya daktari inasema baada ya miezi 4 nitakufa kutokana na kansa ya kongosho (pancreatic cancer stage 4.)
Kwa hiyo miezi minne ijayo nitaweza kuona kile marehemu wanachoona sijui kufa kunaumaje?
Juzi nimepita kando ya makaburi nikaishia kutabasamu tu nilipogundua next 4 month nitafukiwa...
Amen mpendwa!! Maandishi yako haya yanaweza kutafsiriwa kama uungwana na huruma kubwa dhidi ya binadamu wenzako na waungwana wenzio.
Asante, nitazingatia mpendwa!
Nakushukuru ndugu! Kauli yako ni kauli ya waungwana wengi wenye mapenzi mema na binadamu wenzao.
Kwa maana hiyo hiyo, kauli ya wengi ni kauli ya mungu!! Mungu ataweka wepesi tu siku moja.
Amen!!
Ndugu mpaka hivi sasa niko kwenye hali ya mtanziko, kwa maana sijapata mtu alie tayari kutafuta suluhu ya hili gumu kwa muktadha ninaopendekeza kulingana na tatizo langu mbali na sokwe ambae amependekeza suluhu itafutwe hospitali zaidi.
Asante.
Ndio namwamini yesu kama bwana na mwokozi wa maisha yangu, ila nadhani sijapata mtu wa mungu mwenye karama za mungu kuweza kuratibu na kuwezesha mlolongo mzima wa
wokovu kupitia jina la yesu.
Shukrani ndugu,
Pole kwa magumu yaliyokukuta na pia hongera kwa kuweza kutoka kwenye dhoruba hilo maana kuna baadhi ya watu wanaona kama vile masuala haya tunayozungumzia hapa ni hadithi za abrakadabla na kusadikika tu, mbaya zaidi wanafikia hatua ya kuanza kuhukumu watu waungwana na wasamaria...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.