Kinachomponza Prof. Palamagamba J.A.M.Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,516
Nawasalimu waungwana wa JF,

Imekuwa hulka yangu kuzuia upotoshaji na ubabaishaji kuwahusu watu ambao nawafahamu hata kama ni kwa kiasi. Mmojawapo ni Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Hii leo si mara yangu ya kwanza 'kumtetea' Prof. Kabudi. Sioni soni wala sina tashwishwi 'kumtetea' Prof. Kabudi kwakuwa si mtu anayezungumzwa azungumziwavyo.

Nimewahi 'kumtetea' kuhusu Uwakili wake na ujumbe wake Bungeni: https://www.jamiiforums.com/threads...ungumza-bungeni.1242547/page-20#post-28374171. Sitakoma 'kumtetea' kwakuwa namuamini, namheshimu na najua uwezo wake katika kulitumikia Taifa hili. Nafahamu kujitoa kwake kwa maslahi ya Taifa zima.

Mfano, gawio lililopatikana kutoka Airtel Tanzania kutokana na matunda ya Timu ya Majadiliano ya Serikali iliyoongozwa naye litasaidia katika utekelezaji wa miradi ya kiserikali itakayowanufaisha watanzania wengi kwa ujumla wao. Prof. Kabudi anapaswa kuombewa, kupongezwa na kutiwa moyo wa kuendelea na msimamo, uzalendo na utendaji wake uliotukuka. Pamoja na kuwa Wizara moja, amekuwa akifanya kila aambiwalo kulifanya kwa maslahi mapana ya nchi hii kwa weledi mkubwa.

Profesa Kabudi sasa amekuwa gumzo kufuatia kauli yake ya juzi pale Ikulu kuwa 'Mheshimiwa Rais amemtoa jalalani'. Wapo wanaoita hata Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jalala. Wapo wanaoizungumzia kauli hiyo kwa kejeli na hujuma za kisiasa bila hata ya kujua mantiki na maana halisi ya kauli yake. Profesa Kabudi anaponzwa na kuzungumza kwa 'parables'. Anapozungumza anaamini kuwa ataeleweka. Inakuwa tofauti. Anatumia 'akili kubwa' kufikisha ujumbe wake.

Prof. Kabudi amekuwa mtumishi wa Serikali wa kawaida katika muda wote wa maisha yake ya kikazi. Kuanzia kuwa Mhadhiri Mkufunzi (Tutorial Assistant) hadi Profesa Mshiriki wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amekuwa mtumishi wa kawaida.

Kadiri nimjuavyo, hakuwahi kushika wadhifa wowote mkubwa wa kisiasa au kiserikali. Amestaafu utumishi wa umma mwaka 2016. Kutolewa kuwa mtumishi wa kawaida hadi kuwa Mbunge na baadaye Waziri Kamili ni jambo la kustaajabisha. Ni jambo la kushukuru. Hujikuta akishukuru kila mara-kwa Mwenyezi Mungu na kwa Rais Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa utumiaji wake wa maandiko matakatifu katika kuzungumza kwake, maandiko ambayo huitaji 'akili kubwa' kuyaelewa, Prof. Kabudi hujikuta akiwaacha solemba wasikilizaji wake kwa kuongea mambo yanayohitaji 'akili kubwa' kuyaelewa. 'Jalala' ni sehemu duni. 'Jalala' ni sehemu ya chini. 'Jalala' la Prof. Kabudi ni alipokuwepo kabla ya sasa kuwa Mbunge na Waziri Kamili. Ametolewa sehemu duni hadi yenye unafuu mkubwa. Kwanini asishukuru na kusema hatamsahau Mhe. Rais?

Narudia tena, kulingana na usomi wake na umahiri wake wa matumizi ya maneno ya kimaandiko na Kiswahili, Prof. Kabudi huponzwa na uficho unaozunguka hoja zake. Labda ajitahidi kuzungumza kwa lugha nyepesi na ya moja kwa moja ili kutowaacha wasikilizaji wake solemba na kumtafsiri kadiri watakavyo.
 
Kama na Wewe ni Msomi unatetea ujinga kama huu, kweli Shule za Watanzania ni hovyo!

Mtu mwenye elimu Kiwango cha Profesa sio mtu Duni Ndugu yangu! Sio lazima uwe Mbunge /waziri ndio uwe wa Maana! Kila mwajiriwa wa Serikali ni Ofisa wa Serikali.

