Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Mfano moja ambao naupenda ni huu Managing Director wa Interconsult ni Mosha alikuwa shirika la reli zamani alianzisha hii kampuni ambayo inafanya vizuri miaka ya 1980s alifanikiwa kwa kupata Tenda nyingi za jeshi nchi nzima na sasa ameendeleza vizuri.

Lakini naye haajiri mtu mpaka awe mchaga mwenzie, ni wachache sana ambao utakuta sio wachaga. Lakini hili halina ubaya kwa sababu ni kampuni binafsi ingawaje wanakomba tenda nzuri nzuri kutoka serikalini. THIS IS ONE OF THE FEW TANZANIAN CONSULTANTS YOU CAN MENTION.
 
kusema ukweli nakumbuka back in 1990's niliwahi kupewa inside information na jamaa alikuwa anafanya kazi TANCONSULT wakati nabid kazi fulani na of course jamaa liyenipa hiyo inside info alikuwa siyo mchagga lakini wachagga walipogundua hili jamaa libidi wamfukuze kazi lakini baadae ilibidi wamlipe pesa nyingi sana kwani alishinda kesi ya kufukuzwa kazi

Inshort nilishinda ile tenda lakini ilibidi ni subcontract kwa wadosi fulani pale mjini.

Hao interconsult ni kweli nakumbuka in 90's walikuwa ni Machame tupu lakini sijui kama wamebadilika kutokana na dunia na wakati na kama watakuwa hawajabadilika then wanakazi kubwa
 
Phillimon Mikael.

najua wewe una matatizo na hukuanza hapa toka kule Tamko la chadema, unapenda kijinga, nimekupa fact za Mramba mbona sikumtaja DR.Chami? mmoja wa wafanyabiashara waliopewa kibano na Mramba na Kittlya ni bakhressa. Zacharia na superdoll. mtafute Mramba(mr.fupi0 apinge hili, au Kittlya.

nimekupa fact nyingine kuwa mdogo wake Lauwo ni form six na amepewa sehemu ambayo haifanani na elimu ndogo yake aliyonayo kisa ni mchagga, na nimekupa mfano halisi wa Benny kijana wa kinyakyusa aliye na masters toka UK lakini aliona cha moto toka kwa wachagga wa TRA.

majina niliokupa yote uliza au fuatilia.

na kichuguu amekueleza kuna mtu ana B.A Education alichukuliwa na TRA kisa ni uchagga, kifupi kuwa mchagga ni qualification tosha huhitaji kingine TRA.

NAKUBALI wachagga mmesoma au ndio degree za kina mrema sisi waswahili hatuna?
mikael ulitolewa kamasi na chinga kwenye topik ya Mbowe na chifupa hapa huwezi.

au hata Mbowe alipopewa kazi na mtei benki kuu alikuwa msomi? hujui kisa ni uchagga na ukwe?

TRA INABIDI IFUMULIWE SANA kama NSSF ambayo ilioza kwa uchagga na sasa inafanya wonders jee director general wake ni mchagga?

taasisi yeyote inatakiwa isiwe na misingi ya discrimination katika hali yeyote mfano ukabila iweje TRA? INA MAANA sisi waswahili hatusoma hata RRO? AU ma assessors wa kodi?

acheni hizo.

Samvula chole.

mbunge aliyelalamika upendeleo wa barabara bungeni ni mbunge wa nzega alikuwa ana mlalamikia mr. fupi(mramba) kwa kupendelea kwao. mfano halisi alitenga bilion 17 kwa barabara ya jimboni kwake huku barabara ya kusini dar- lindi imetengewa bilion 1 tena ni barabara muhimu. hao ndio wachagga au mikael barabara hii kwa vile ni ya waswahili? hivyo haijaenda shule?
 
Mswahili,
ndugu yangu nimekubali na hoja zako kwa sababu moja kubwa sana. Nimeitazama list nzima ya viongozi wa juu ambayo haina Ukabila lakini hawa watu hawakupata ajira zao through process ya TRA ila waliteuliwa na serikali moja kwa moja nje ya ofisi ya ajira ya TRA. Serikali haina Ukabila isipokuwa kila tunapotoa nafasi za kazi na hasa ile ya Human Resources hapo ndipo penye source ya Ukabila.
Nimekuelewa sana na kwa sababu Watanzania wengi walalhoi hawahitaji kuwa ma director au commissioner ila nafasi za kwaida (ajira) kulihudumia taifa, hapo ndipo tunapozungumzia.

