Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,671
Naifikiria miaka mia moja ijayo, au labda mia mbili au mia tatu!! Ni nini itakuwa hatma ya dunia? mbari ya binadamu (human race) itaendelea kutawala?
Mpaka kufikia siku ya leo, Tarehe 13 March 2017, Dunia ina jumla ya watu bilioni saba na milioni mia nne thelathini na tisa. Idadi hii inaongezeka kwa asilimia 1.18% kila mwaka... Maana yake kwamba mpaka kufikia mwaka 2030 dunia itakuwa na watu bilioni 8.5 na ikifika mwaka 2100 dunia itakuwa na watu bilioni 11.2.!!
Lakini bado! Yes.. Bado, bado hatufiki hata robo ya uwezekano wa ninachokifiria.. Ninachotamani kila mtu afikiri.!!
Sayari yetu iko katika mfumo wa jua ambalo ni nyota moja kati ya nyota bilioni 100 zilizondani ya Milkway galaxy.. Na hii ni galaxy moja tu kati ya galaxy trilioni 10 zilizopo kwenye Universe.!
Kwa hiyo dunia ni kama punje ya mchanga kwenye pwani.. Haiwezekani ikawa mahala pekee penye uhai.!
Lazima kuna la zaidi katika haya maisha.. Yes, there must more to this life! Lazima kuna siri zilizofichika labda ubongo wetu hauna uwezo wa kufikiri na kufichua siri hizo kwa sababu binadamu wote, hata wale wenye akili kupitiliza, wote tunatumia chini ya asilimia 20 ya uwezo halisi wa ubongo wetu!
Itakuwaje tukiweza kuvumbua siri, siri ambayo itatufanya tuwe na binadamu wenye uwezo wa kutumia zaidi ya asilimia 20 ya nguvu ya ubongo wetu? Itakuwaje tukiweza kuwa na mbari ya binadamu (human race) yenye kutumia nguvu yote ya ubongo.. Je, wanaweza kusaidia kufunua siri za mambo yaliyojificha??
Lazima kuna la zaidi katika haya maisha.. Yes there must be more to this life..
Naifikiria miaka mia moja ijayo, au labda mia mbili au labda mia tatu!! Dunia yetu itakuwa wapi? Mbari ya binadamu itakuwepo??
Ninachokiwaza ni wendawazimu, lakini ni "wendawazimu" ndio ambao kwa historia yote wameisukuma mbari ya binadamu kwenda mbele..
Najua ninachokiwaza, na uzuri si mimi peke yangu ninayekiwaza, lakini zuri zaidi sio kwamba tu tunawaza.. Bali pia tunajua.. Kuna jambo la tofauti linatokea kila kona ya dunia.. Kuna mbari mpya ya binadamu inaibuka, mbari ambayo haifanini na mimi na wewe..
Kuna mbari mpya inaibuka kila pembe ya dunia!!
Je, itatuacha tuendelee kuishi? Au itatamani kutufuta kutoka kwenye uso wa dunia??
Tumekuwepo kwenye uso wa dunia zaidi ya miaka bilioni 4, tumetawala na kujimilikisha dunia kuwashinda wanyama na viumbe wengine wote.. Lakini kwa mara ya kwanza, naliona tishio la binadamu kufutwa katika uso wa dunia.!!
Naifikiria miaka mia moja ijayo, labda mia mbili au mia tatu? Dunia yetu itakuwepo? Mbari ya binadamu itakuwa wapi??
There must be more to this life.. Kuna siri zinahitaji kuwekwa wazi ili kulinda uwepo wa mbari yetu ya binadamu.!!
------------------
SIKU YA JUMAMOSI JIONI, HAPA HAPA KWENYE THREAD HII... TUTAZINDUA SIMULIZI MPYA KABAMBE INAYOITWA "THE OTHER HALF".!!
(Jumamosi Jioni ndio tunaanza Episode 1)
Usikose..
The Bold.