BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,119
Hatua hiyo imefikiwa baada ya Wabunge wa upinzani kutolewa ndani ya Ukumbi wa Bunge kutokana na kupinga mabadiliko hayo yaliyoibua vurugu Bungeni pamoja na maandamano makali kutoka kwa Wananchi wanaoshinikiza Uchaguzi ufanyike kama ulivyopangwa awali.
Kwa uamuzi huo, Rais Macky Sall atabakia kuwa madarakani kwa kipindi cha mwaka mmoja zaidi ya muda wa Kikatiba hadi pale mrithi wake atakapopatikana. Sall alitakiwa kuondoka Ikulu Aprili 2, 2024 kama Uchaguzi ungefanyika Februari 25, 2024.
Tangazo la kuahirishwa kwa Uchaguzi limeripotiwa kuzusha vurugu katika Miji mbalimbali ya Taifa hilo, hali iliyosababisha Serikali kuziagiza Kampuni za Simu kuzima Huduma ya Intaneti kwa madai kuwa inatumika kusambaza taarifa za Uchochezi na Machafuko.