Nimekubali pia kuna sehemu kibao nchini ambazo wapo watu wameweka kaka zao, dada zao, shemeji zao na kila aina ya KUJUANA kiasi kwamba haiwezi kutafsirika nje ya Ukabila hasa pale Wachagga na Wanyakyusa wanapoingiza mila zao. Mtanisamehe ndugu zangu wa Kili na Mbeya maanake palipo na ukweli inabidi tuseme na pengine mtaweza kulitazama swala hili kwa sura nyingine. Pia kuna kijimila dulani kuwa usipoajiri jamaa zako basi wewe zoba kama vile kutoiba ama kuchukua rushwa ukiwa ktk nafasi nyeti!...yaleyale ya Ujanja ni Kupata!
Wachagga na Wanyakyusa kila mtoto aliyezaliwa na damu yao iwe hata toka kwa Mwanamke huhesabika kama wao. Pamoja na kujichanganya kote kwa Makabila lakini hawa jamaa zetu wamekataa kabisa kutambua mtoto nje ya makabila yao na kujichanganya kwao ni ktk kuzidisha nguvu ya makabila yao.
Kuna kila haja ya kuendeleza mada hii tupate picha halisi ya mchezo huu ambao ulikuwepo wakati wa Nyerere na ulikuwa ukipigwa vita vibaya sana. nakumbuka kuna vijana marafiki zangu walikuwa mashushushu enzi zileee. Kazi yao ilikuwa kuwaibua viongozi ndani ya mashirika ambao huwapendelea ndugu na makabila yao ktk nafasi za kazi.. ndio maana mliona uhamisho wa baadhi viongozi wazuri wachapa kazi ktk baadhi ya sehemu kutokana na kosa ambalo lilionekana dogo tu... Ukabila!
 
nilishangaa Mwanakijiji anajibu hoja kwa kutuletea hotuba za Nyerere

Nyerere alikuwa mtoa hotuba mzuri sana lakini wakati huo huo hakuwa mtekelezaji na leo imefika point ya kuzungumzia haya ina maana watu washanyaza vya kutosha lakini duku duku lipo

Tazama idadi ya wafanya kazi wa serikalini wano pewa nafasi ya kuja kusoma Nje utaona tuuu kuwa wengi wao wanatoka mikoa ya juu au ni wachagga

Sidhani hii inahitaji mtu awe Genius kujua hili

actually hata huyo mwanakijiji asingefika hapo alipo kama si ukabila na hilo yeye analijua
 
samnvulachole,

Kuna tofauti kubwa sana wakati wa Nyerere na leo! kulikuwepo na watu wakitazama ubadhilifu wa viongozi ktk nafasi zao hasa huku chini tunakolilia. Sema Nyerere aliwabeba marafiki na wafadhili wake wengi ktk nafasi za juu bila kujali makabila yao. Viongozi ambao leo wanatumaliza tukiwa hai!
Jaribu kutazama kinachozungumziwa hapa kuna nafasi mbili. Top position za ajira toka serikalini hazina Ukabila ila wahusika ndio wenye kuukuza ktk kulinda nadhani rushwa linalotembea nchini sasa hivi.
 
