Heshima kwenu wakuu.
Samahani wakuu, naomba msaada namna ya kuipata hadithi au mwandishi wa hadithi fulani iliyopata kuchapishwa hapa jukwaani. Hadithi hii nilipata kusoma hapa jukwaani hapo nyuma kitambo lakini nimesahau jina na pia mwandishi wake. Hivyo naomba mwenye kuweza kunipa link yake...
Kiongozi ubarikiwe sana. Na Mimi mke wangu alipimwa na kukutwa na tatizo hili. Je naweza kupata muongozo zaidi kuhusu hiyo clinic iliyokusaidia?. Ila mimi nipo mkoani sio Jiji la Dar.
Mkuu mimi hii njia yako ninaichukua na kuitumia kwenye maisha yangu binafsi. Siku moja nitakupa mrejesho. Hakika ni bonge moja la idea lakini je atakusikiliza? Hapa ndipo kazi ilipo.
Daaah! Kiongozi hii hoja yako imenipandisha hasira sana. Yaani umetoa hoja nzito, kubwa na iliyoshiba sana. Mkuu ubarikiwe sana na uishi miaka mingi asee. Nafurahi sana kuona kuna watu wenye upeo mpana ndani ya nchi hii. Asante sana kwa kunifanya niendelee kuamini kuwa sijawa zombi bado. Kwa...
Mkuu samahani sana kama nitakosea kukuuliza swali. Naamini wewe una wazazi. Vipi wazee wako wakikuomba ushauri? Utawashauri au utakataa kuwashauri kwa kuwa wewe hauna mamlaka ya kuwapangia? Ni nini mchango wako Kwa wazee wako? Je ni kuwapa pesa tu?
Nashukuru sana mkuu Kwa kuelewa lengo langu kuu. Hoja ni kuwa aweke fedha hizo wapi ili awe anakula pole pole na sio kuwekeza. Nadhani wajumbe wengi wameshindwa kuelewa kusudi kuu la andiko langu
Nimekuelewa sana mkuu. Ngoja nimshirikishe mzee nione kama kuna kitu atasema. Japo mimi nimeliona ni wazo zuri ukizingatia kuwa mshua mambo ya kilimo anayawezea sana na amekuwa akifanya muda mrefu. Kwa wazo hili naona mzee akipata eneo akatulia mwenyewe akawa analima huku anafuga anaweza kufanya...
Mkuu hili wazo pia zuri. Ngoja nitafakari pia. Lakini huoni kuwa ufugaji pia una changamoto zake za kutosha? Vipi changamoto za usimamizi wa hiyo mifugo? Malisho ya mifugo usimamizi ukoje ukizingatia hulka ya vijana wa leo katika utendaji kazi wao? Vipi mlipuko wa magonjwa kwa mifugo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.