Ok asante kwa kuwa mzalendo nimeipenda reply yako...nisaidie kipimo cha uzalendo na mimi nijikague kama ni mzalendo au mfuasi wa mabeberu...hahaaaa! Kazi njema mkuu
Haya mrembo mbona namba ya simu haujaweka? wewe hutaki uteuzi? Umetoka povu namna hii kuwatetea wanyonge,huku ubongo wake umefungia kabatini unatumia tumbo kufikiri na kuandika
Khaaa! Agustino nawe kujikomba gani sasa huku hivi umeenda shule kweli? Au ndio akili zako kwa sasa ziko likizo unatumia masuburi kufikiria,mimi naamini hata mzee baba akiusoma huu uzi wako atagundua umezidisha kujikomba..huteuliwi kamwe umechelewa,heri ya Propesa Lipumbavu kuliko wewe
Mnyika alishajua hawezi kurudi bungeni naamini amejiandaa kwa maisha mengine nje ya bunge,sisi wengine ni wakaaji wa jimbo hili hatujawahi kumwona toka uchaguzi mkuu 2015 mambo nengine jimboni ni ya hovyo na yeye wala hata haangaiki,mleta mada ameeleza vizuri, Mnyika ni kama Nassari tu,wameshiba...
Wanajamvi,
Mimi binafsi nina eneo langu la takribani ekari 18 maeneo ya bwawani wilaya ya Mvomero njia ya kuelekea Dodoma baada ya kuvuka mizani mkono wa kulia mwendo kama wa dk 30 kwa pikipiki,ardhi ni nzuri bado virgin ila changamoto yake eneo hilo halina vyanzo vya maji kama mito ya uhakika...
Kama ikitokea CAG akaitikia wito wa kufika mbele ya kamati ya maadili kuhojiwa wadau tuna haki ya kujua hiyo team ya maadili inaundwa na wabunge gani,profile zao tafadhali maana huko sifa mojawapo ni kujua kusoma na kuandika, sasa Profesa atahojiwa na nani au watakuwa na TOR za kuwaongoza. Yetu...
Kama habari hii ni ya kweli basi tunabidhaa nyingi tu zinaozea shambani/sokoni pawe na business plan nzuri masoko yatafutwe dege letu litupelekee matunda kama ndizi,embe,tikiti machungwa huko ughaibuni na hasa middle east wazee wa jangwa hawana matunda nasisi wakulima tutajirike...hongera...
Kazi kwelikweli,inasemwa katika biblia sina hakika kwa dini zingine kuwa waendao jehanamu ni wengi kuliko mbinguni/peponi haya yatadhibishwa na hii mada na wachangiaji wake,devil at work lakini haizuii watumishi kupiga kazi ya Mungu aliehai,call them any names you wish but they will proceed...
Pole mkuu unatoka povu na mambo ya imani basi sawa watu kama wewe watakupongeza kwa huu mchango wako ila wale wanomwabudu Mungu hawawezi kubishana na mtu kama wewe watakuombea na wewe upate nuru ya kuujua ukweli bado uko gizani endelea kukashifu tu viongozi wa dini,kuhusu nani tapeli nani si...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.