Ubinadamu si sisi, kwa tafsiri sisisi
Wengine wetu mafisi, wa mawazo mufilisi
Wajitia majasusi, wajifanya mamilisi
Nasema hao si sisi, wana chembe za ufisi
Wana wingi wa matusi, zina sumu zao hisi
Wamejawa uyabisi, machoni utusitusi
Wafurikwa na ubinafsi, wajiona ni wakwasi
Nasema hao si sisi...