Rais Dkt.John Pombe Magufuli amekutana na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako Ikulu Dar es salaam Mhe.Rais amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za serikali za msingi na sekondari.
Rais Magufuli: Tumesema elimu bure, elimu bure haiwezi kaja tena kwa mgongo mwingine ikawa elimu pesa. Tumeweka utaratibu kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari form four hakuna kulipa ada yoyote. Nimewapa maelekezo kwamba kuanzia leo iwe ni marufuku na wakalisimamie hili. Mzazi sitaki kusikia akilalamika mwanae amerudishwa shule kwa sababu ya michango.
Rais Magufuli: Na walimu wote wasishike mchango wowote toka kwa mwanafunzi, mchango kama kuna mwananchi anataka kuchangia apeleke kwa mkurugenzi, mkurugenzi kama anataka kutengeneza madawati atatengeneza na kupeleka kwenye shule inayohusika. Siyo mwanafunzi ameenda shuleni akarudishwa kwasababu hajatoa michango.
Rais Magufuli: Kwahiyo nimemweleza waziri na waziri mwenzake kwasababu ndio wanaoshughulikia elimu. Lakini kwa taarifa hii mkawaeleze wakuu wa mikoa, wakuu wa mikoa na wakurugenzi.
Rais Magufuli: Nikisikia kuna shule katika wilaya fulani ambayo mtoto anarudishwa kwasababu hajachangia michango huyo mkurugenzi hana kazi. Na hii waanze kutekeleza kuanzia leo. Maafisa elimu wote wakasimamie hili, wanalipwa kwa ajili ya kusimamia. Tunajua enrolment ya wanafunzi imeongezeka hizi ni challenge ambazo lazima tuzibebe sisi kama serikali lakini hii isiwe sasa ni demotivation nyingine ya kuwazuia watoto, sasa hivi watoto wameacha kwenda shule kutokana na michango hii inayotolewatolewa sasa waziri mkalisimamie hili.
Maagizo haya yanakuja ikiwa ni siku moja baada ya malalamiko ya mwanaJF kuhusu kutozwa sh 70,000 huko Butiama mkoani Mara, zaidi soma=> Mkanganyiko elimu bure: Huko Butiama wananchi walazimishwa kuchanga elfu 70, la sivyo unanyang'anywa kuku, sufuria, n.k.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua dhidi ya viongozi na watendaji ambao shule za msingi na sekondari zilizopo katika maeneo yao zinawatoza wanafunzi michango mbalimbali kinyume na muongozo uliotolewa na Serikali wa utoaji wa elimu bila malipo.
Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo asubuhi tarehe 17 Januari, 2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Lazaro Ndalichako na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Said Jafo.
Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inatoa Shilingi Bilioni 23.875 kila mwezi kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa elimu bila malipo lakini inashangaza kuona bado kuna walimu wanaendelea kuwatoza michango ama kuwarudisha nyumbani wanafunzi ambao wanashindwa kutoa michango hiyo.
“Nawaagiza Mawaziri, sitaki kusikia mwanafunzi anarudishwa nyumbani kwa kushindwa kutoa michango, na fikisheni maagizo haya kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na wote wanaohusika, nikisikia tena mahali jambo hili linaendelea hawa niliowateua mimi wataondoka.
“Haiwezekani tumefuta ada, halafu walimu wanaamua kuanzisha michango tena mikubwa ambayo watu masikini wanashindwa kusomesha watoto wao, na kama wazazi wanataka kuchangia kitu shuleni wapeleke michango yao kwa Mkurugenzi, lakini sitaki kusikia mwanafunzi anapewa sharti la kutoa mchango ndipo apokelewe shule” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kupata taarifa kuwa zipo baadhi ya shule ambazo wanafunzi wanadaiwa michango mbalimbali tena kwa kiwango kikubwa ikiwemo chakula, maabara, madawati na ziara za kujifunza, hali iliyosababisha wazazi kushindwa kumudu.
Waziri Prof. Joyce Lazaro Ndalichako ameagiza walimu na viongozi wa halmashauri kuwarudisha shule mara moja wanafunzi wote waliorudishwa nyumbani kwa kutotoa michango na pia kurejesha mara moja michango iliyokusanywa kinyume na mwongozo wa Serikali.
