Recent content by Filipo Lubua

  1. Filipo Lubua

    Tangazo hili la ASAS linachochea kufanya kazi bila kufuata kanuni bora za afya, lizuiliwe

    Hili tangazo ni hatari sana. Linashawishi watu kufanya kazi pasi na kuchukua tahadhari stahiki za kiafya, eti kwa sababu ya brand yako ya maziwa. Unaruhusuje tangazo kama hili liende hewani? Tangazo ambalo linawashawishi watu kufanya kazi bila kufuata kanuni bora za afya eti tu kwa sababu...
  2. Filipo Lubua

    Tumefikia Utimamu wa Uwazimu

    Twajaa utimamu wa uwazimu, bila dhima twamhukumu imamu Huzunini twajifanyia karamu, Ramadhani twabugia kharamu Wenye wehu tumewapa hatamu, dhiki yetu itadumu dawamu Maumivu yatujia kwa jamu, watoto wetu watatulaumu Isikize yangu nudhumu, niambapo kwa yangu taalimu Niseme hilaze bin-Adamu...
  3. Filipo Lubua

    Mnapoendelea na Siku Tatu za Maombi, Msisahau Kusoma Aya Hizi

    Serikali imetangaza ongezeko la wagonjwa wengine wapya 53 na sasa jumla ya walioambukizwa Tz ni 147. Hawa 53 wapya, wikiendi ilopita, mlikuwa nao huko makanisani, misikitini, vijiweni, baani, na kungineko? Kama walikuwa huko, waliambukizwa na nani? Nao wameshawaambukiza wangapi? Idadi halisi ya...
  4. Filipo Lubua

    Mnapoendelea na Siku Tatu za Maombi, Msisahau Kusoma Aya Hizi

    Mnapoendelea na siku tatu za maombi, msisahau kusoma aya hizi: "Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu. [kwa hiyo] kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu, mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga...
  5. Filipo Lubua

    COVID-19 - Lest We Forget We Still Have Some Tears to Shed

    Evidently, on social media, Tanzanians (and I think, for the most part, Africans) were having fun, cracking jokes, and singing songs to mock COVID-19, as of two to one week ago. Many of us have witnessed scads of jokes circulating on social media as if, as a country, we have special immunity to...
  6. Filipo Lubua

    Nape: Sina kinyongo na uamuzi wa Rais Magufuli; Akasirishwa na aliyemtishia Bastola

    Wagalatia 4:15-17 "Mlikuwa wenye furaha; sasa kumetokea nini? Naapa kwamba wakati ule mngaliweza hata kuyang'oa macho yenu na kunipa mimi. Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa sababu ya kuwaambieni ukweli? Hao watu wengine wanawahangaikia ninyi, lakini nia zao si njema. Wanataka kuwatenganisha nami...
  7. Filipo Lubua

    Wengine Wetu Mafisi

    Ubinadamu si sisi, kwa tafsiri sisisi Wengine wetu mafisi, wa mawazo mufilisi Wajitia majasusi, wajifanya mamilisi Nasema hao si sisi, wana chembe za ufisi Wana wingi wa matusi, zina sumu zao hisi Wamejawa uyabisi, machoni utusitusi Wafurikwa na ubinafsi, wajiona ni wakwasi Nasema hao si sisi...
  8. Filipo Lubua

    Swali la Msingi: Kwani ni lazima kila Mwana CCM kumchagua Magufuli? Na ni...

    Si lazima kufanya chochote kati ya hivyo. Ila ni lazima kila MwanaChadema na kila MwanaCCM kuunga mkono mabadiliko. Mabadiliko yanakuja kwa kubadilisha mfumo wa uongozi, wakati mwingine hata kama mabadiliko hayo yataleta mabadiliko ya kisiasa tu. Narudia, ni sharti na wajibu wa kila Mtanzania...
  9. Filipo Lubua

    GE2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

    Rafiki yangu mmoja akasema "Mkuu wa Malofa ni Lodi Lofa". Basi kama huyu jamaa aliyewaita Watanzania "Malofa" alishakuwa rais wa hao Malofa, yeye mwenyewe ndiye Lodi Lofa, a.k.a. "LordLofa". Kwa wale mlowahi kusoma gazeti la Sani, basi mnazielewa tabia za Lodi Lofa. Hilo la "Wapumbavu"...
  10. Filipo Lubua

    Kikwete, Vipi wanawake wasitie Nia?

    Nina swali rahisi tu kwa Mwenyekiti Wa CCM Katika mchakato wa utiaji nia hadi sasa, bado sijaona mwanamke hata mmoja aliyejaribu kufanya hivyo. Je Rais wangu, bado mfumo wetu wa kidemokrasia haujatuwezesha kuwa na wanawake majasiri, wenye uwezo wa kutuongoza? Mfumo wetu wa Viti-Maalumu...
  11. Filipo Lubua

    Video: Sehemu ya hotuba yangu nikitangaza nia ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Imekuwaje hukutupatia mpango kazi wa namna utakavyoyatatua matatizo uliyoyaorodhesha? By the way kwanini unafikiri kigezo kikubwa cha kuwa Rais ni kuzaliwa kwenye familia maskini kama yako? Tumechoka watu wanaolalamikalalamika na kututajia matatizo yetu kila siku, tunahitaji watu wanaotuambia...
  12. Filipo Lubua

    Tanzania, unaugua ugonjwa gani?

    Ndugu Watanzania, Nadhani ni kweli tunapaswa tupimwe akili zetu. Inakuwaje nchi inajenga ushabiki wa kisiasa kiasi hiki, na kushindwa kuutazama uadilifu na historia ya watu wanaoomba kuongoza nchi? Haiwezekani kila anayefanya ufyongo na kujiuzulu au kutimuliwa nafasi walizokuwa nazo, anaibuka...
  13. Filipo Lubua

    Kutoka Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria Musoma: Prof. Muhongo atangaza nia ya Kugombea Urais

    Ama kweli Watanzania tutafutiwe mtaalamu aje atupime akili zetu. Hivi kweli mtu mwenye akili timamu unaweza kuwaza Profesa Muhongo anaweza kuwa Rais kwa zile tabia zake kweli? Hey people! Let's be serious! This is not only our country, but the country of the future generations.
  14. Filipo Lubua

    Picha: Jakaya Kikwete akibusu mkono wa Papa Benedict

    Ngoja waendelee kuwaaminisha Waislamu kuwa nchi inaendeshwa kwa mfumo-kristo. Watayavuna matunda ya kazi yao
  15. Filipo Lubua

    Waislamu Waazimia Kumuunga Mkono Lowassa!

    Hivi Watanzania tutaelewa siasa lini? Au hujajua kuwa mbele ya pesa hata dini inawekwa pembeni? Hao si ndio waliosema 'mtumikie kafiiri upate mradi wako'? Wamempokea kwa shamrashamra, sio kwa sababu wanamkubali lakini kwa sababu alikuwa pale kwa ajili ya kuwapatia pesa za msikiti!
Back
Top Bottom