NEC: Chama cha Siasa kutangaza kugomea uchaguzi hakuwezi kuifanya Tume iuahirishe! Tume haiko kushawishi chama kushiriki

Vyama vyote vya Siasa vinapata fedha ktk Serikalini ili kujiendesha, hivyo kwa kuwa tunavilipa pia vina jukumu la kushiriki chaguzi zote zilizoko kisheria, hivyo kwa maoni yangu Chama ambacho kinasusia Uchaguzi kilazimishwe kurudisha fedha zetu za ruzuku, hata sehemu tu ya fedha zetu irudi hazina, ...

Wengine wanasusia kwa sababu ile pesa ya ruzuku inanyakuliwa kama mwewe anavyonyanyua kifaranga na haikai hata wiki moja. Kwanza kumlipa mwenyekiti pesa aliyokikopesha chama kwenye uchaguzi mkuu. Pili kumlipa mjumbe wa kamati kuu milioni kama mia mbili kwa kukiongezea chama idadi ya wabunge na hivyo kuongeza ruzuku. Hapo bado mishahara, pango, umeme nk. Kutabaki pesa ya uchaguzi mdogo hapi?
 
Vyama vyote vya Siasa vinapata fedha ktk Serikalini ili kujiendesha, hivyo kwa kuwa tunavilipa pia vina jukumu la kushiriki chaguzi zote zilizoko kisheria, hivyo kwa maoni yangu Chama ambacho kinasusia Uchaguzi kilazimishwe kurudisha fedha zetu za ruzuku, hata sehemu tu ya fedha zetu irudi hazina, ...
Fedha zenu?!?!???!???!!!?
 
Kwani fedha za ruzuku ni kwa ajili ya uchaguzi tu? Mbona km mnakuwa hamtumii akili kufikiri wakati mwengine!
Hata km unalipwa kwa kupost basi jaribu kupost kuonuesha maendeleo yaliyofikiwa na chama chako nafhani itakuongezea wanachama zaidi kuliko kuwa km zwazwa.
 
Vyama vyote vya Siasa vinapata fedha ktk Serikalini ili kujiendesha, hivyo kwa kuwa tunavilipa pia vina jukumu la kushiriki chaguzi zote zilizoko kisheria, hivyo kwa maoni yangu Chama ambacho kinasusia Uchaguzi kilazimishwe kurudisha fedha zetu za ruzuku, hata sehemu tu ya fedha zetu irudi hazina, ...
Kweli ukiwa CCM wewe ni hayawani namba moja
 
Vyama vyote vya Siasa vinapata fedha ktk Serikalini ili kujiendesha, hivyo kwa kuwa tunavilipa pia vina jukumu la kushiriki chaguzi zote zilizoko kisheria, hivyo kwa maoni yangu Chama ambacho kinasusia Uchaguzi kilazimishwe kurudisha fedha zetu za ruzuku, hata sehemu tu ya fedha zetu irudi hazina, ...
Mku nao wafuasi wao kuna fedha zao wameshakubali kutoshiriki .Mambo yamebadilika kila tasisi iko vizuri kwa kutegemea Itikadi zao sio tatizo kuruzika na kuchanga pale panakofaa kwa utashi wa raia husika
 
Vyama vyote vya Siasa vinapata fedha ktk Serikalini ili kujiendesha, hivyo kwa kuwa tunavilipa pia vina jukumu la kushiriki chaguzi zote zilizoko kisheria, hivyo kwa maoni yangu Chama ambacho kinasusia Uchaguzi kilazimishwe kurudisha fedha zetu za ruzuku, hata sehemu tu ya fedha zetu irudi hazina, ...
Mikutano ya vyama ipo kwa mujibu wa sheria ilivyokatazwa kwa uwoga wa mwenyekit mbona hujayasema haya? Bunge la katiba watu wametumbua pesa wee na hakuna kilichotokea mbona hujawahi kuhoji au kupendekeza haya? K
Kivuko kibovu je pesa zirudishwe?
Wewe huipendi nchi una maslahi ya kikundi
 
Kweli ukiwa CCM wewe ni hayawani namba moja
FB_IMG_1511959900367.jpg
 
UKAWA umesusia uchaguzi kwa hoja ya kuogopa vurugu na kukatana mapanga kama ilivyotokea katika uchaguzi wa madiwani. Inafaa kujiuliza kwa undani juu ya maamuzi hayo.
Maswali haya na mengine yanaweza kutuongoza kuangalia kwa makini maamuzi yaliyofanywa.
1. Je, kususia uchaguzi kutaleta suluhisho la tatizo?
2. Je, Kuna sababu nyingine iliyopelekea kususia?
3. Kutakuwa faida gani ya kususa uchaguzi?
4. Kutakuwa na madhara gani kususa uchaguzi?

Kwa maoni yangu:
Je, kususia uchaguzi kutaleta suluhisho la tatizo?
Kususia bila kuwa na mkakati madhubuti wa kushinikiza mabadiliko hakuwezi kuleta suluhisho la tatizo ambalo ni tume ya uchaguzi. Pia kususia bila kupendekeza njia nzuri ya kutatua tatizo haisaidii. Mazungumzo yaliyopendekezwa hayawezi kuleta tume huru ya uchaguzi.