Wenzetu wanaojitambua wanathamini Taaluma zao zaidi kuliko vyeo vya kisiasa
Wewe una Malengo yako kutetea unachotetea,
 
Prof. Kabudi kaongea vizuri tu ila chuki za watu wanaona wivu na kazi anayofanya. ni Prof. Kabudi aliyemwabia Tundu Lissu nyamaza na acha kuisema nchi vibaya, Lissu akanyamaza kimya. Kitendo hicho kiliwaumiza sana wapinzani( sasa wanamshambulia).

Sehemu pekee ambayo CHADEMA hawataki kuisema na ambayo imebeba ujumbe wa kauli ya Kabudi ni pale aliposema " baada ya kustaafu" . kama mtu alikuwa kastaafu inakuwaje akawa tena mtumishi wa UDSM? Hapo ndipo ukweli wa alichosema Prof. kabudi upo lakini unaamua kupotoshwa makusudi
 
Uliyoandika ni tafsiri yako wewe kwa maneno yake kujalibu kuyaweka katika positive way.Kauli ya Kabudi haihitaji aakili kubwa sana kuyaelewa,hata akili ndogo tu kama Bashite anaelewa.Amekuwa mhadhiri na mpaka professa ,hapo tu alikuwa ashakusanya zaidi mil.120 kama mishahara.Baadae akawa mtumishi wa kawaida akakusanya kama mil.20 kama misahara.Tangia ameajiriwa UDSM hadi sasa marupurupu aliyopata ni zaidi ya mi.30.

Mtu mwenye level ya Kabudi/profesa hakutakiwa kuwa mpambe anayefanya mambo kama zombie asiye na akili.Kauli zake nyingi tangia ameshika madaraka zinaonekana ameambukizwa uzombi.Si yule wa katiba mpya.Kwa nini mawazo yake yabadilike baada ya kuonja madaraka kama sio kwamba akili zishakuwa corrupted?

Hii ni fundisho kuwa kwenye jamii ya kileo kunahitajika financial education maana haiwezekani Kabudi analalamika kuokotwa jalalani wakati Msukuma na Kibajaji wanafurahia mafanikio yao.Elimu ya kabudi haijamsaidia kiuchumi.Hii inaonekana kwa watumishi wengi ambapo baada ya kustaafu maisha yanakuwa magumu wengine wanarukwa na akili na kuwa vichaa.
Hapa mtaani kwetu tulishakuwa na mzee anaishi maisha ya chini kabisa katika vyumba vya kupanga karibu kabisa na mitaro ya majitaka ya keko huku lakin ukisikiliza maelezo yake ni kwamba alifanya kazi ikulu kipindi cha mwinyi,alifundisha UDSM ana wakina Sengo na Senkoro na wengineo maarufu na ukimcheki anaakili tu nzuri na anajua mambo na alisoma kweli,lakin maisha yake ni shida sana na baadae nilisikia alifariki.

Kabudi akiwa waziri sasa ayajenge maisha yake kiuchumi.Isije ikawa baada ya miaka 20 mbele Mungu akimpa uzima aje alielie tena.Hatutomwelewa.
 
Kwa hiyo kwa akili yako unaamini kabisa tunakusubiri wa utueleweshe kuhusu hoja za Kabudi ndio tuelewe huwa anaongea nini. Unamaanisha wote tunaomkosoa hatuna akili kubwa hivyo tunahitaji ww mwenye akili kubwa kutuelewesha. Kwamba ameongea na Airtel mpaka tumepata gawio, kimsingi yeye ndio aliyepata nafasi ya kuongea na hao Airtel, ila mtu yoyote mwenye nia njema angeweza kuongea na hata kupata zaidi ya hiyo 1b. Acha dharau dogo na kutaka kutakatisha Kaniki kwani ndio rangi yake. Huyo mzee anajikomba fullstop.
 
ni kweli UDSM ni jalala la vilaza. Angalia product za UDSM mfano Tundu Lisu, Zitto, ndio utajua ni jalala la vilaza tena kitengo cha sheria kimezidi
Ni kweli kabisa japo na mimi nimesoma UD ila kwa anayofanya prof.Kabudi,PhD ya Magufuli nayo inanitatiza aliipataje maana haihitaji akili kubwa kujua yule ana ukilaza fulani hivi na huenda alipewa Ph D ya heshima tu lakin kama nae alifanya reseach na kufanya oral na written presentation basi UDSM huenda kuna vilaza.
 
