Unacheza na akili za watu, unajipanga na uchaguzi kukiwa na tume ileile ya uchaguzi. Hatua ya kwanza ingekuwa kudai TUME HURU. Ilikuwa rahisi kwako kutangaza wagombea wote waliosalia kwenye serikali za mitaa wajitoa, leo macho yote uchaguzi 2020, umemsahau Akwilina. TUME HURU! TUME HURU
Uwepo wa Lisu ulitegemea kuongeza ushindani na hamasa ya uchaguzi, hasa baada misukosuko aliyopambana nayo. Wanachama na wasio wanachama wanatambua msimamo wa Lissu usioyumba lakini kwa upande mwingine ni mwaminifu na mtii kwa chama na viongozi. Kimempata nini hata akabadilisha msimamo wa...
Umejitahidi kuchambua lakini umesahau hoja moja ya msingi ambayo haisemwi lakini ni ya muhimu sana nayo ni USALAMA. Hata kama yakawepo hayo yote kama hakuna usalama ni kazi bure. Matukio ya kutekwa mauaji au kunyang´anywa mali za watu hususani inapotokea kwa wataliii wenyewe linapoteza watalii...
Demokrasia ipo wapi CHADEMA? Ilitosha kusema kauli ya Lowassa haukuwa msimamo wa Chama, mazungumzo Yao yalikuwa binafsi. Naanza kuwaelewa wanaohama CHADEMA. Hivi uhuru wa kutoa maoni upo chadema? Sasa tunahitaji Chama kingine mbadala. Hata Lowassa maelezo yake yalikuwa wazi kuwa yeye binafsi...
Lema unauliza mema yapi wakati Lowassa ameyataja wazi anayoyaona yeye kuwa mema? Hayo uliyosema Lema hayawezi kuwa mema, na hayo aliyosema Lowassa hayawezi kuwa mabaya. Uwe makini, unazidi kuleta mpasuko, hukuwa na sababu ya kumshambulia Lowassa katika hili.
Niliwahi andika tutafakari madhara ya kususa uchaguzi, moja ya dhara lilikuwa CCM kuvuna wanachama kirahisi ambao nikama wametelekezwa na ukawa. Nini kilikuwa nyuma ya pazia kususa uchaguzi, haifai kushabikia tu bila kujiuliza kwa undani kwasababu imesema kamati kuu.
UKAWA umesusia uchaguzi kwa hoja ya kuogopa vurugu na kukatana mapanga kama ilivyotokea katika uchaguzi wa madiwani. Inafaa kujiuliza kwa undani juu ya maamuzi hayo.
Maswali haya na mengine yanaweza kutuongoza kuangalia kwa makini maamuzi yaliyofanywa.
1. Je, kususia uchaguzi kutaleta suluhisho...
Umesema kweli, hakuna mikakati madhubuti, wanakuja na matamko ya kususia uchaguzi bila mikakati mbadala itakayoshinikiza kuwepo Kwa tume huru ya uchaguzi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.