mnamtukana bibi wa watu bure,mbona bunge limehairishwa hadi kesho juu ya swala hilo?
hivi lini mtakuwa? Kwa masuala kama haya acheni kuchangia kiushabiki wakuu, tuhabarisheni juu ya hiyo meli madhara yaliyotokea na kinachojiri bungeni.
mnamtukana bibi wa watu bure,mbona bunge limehairishwa hadi kesho juu ya swala hilo?
huyu mama kawa kichekesho leo, mwanzo kakataa kuhairisha Bunge, baada ya wabunge kutoka Nje akaona imekula kwake mara moja akahairisha Bunge kwa aibu kubwa, Nchi hii haina Spika wa Bunge
Kwa msisitizo mkubwa, nashauri wabunge wote wa upinzani wafanye press conference sasa hivi, watoe pole kwa waliokutwa na maafa, na wawaeleze watanzania kwa nini wamemua kutoka nje ya bunge. Na baada ya hapo baadhi yao wasafiri haraka kwenda Zanzibar. Hilo tu. Makinda na wabunge wa CCM waendelee na bajeti yao ya ulaji.
Kwa Kanumba bunge lilisimama, IGP mstaafu hakuna kitu, mpigania uhuru Mzee Kyaruzi hakuna kitu, watu 200 Zanzibar wanazama wanaendelea as if hakuna chochote kilichotokea. Wabunge wa CCM wanamuwakilisha nani?