zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 19,081
- 28,742
Habari za kazi wanajukwaa, bila ya kupoteza muda niende kwenye mada.... Je biblia iliiga simulizi zake kutoka dini za kipagani na kuhadaa watu kuwa ni stori za ukweli???
Kwenye biblia kuna hadithi kadhaa za watu muhim ambazo nyingi zilishakuwa zimesimuliwa hata kabla ya biblia kuandikwa tuangalie mifano michache hapo chini
1.Story ya Hawa/Eve wa biblia Vs Story ya pandora box. Story hizi zinafanana kwa kiasi kikubwa sababu zote zinaelezea uumbaji wa mwanadamu wa kwanza ulikuwaje na kivipi mwanamke alipelekea anguko la dunia hii. Story ya pandora inaelezea kuwa mwanadamu wa kwanza aliumbwa na miungu ya kipagani kutumia udongo, akapuliziwa uhai na miungu akapelekwa kuishi duniani, pia anapata mwanaume anaitwa epimethius, aanapewa BOX na anaambiwa asifungue ila siku moja anashawishiwa kupitia mungu anaitwa HERA kufungua bila kujua lina kila aina ya ubaya kuanzia tamaa,uchoyo,kifo,mauaji,visasi na dhambi zingine nyingi na hivyo kupelekea dhambi kuingia duniani!! ukiangalia kwa umakini story hii inafanana kabisa na kisa cha adam na eva ambao nao waliumbwa kwa udongo,waliwekwa duniani, walipewa pumzi na Mungu pia walipewa masharti wasile tunda flani ila mwisho wa siku eva anashawishiwa na nyoka na kula hivyo kupelekea anguko la mwanadamu . Kinachoshangaza hadithi hii ya pandora ilishaanza kusimuliwa miaka zaidi ya 800-1000 kabla ya kristo ila story ya adam na hawa kwa mara ya kwanza inaandikwa kwenye biblia miaka 400 kabla ya kristo je iliigwa au kila mtu aliandika kivyake???
2. Nuhu na gharika Vs utnapishtim na gharika. Kwenye biblia Nuhu aliagizwa na Mungu ajenge boti kubwa achukue wanyama wote na kuingia humo maana kuna mvua kubwa inaletwa na Mungu ambayo itafuta uzao wote wa mwanadamu na baada ya gharika anatoa sadaka kumshukuru Mungu. Stori hii inafanana na kisa cha EPIC OF GILGAMESH kilichoandikwa takribani miaka 2700 kabla ya kristo ilihali kuendana na biblia gharika na Nuhu limetokea takribani miaka 2147-2500 kabla ya kristo. Sasa basi kwenye kisa cha Epic of gilgamesh tunaona kuna mtu anaitwa utnapishtim huyu naye anaambiwa na mungu EA kwamba ajenge boti (yenye vipimo sawasawa na Nuhu),anachukua wanyama wote, mvua kubwa inanyesha na uzao wote unakufa, baada ya gharika utnapishtim anatuma ndege wawili kupima kma mafuriko yameisha na kma vile Nuhu na yye anatoa sadaka kwa miungu iliomponya na gharika. Kisa hiki kimesimuliwa hata kabla story ya Nuhu wa biblia hajazaliwa!!!! Je imenakiliwa ama ni matukio mawili tofauti??
3. Story ya Musa kwenye Biblia Vs Story ya Sargon wa Akkadia. Visa vya watu hawa wawili vinafanana kabisa kuanzia kuzaliwa mpaka utawala wao. Wote wanazaliwa kwa siri, wote wanawekwa kwenye kikapu kinachoelea kwenye mto, wote wanaokotwa na malkia/binti mflame wa nchi husika na wote wanatunzwa kwenye kasri huku mwishoni kabisa wote wanaongoza jamii zao kwenye ukombozi!!! Zingatia kwamba Sargon aliishi miaka 2279 Kabla ya kristo ilihali Musa amezaliwa miaka 1391 kabla ya kristo?? Je hi nayo ni copy and paste ama ni matukio mawili tofauti
4. Amri kumi za Mungu Vs amri za Hammurabi. Hapa sina mengi ya kusema ila takribani mfumo na amri za Mungu alizopewa Musa zinafanana na Amri za mungu SHAMASH alizompatia mfalme Hammurabi wa mesopotamia zingatia kitabu cha kutoka kimeandikwa takriban miaka 500 kabla ya kristo na Musa aliishi takriban miaka 1300 kabla ya kristo huku Hammurabi alishakufa miaka 1750 kabla ya kristo yaani amekufa miaka zaidi ya 400 kabla musa hajazaliwa wala amri 10 za Mungu hazijaandikwa je mfanano huu ni coincidence au ni copy and paste na kuhadaa watu
Mifano ni mingi takribani 100 ya simulizi za biblia zinazofanana kwa 90% ya simulizi za hadithi za kipagani hasa za sumeria na kigiriki ambazo zimesimuliwa miaka mingi hata kabla Biblia haijaandikwa wala watu wanaotajwa kwenye biblia hawajazaliwa bado
NB: Mada hii nimeweka ili mjadala huu upate hitimisho kama ni kweli biblia ni copy and paste ama ni halisi ila tuujadili kwa ushahidi wa kihistoria na sio kwa misingi ya kidini hivyo sitegemei kashfa za kidini humu ila tujadiliane kwa kuelimishana nategemea wengi tutajifunza mengi katika uzi huu wa kufikirisha