Nawasalimu waungwana wa JF,

Imekuwa hulka yangu kuzuia upotoshaji na ubabaishaji kuwahusu watu ambao nawafahamu hata kama ni kwa kiasi. Mmojawapo ni Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Hii leo si mara yangu ya kwanza 'kumtetea' Prof. Kabudi. Sioni soni wala sina tashwishwi 'kumtetea' Prof. Kabudi kwakuwa si mtu anayezungumzwa azungumziwavyo.

Nimewahi 'kumtetea' kuhusu Uwakili wake na ujumbe wake Bungeni: https://www.jamiiforums.com/threads...ungumza-bungeni.1242547/page-20#post-28374171. Sitakoma 'kumtetea' kwakuwa namuamini, namheshimu na najua uwezo wake katika kulitumikia Taifa hili. Nafahamu kujitoa kwake kwa maslahi ya Taifa zima.

Mfano, gawio lililopatikana kutoka Airtel Tanzania kutokana na matunda ya Timu ya Majadiliano ya Serikali iliyoongozwa naye litasaidia katika utekelezaji wa miradi ya kiserikali itakayowanufaisha watanzania wengi kwa ujumla wao. Prof. Kabudi anapaswa kuombewa, kupongezwa na kutiwa moyo wa kuendelea na msimamo, uzalendo na utendaji wake uliotukuka. Pamoja na kuwa Wizara moja, amekuwa akifanya kila aambiwalo kulifanya kwa maslahi mapana ya nchi hii kwa weledi mkubwa.

Profesa Kabudi sasa amekuwa gumzo kufuatia kauli yake ya juzi pale Ikulu kuwa 'Mheshimiwa Rais amemtoa jalalani'. Wapo wanaoita hata Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jalala. Wapo wanaoizungumzia kauli hiyo kwa kejeli na hujuma za kisiasa bila hata ya kujua mantiki na maana halisi ya kauli yake. Profesa Kabudi anaponzwa na kuzungumza kwa 'parables'. Anapozungumza anaamini kuwa ataeleweka. Inakuwa tofauti. Anatumia 'akili kubwa' kufikisha ujumbe wake.

Prof. Kabudi amekuwa mtumishi wa Serikali wa kawaida katika muda wote wa maisha yake ya kikazi. Kuanzia kuwa Mhadhiri Mkufunzi (Tutorial Assistant) hadi Profesa Mshiriki wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amekuwa mtumishi wa kawaida.

Kadiri nimjuavyo, hakuwahi kushika wadhifa wowote mkubwa wa kisiasa au kiserikali. Amestaafu utumishi wa umma mwaka 2016. Kutolewa kuwa mtumishi wa kawaida hadi kuwa Mbunge na baadaye Waziri Kamili ni jambo la kustaajabisha. Ni jambo la kushukuru. Hujikuta akishukuru kila mara-kwa Mwenyezi Mungu na kwa Rais Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa utumiaji wake wa maandiko matakatifu katika kuzungumza kwake, maandiko ambayo huitaji 'akili kubwa' kuyaelewa, Prof. Kabudi hujikuta akiwaacha solemba wasikilizaji wake kwa kuongea mambo yanayohitaji 'akili kubwa' kuyaelewa. 'Jalala' ni sehemu duni. 'Jalala' ni sehemu ya chini. 'Jalala' la Prof. Kabudi ni alipokuwepo kabla ya sasa kuwa Mbunge na Waziri Kamili. Ametolewa sehemu duni hadi yenye unafuu mkubwa. Kwanini asishukuru na kusema hatamsahau Mhe. Rais?

Narudia tena, kulingana na usomi wake na umahiri wake wa matumizi ya maneno ya kimaandiko na Kiswahili, Prof. Kabudi huponzwa na uficho unaozunguka hoja zake. Labda ajitahidi kuzungumza kwa lugha nyepesi na ya moja kwa moja ili kutowaacha wasikilizaji wake solemba na kumtafsiri kadiri watakavyo.
"Prof. Kabudi huponzwa na uficho unaozunguka hoja zake" uko sahihi,ni akili kubwa kwahiyo inahitajika akili kubwa kuelewa...
 
Back
Top Bottom