We unajitoa akili kwa makusudi au umepewa buku 7?uaisafisha serikali kwa lipi? Mtu ametekwa alfajiri hao unao watetea wanasema walikuwa na kikao na madereva wa mwendo kasi, wanatuletea coloured picture za cctv, wanamwachia karibu na ikulu, sehemu iliyo na ulinzi wa kufa mtu, wanatoweka nakuacha...
Na serikali yako je? Inatangaza imeajiri watu 3,000 afya ila 90% ni attendants. Inasema imeajiri waalimu 4000. Wengi wao ni washule za msingi na za awali. Usanii mtupu. Afadhali ajira za Mo kuliko serikalini, wanaajiri zaidi cheep labour ili waonekane wameajiri.
Wanafanya jaribio la kuichoma gari,"wanashindwa" inawezekana ile gari imetengenezwa kwa madini ya asbestos. Na eneo walipomwachia haiingii akilini kwani ni eneo lenye ulinzi mkali. Drama nyingine ni kuacha silaha ndani ya gari. Mi naamini " kuchamba sana utatoka na mavi"
Mapovu yanini? Jibu hoja. Kwa nilivyomuona Mo ktk ile clip, upon umuhimu wa kupelekwa nje ya nchi kwa checkup. Alidhoofu zaidi ya Roma baada ya kutekwa na kuachiwa. Mo ana mengi ya kutueleza kuhusu tukio hili, ila najua hatosema chochote kama ilivyokuwa kwa Roma. Labda utawala ubadilike.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.