Waziri Mhe. Selemani Said Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwasilisha taarifa ya shule ambazo zimetoza michango kinyume na mwongozo wa Serikali ifikapo Ijumaa wiki hii (tarehe 19 Januari, 2018) ili hatua zichuliwe dhidi ya walimu na maafisa elimu ambao kwa makusudi wamekiuka mwongozo huo.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
17 Januari, 2018
Rais Magufuli: Tumesema elimu bure, elimu bure haiwezi kaja tena kwa mgongo mwingine ikawa elimu pesa. Tumeweka utaratibu kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari form four hakuna kulipa ada yoyote. Nimewapa maelekezo kwamba kuanzia leo iwe ni marufuku na wakalisimamie hili. Mzazi sitaki kusikia akilalamika mwanae amerudishwa shule kwa sababu ya michango.
Rais Magufuli: Na walimu wote wasishike mchango wowote toka kwa mwanafunzi, mchango kama kuna mwananchi anataka kuchangia apeleke kwa mkurugenzi, mkurugenzi kama anataka kutengeneza madawati atatengeneza na kupeleka kwenye shule inayohusika. Siyo mwanafunzi ameenda shuleni akarudishwa kwasababu hajatoa michango.
Rais Magufuli: Kwahiyo nimemweleza waziri na waziri mwenzake kwasababu ndio wanaoshughulikia elimu. Lakini kwa taarifa hii mkawaeleze wakuu wa mikoa, wakuu wa mikoa na wakurugenzi.
Rais Magufuli: Nikisikia kuna shule katika wilaya fulani ambayo mtoto anarudishwa kwasababu hajachangia michango huyo mkurugenzi hana kazi. Na hii waanze kutekeleza kuanzia leo. Maafisa elimu wote wakasimamie hili, wanalipwa kwa ajili ya kusimamia. Tunajua enrolment ya wanafunzi imeongezeka hizi ni challenge ambazo lazima tuzibebe sisi kama serikali lakini hii isiwe sasa ni demotivation nyingine ya kuwazuia watoto, sasa hivi watoto wameacha kwenda shule kutokana na michango hii inayotolewatolewa sasa waziri mkalisimamie hili.
Maagizo haya yanakuja ikiwa ni siku moja baada ya malalamiko ya mwanaJF kuhusu kutozwa sh 70,000 huko Butiama mkoani Mara, zaidi soma=> Mkanganyiko elimu bure: Huko Butiama wananchi walazimishwa kuchanga elfu 70, la sivyo unanyang'anywa kuku, sufuria, n.k.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua dhidi ya viongozi na watendaji ambao shule za msingi na sekondari zilizopo katika maeneo yao zinawatoza wanafunzi michango mbalimbali kinyume na muongozo uliotolewa na Serikali wa utoaji wa elimu bila malipo.
Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo asubuhi tarehe 17 Januari, 2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Lazaro Ndalichako na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Said Jafo.
Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inatoa Shilingi Bilioni 23.875 kila mwezi kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa elimu bila malipo lakini inashangaza kuona bado kuna walimu wanaendelea kuwatoza michango ama kuwarudisha nyumbani wanafunzi ambao wanashindwa kutoa michango hiyo.
“Nawaagiza Mawaziri, sitaki kusikia mwanafunzi anarudishwa nyumbani kwa kushindwa kutoa michango, na fikisheni maagizo haya kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na wote wanaohusika, nikisikia tena mahali jambo hili linaendelea hawa niliowateua mimi wataondoka.
“Haiwezekani tumefuta ada, halafu walimu wanaamua kuanzisha michango tena mikubwa ambayo watu masikini wanashindwa kusomesha watoto wao, na kama wazazi wanataka kuchangia kitu shuleni wapeleke michango yao kwa Mkurugenzi, lakini sitaki kusikia mwanafunzi anapewa sharti la kutoa mchango ndipo apokelewe shule” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kupata taarifa kuwa zipo baadhi ya shule ambazo wanafunzi wanadaiwa michango mbalimbali tena kwa kiwango kikubwa ikiwemo chakula, maabara, madawati na ziara za kujifunza, hali iliyosababisha wazazi kushindwa kumudu.
Waziri Prof. Joyce Lazaro Ndalichako ameagiza walimu na viongozi wa halmashauri kuwarudisha shule mara moja wanafunzi wote waliorudishwa nyumbani kwa kutotoa michango na pia kurejesha mara moja michango iliyokusanywa kinyume na mwongozo wa Serikali.
Waziri Mhe. Selemani Said Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwasilisha taarifa ya shule ambazo zimetoza michango kinyume na mwongozo wa Serikali ifikapo Ijumaa wiki hii (tarehe 19 Januari, 2018) ili hatua zichuliwe dhidi ya walimu na maafisa elimu ambao kwa makusudi wamekiuka mwongozo huo.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
17 Januari, 2018