ONYO LA POLISI: Ujumbe wa simu kutumiwa fedha, kuwasiliana na mganga ama kushinda bahati nasibu

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Jeshi la Polisi limeonya wananchi kuhusu ukiukwaji wa sheria unaofanywa na baadhi ya watu wanaotumia ujumbe mfupi wa maandishi katika simu wakidai kutumiwa fedha, kuwasiliana na mganga fulani ama kushinda bahati nasibu.

Jeshi la Polisi kupitia taarifa yake iliyoitoa leo, Jumatano limewatahadharisha wananchi kupuuza ujumbe pamoja na simu wanazopigiwa kwani zina nia ovu ya kutaka kuwatapeli.

Katika taarifa hiyo, Jeshi la Polisi limesema kwa yeyote atakayepata usumbufu wa ujumbe au kupigiwa simu hizo aripoti Polisi, na Kitengo cha Upelelezi na Makosa ya Mitandao kinaendelea na uchunguzi ili kuwabaini wahusika na kuwachukulia hatua.

FB_IMG_1528279358455.jpg


Hili swala limejadiliwa sana hapa. Zaidi soma=>Meseji (SMS) za dawa za Kiganga: Je, hawa ni matapeli? TCRA mko wapi? Namba wanatoa wapi?
 
Kutakuwa na mkuu wa police kashapigwa tayari sijui atakuwa Kamanda nani? Sijui ni muraaa au wa kule kwa Fid Q.

Kwa sababu hizo inshu ni za kitambo kama mwaka na zaidi sasa lakini onyo ndio linatolewa leo.
 
Naona baada ya kupigwa biti na albert msando makampuni ya simu yana act now
 
nipeleke tatzo langu kwa polisi hawa hawa au? Bora niwatumie hio hela kuliko kwenda et polisi.
 
Nilichogundua hizi info zetu wanatoa kwenye vitabu vya kuanduka namba kwenye maofisi, binafsi nimepokea mara mbili tuu text kama hizi, ma kumbukumbu zangu zinaniambia nimeandika mara 2 tuu namba zangu za kweli kwenye kitabu, pale TPDC Azikiwe
 
Nyie polis mtakuwa mnahusika bhn,watu washalizwa ndomnakuja Leo na mikwara yenu?au ndo kawaida yenu tatizo likitokea madhara yanatokeaa af nyie mnafika mwisho,tushawazoea nyie hamtupi kazi
 
Back
Top Bottom