Aisee bila kulipa ada husajiliwi kwa maana hiyo ukienda kufanya usajili unaambatanisha bank slip yako ya malipo ya ada ndo unasajiliwa hii hutumika vyuo vingi hapa bongo
kama kwenye mkopo wako unnalipiwa tuition fee basi fanya uwahi kujisajili kama umeshindwa kujua kiasi cha ada unachotakiwa kulipa wanao husika na usajili watakujuza. Hosteli kwa mzumbe hawakupi hadi uwe umelipa ada ya chuo..na pesa ya hosteli unatakiwa kuilipa wewe na sio bodi ya mkopo
Hapo ni jumla ya ada yote plus michango ndo inakuja hiyo total ya 1465000 Ila semester ya kwanza anapaswa kulipia 815000/= Then semester ya pili atamalizia 650000/=
Maana hiyo ni Saris account ya Mzumbe
Huyu jamaa ndo anaepaswa hasa kupimwa mkojo...Ama kweli masikini akipata.....Ubinafsi ubinafsi ubinafsi dhambi kubwa inayotuteketeza watanzania...huyu anaonyesha dhahiri ata akifika huko chuo kusoma kwake kutakuwa ni kwa kujijali mwenyewe..Badilika kijana hapa ndo unaanza kutengeneza future...
Wale wa Mzumbe campus ya MBEYA karibuni sana ukienda MBEYA kuna stendi kubwa mbili ya nane nane na stendi kuu ya mjini kote ukishuka utafika tu chuo bila shida..kumbuka kutokuja na mizigo mingi kipindi hiki itakuletea usumbufu..kwa wale wanaohitaji hosteli za bei nafuu ziko ndani ya chuo humo...
Fungua Google then Andika Mzumbe Saris kisha ifungue ikikubali weka username ambayo ni form four index namba yako iwe mfumo huuu S000/0000/0000 kisha password ni surname yako kwa herufi ndogo baada ya hapo kila kitu chako utakiona
Pesa unapewa kwa awamu NNE kwa mwaka inamaanisha kwa kila semester unapewa Mara mbili na semester moja INA miezi minne so kila baada ya miezi miwili utapatiwa fungu lako
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.