JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Nimesikia sehemu kuwa binadamu anaweza kupata usugu wa vimelea kutokana na kutumia mazao yatokanayo na wanyama mbalimbali, mfano wa mazao hayo ni nyama nk. Hofu yangu ni kuwa wafugaji wengi siku hizi wamekuwa si waaminifu kabisa, wamekuwa wakitumia madawa hatari kwa ajili ya kukuzia haraka wanyama ili waingize sokoni, au wakati mwingine wamekuwa wakitumia madawa kwa ajili ya kuhifadhi mazao hayo ili yakae muda mrefu bila kuharibika. Kumekuwepo cases nyingi za nguruwe na kuku kuchanganyiwa dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI. JamiiCheck.com naomba mniondoe wasiwasi huu maana tunakoelekea huko mbeleni ni hatari.
Nimeona mtandaoni Mkuu wa kitengo cha Digital, Crown Fm ameandika kuwa Mara ya mwisho Yanga SC kufungwa kwenye Ligi Kuu ni Oktoba 4, 2023 bado siku 3 itimize mwaka mmoja pasipo kupoteza mchezo kwenye Ligi Ligi Kuu ya NBC PL. Eti wadau huyu anasema kweli au anatupanga maana huwa naona kama mnazi wa Yanga isijekuwa mapenzi ya timu yamefanya achakachue takwimu atupange. JamiiCheck fanyenyi jambo tujue Ukweli.
Salama wakubwa wa JamiiCheck? Katika pitapita zangu mitandaoni kuna mtu nimeona akishauri kuwa ni vizuri kumnyoa mtoto mchanga nywele alizozaliwa nazo ili mtoto akue vizuri. Amedai kuwa mtoto asiponyolewa nywele hizo anaweza pata madhara ya ngozi ya kichwa, ukuaji duni lakini mwisho ni mambo ya kiimani. Binafsi nipo njiapanda maana nimekuwa nikiona watoto wengine wakinyolewa ndani ya wiki moja baada ya kuzaliwa, lakini wengine hawajawahi guswa nywele zao mpaka wanakuwa wakubwa.
Wakati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kikitangaza kufanya Maandamano ya amani leo Jijini Dar Es salaam chini ya Mwenyekiti wake Freeman Mbowe, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amechapisha mtandaoni mwake akisema anazo taarifa kuwa Mwenyekiti Mbowe yupo Arusha na hivyo kumualika ofisini kwake Jijini Arusha. Makonda ameandika "Kaka yangu Mbowe kumbe umeingia Arusha na hausemi. Karibu Ofisini basi ukiamua Kutoka" Ikumbukwe kuwa saa chache zilizopita, nyumba ya Freeman Mbowe iliyopo Mikocheni ilizingirwa na Jeshi La Polisi huku mkewe Dr Lilian Mtei akiripotiwa kuzuia kutoka nyumbani kwake. Source: Jambo TV
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…