Je, Kuna sababu nyingine iliyopelekea kususia?
Sababu ya kiuchumi inaweza kuwa sababu mojawapo ya kususia uchagu, ili ruzuku ielekezwe kwenye matumizi mengine ya chama.

Kutakuwa faida gani ya kususa uchaguzi?
Hukuta kuwa na faida kwa UKAWA kususa uchaguzi bali kwa upande wa vyama vingine vya upinzani itakuwa nafasi nzuri kujitangaza na kujiongzea umaarufu na kwa upande wa ccm kushinda bila kupata upinzani

Kutakuwa na madhara gani kususia uchaguzi?
Kutakuwa na madhara wakati wa kampeni, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi:
Wakati wa kampeni wananchi watakosa fursa kusikia kasoro za utendaji wa serikali.
Chama tawala kutumia muda huo kudhoofisha UKAWA bila kuwa na mjibizo wa hoja na kuwaacha wananchi njia panda.
Kampeni kukosa mvuto na ushindani.

Wakati wa uchaguzi wananchi kulazimika kuchagua chama wasichokipenda kwa kukosa mbadala.
Watu wengi kutoshiriki uchaguzi.

Baada ya uchaguzi: Mshindi kukosa nguvu za kiutawala na kiuongozi kutokana na wengi kutoshiriki katika uchaguzi

Nini kingefanyika:
Kutumia nafasi hiyo ya kampeni kuelimisha wananchi ubovu wa tume ya uchaguzi ambayo sio huru.
Kutafuta mbinu mbadala kukabiliana na uhuni na fujo ambazo zingejitokeza wakati wa chaguzi.
Kutumia nafasi hiyo kuanzisha kampeni maalumu ya kudai tume huru ya uchaguzi.
 
Mleta uzi fahamu tunahitaji kufanya siasa ila sio kushiriki uchaguzi wa kutakatisha siasa chafu za awamu ya tano. Kama kuna mwananchi anasubiri kampeni za kesho kutwa ndio ajue mapungufu na ukatili dhidi ya awamu hii ya tano basi huyo hataelewa hata wapinzani waliojitoa wakishiriki. Hakuna kiongozi wa upinzani ambaye yuko tayari kupeleka wafuasi wake kukatwa mapanga huku mshindi akitangazwa ccm hata kama kashindwa. Bora hao wafuasi wabaki salama wajionee na kufanya kazi kwenye hivyo viwanda vinavyohubiriwa. Pia kususia kutaufanya umma kujua kwamba wanaongozwa bila ridhaa yao bali kibabe na kinyama, hata dunia itajua huu uhuni wa kipuuzi unaoendelea. Ila usijali bado vyama vya upinzani vipo vinavyoshiriki, nenda kashirikiane navyo kueleza hayo mapungufu ya serekali na kushinikiza tume huru ya uchaguzi.
 
Mleta uzi fahamu tunahitaji kufanya siasa ila sio kushiriki uchaguzi wa kutakatisha siasa chafu za awamu ya tano. Kama kuna mwananchi anasubiri kampeni za kesho kutwa ndio ajue mapungufu na ukatili dhidi ya awamu hii ya tano basi huyo hataelewa hata wapinzani waliojitoa wakishiriki. Hakuna kiongozi wa upinzani ambaye yuko tayari kupeleka wafuasi wake kukatwa mapanga huku mshindi akitangazwa ccm hata kama kashindwa. Bora hao wafuasi wabaki salama wajionee na kufanya kazi kwenye hivyo viwanda vinavyohubiriwa. Pia kususia kutaufanya umma kujua kwamba wanaongozwa bila ridhaa yao bali kibabe na kinyama, hata dunia itajua huu uhuni wa kipuuzi unaoendelea. Ila usijali bado vyama vya upinzani vipo vinavyoshiriki, nenda kashirikiane navyo kueleza hayo mapungufu ya serekali na kushinikiza tume huru ya uchaguzi.
Mtoa uzi yupo sahihi ila wewe ndio unajifanya kichwa maji. Unasema dunia ijue,ikijua itaifanya nini Tz ya Dr Magu,kwani hata mliposema Tz isipewe misaada ni nchi gani iliwafuatisha zaidi ya kuwapuuza. Mnajisumbua sana,Dr Magu mbele kwa mbele,Odinga alisusia uchaguzi kenya,mbona Rais yupo na anapiga kazi na alikwenda kumsalimia Lisu
 
CCM hawataki kabisa kusikia kusikia habari kuwepo kwa tume uhuru ya uchaguzi, na wanajua kuwa siku watakayo ruhusu kuwepo kwa hiyo tume ndio utakuwa mwisho wao kusikika kwenye siasa za nchi hii, Ila bado naamini kuwa kuna siku watakosea kwenye uteuzi huo badala ya kumpata wa kuwa tetea atakuja atakaye kwenda kinyume na matarajio yao . Kwani ni nani aliamini kuwa yule kaburu Declark wa Afrika kusini angeruhusu uchaguzi ambao unge ruhusu utawala dhalim
u wa kaburu kung'oka madarakani.
 
Back
Top Bottom