Naomba kuwasilisha
Kwenye biblia kuna hadithi kadhaa za watu muhim ambazo nyingi zilishakuwa zimesimuliwa hata kabla ya biblia kuandikwa tuangalie mifano michache hapo chini
1.Story ya Hawa/Eve wa biblia Vs Story ya pandora box. Story hizi zinafanana kwa kiasi kikubwa sababu zote zinaelezea uumbaji wa mwanadamu wa kwanza ulikuwaje na kivipi mwanamke alipelekea anguko la dunia hii. Story ya pandora inaelezea kuwa mwanadamu wa kwanza aliumbwa na miungu ya kipagani kutumia udongo, akapuliziwa uhai na miungu akapelekwa kuishi duniani, pia anapata mwanaume anaitwa epimethius, aanapewa BOX na anaambiwa asifungue ila siku moja anashawishiwa kupitia mungu anaitwa HERA kufungua bila kujua lina kila aina ya ubaya kuanzia tamaa,uchoyo,kifo,mauaji,visasi na dhambi zingine nyingi na hivyo kupelekea dhambi kuingia duniani!! ukiangalia kwa umakini story hii inafanana kabisa na kisa cha adam na eva ambao nao waliumbwa kwa udongo,waliwekwa duniani, walipewa pumzi na Mungu pia walipewa masharti wasile tunda flani ila mwisho wa siku eva anashawishiwa na nyoka na kula hivyo kupelekea anguko la mwanadamu . Kinachoshangaza hadithi hii ya pandora ilishaanza kusimuliwa miaka zaidi ya 800-1000 kabla ya kristo ila story ya adam na hawa kwa mara ya kwanza inaandikwa kwenye biblia miaka 400 kabla ya kristo je iliigwa au kila mtu aliandika kivyake???
2. Nuhu na gharika Vs utnapishtim na gharika. Kwenye biblia Nuhu aliagizwa na Mungu ajenge boti kubwa achukue wanyama wote na kuingia humo maana kuna mvua kubwa inaletwa na Mungu ambayo itafuta uzao wote wa mwanadamu na baada ya gharika anatoa sadaka kumshukuru Mungu. Stori hii inafanana na kisa cha EPIC OF GILGAMESH kilichoandikwa takribani miaka 2700 kabla ya kristo ilihali kuendana na biblia gharika na Nuhu limetokea takribani miaka 2147-2500 kabla ya kristo. Sasa basi kwenye kisa cha Epic of gilgamesh tunaona kuna mtu anaitwa utnapishtim huyu naye anaambiwa na mungu EA kwamba ajenge boti (yenye vipimo sawasawa na Nuhu),anachukua wanyama wote, mvua kubwa inanyesha na uzao wote unakufa, baada ya gharika utnapishtim anatuma ndege wawili kupima kma mafuriko yameisha na kma vile Nuhu na yye anatoa sadaka kwa miungu iliomponya na gharika. Kisa hiki kimesimuliwa hata kabla story ya Nuhu wa biblia hajazaliwa!!!! Je imenakiliwa ama ni matukio mawili tofauti??
3. Story ya Musa kwenye Biblia Vs Story ya Sargon wa Akkadia. Visa vya watu hawa wawili vinafanana kabisa kuanzia kuzaliwa mpaka utawala wao. Wote wanazaliwa kwa siri, wote wanawekwa kwenye kikapu kinachoelea kwenye mto, wote wanaokotwa na malkia/binti mflame wa nchi husika na wote wanatunzwa kwenye kasri huku mwishoni kabisa wote wanaongoza jamii zao kwenye ukombozi!!! Zingatia kwamba Sargon aliishi miaka 2279 Kabla ya kristo ilihali Musa amezaliwa miaka 1391 kabla ya kristo?? Je hi nayo ni copy and paste ama ni matukio mawili tofauti
4. Amri kumi za Mungu Vs amri za Hammurabi. Hapa sina mengi ya kusema ila takribani mfumo na amri za Mungu alizopewa Musa zinafanana na Amri za mungu SHAMASH alizompatia mfalme Hammurabi wa mesopotamia zingatia kitabu cha kutoka kimeandikwa takriban miaka 500 kabla ya kristo na Musa aliishi takriban miaka 1300 kabla ya kristo huku Hammurabi alishakufa miaka 1750 kabla ya kristo yaani amekufa miaka zaidi ya 400 kabla musa hajazaliwa wala amri 10 za Mungu hazijaandikwa je mfanano huu ni coincidence au ni copy and paste na kuhadaa watu
Mifano ni mingi takribani 100 ya simulizi za biblia zinazofanana kwa 90% ya simulizi za hadithi za kipagani hasa za sumeria na kigiriki ambazo zimesimuliwa miaka mingi hata kabla Biblia haijaandikwa wala watu wanaotajwa kwenye biblia hawajazaliwa bado
NB: Mada hii nimeweka ili mjadala huu upate hitimisho kama ni kweli biblia ni copy and paste ama ni halisi ila tuujadili kwa ushahidi wa kihistoria na sio kwa misingi ya kidini hivyo sitegemei kashfa za kidini humu ila tujadiliane kwa kuelimishana nategemea wengi tutajifunza mengi katika uzi huu wa kufikirisha
Naomba kuwasilisha