mswahili wewe na chinga mnafanana au inawezekana wewe ndio chinga ..kwani wote mnatumia style moja ya uandishi yaani PROVOKING STYLE..
hoja unazotoa zinajadilika ,lakini bado tutarudi palepale...nafasi za juu za kazi pale nyingi ni PRESIDENTIAL au MINISTERIAL APPOINTMENT .sasa tukianza na hizo utakuta makamishna pale wanaidhinishwa au kuchaguliwa na rais...ukija kwa wakurugenzi wa vitengo ni approval ya waziri...TRA inayo bodi chini ya dr mama chigoroga ,,,..sijui huyu ni kabila gani ...wakuu wengi wa vitengo huidhinishwa na BODI...na hao si wachagga.
ukija kwenye utendaji wa TRA yenyewe .kila siku unaendelea kuboreka na sasa wanakusanya billioni 250...mbona hilo husemi...halafu kingine kwa nini unakua sceptical just kwa TRA wakati nchi hii ina taasisi nyingi...mbona hatusemi wakati mh KITWANA KONDO alipopewa uenyekiti wa bodi bandari na mzee mwinyi mnakumbuka alivyojaza wazaramu bandari kuanzia JANGUO lakini still nafasi za ma engneer,wahasibu,ets hakupata WASWAHILI wa kuwaweka ,....mimi ni yangu nataka ukubali kuwa kabila la mtu lisiwe kikwazo kupata ajira au kuandamwa ...mbona hulalamiki muhimbili au madaktari wengi ni wakuja...hutaki udaktari wewe...au tatizo ni pesa.
hilo suala la laowo na mdogo wake sijalifanyia utafiti so i cant comment ...kama ni kweli hana sifa ni halali aondolewe na nitaunga mkono kama ushahidi wa wazi upo ila kama ana minimal requirement ,basi ...suala la mtu mwenye BA[ed] kupata kazi pale si ajabu na wala si wa kwanza kuchukuliwa ..TRA wanacho chuo cha kodi ,pia wana kitengo cha ELIMU YA MLIPA KODI chini ya P.MMANDA[kaMA sikosei]...hapo wanatakiwa watu wenye elimu ya uhusiano na elimu..
mbowe kupata kazi enzi ile haikua ajabu ,kumbuka AZIMIO LA MUSOMA watu walitakiwa kufanya kazi serikalini mara baada ya kumaliza six pale wanaposubiri kuingia mlimani ..na kama bahati mbaya ukifeli basi unaendelea na kazi unasubiri kujiendeleza ukiwa kazini...so kwa watu wanaojua hili wata ku offsmart.
kuhusu NSSF naona hakuna tofauti kati ya dau na mkullo au mattaka...tena sanasana DAU bado hajafanya vivid investment kulinganisha na enzi ya kina mkullo au mattaka [hata mkimsema ..jamaa ni kichwa ]....ila aendelee kujitahidi ..na nafikiri ni mtu anayetumia sana propaganda chini chini..natambua ni PAN AFRICA mzuri na mtoto wa mjini ,,,but we want more results...
bakhressa na zakharia hawawezi kuonewa ,serikali inakubali juhudi zao hata huyu mengi hawakuti hata kidogo...wana mchango mkubwa mno hata kwenye kodi...na wanaleta ajira..
 
Phillimon Mikael.

inaonekana wewe ni kichwamaji kweli. nimekupa fact hizo unabisha tu. na machagga mwenzio MMANDA umeona statement yake hapo kuwa mbona hata jeshini kuna ukabila. alitakiwa kusema kuwa kweli hili ni tatizo tutalifanyia kazi. lakini si kusema hata jeshini. huwezi kuhalalisha kosa lako kwa kuonesha kosa la mwingine.

unasema waswahili hatujasoma jee mhasibu mkuu wa kwanza Mohamed Abood alikuwa mchagga? na hata MR.Ally Mwinyimvua alikuwa mchagga? na huyu ndiye aliyekuwa nafasi ya blandina nyoni,unadai masomo ya uhasibu wanayajua wachagga.

Mkullo ana ACCA toka 74 jee ni mchagga? wakati bodi ya NBAA ilianza 1972-3 huyu ni mswahili.

uliza mapato na mtaji waliona nao NSSF hivi sasa ndio ujue dr dau ni nani? kwa taarifa yako ya wachagga wenzako huyo SI DAU ni dr. Dau ana phd ameipata akiwa na miaka 29 tupe mchagga au kitillya wako na phd gani?
wachaga kama wasomi msingechoma benki kuu. na hata sasa wizi mkubwa umetokea BOT, hao ni wachaga wenzako.
 
phillimon.

watafute Bakhresa na Zacharia uone TRA inavyotumiwa vibaya kama chombo kwa kuendeleza wachagga. mr.fupi(mramba) anapitia humu mbona hakanushi? na fuatilia ile shule yake iko jimboni mwake uone michango ilitoka wapi?

mwalimu Nyerere aliwahi kuunda tume kuchunguza tuhuma kama hizi Bima,hakukanusha tu.

nimekupa data za kuanzia airport hadi bandarini kukuonesha watendaji wa kichagga badala ya kujibu hoja unapayuka tu.

mwisho mswahili kuwa chinga sawa tu kwani chinga na mswahili wanatafuta riziki zao kihalali, ila ukinifananisha na alex massawe ambaye haoni haya kutoa roho ya mtu awe tajiri hapo muhali ndugu yangu.

au huwezi kuona bakhresa au mfanyabiashara wa kiswahili kukwapua pesa za msaada wa ukimwi kama ilivyotokea kwa wafanyabiashara wa huko kwetu.waswahili tuna aibu au haya.
fuatilia vyeti vya salim yusuf wa TRA ambaye ni mtu wa kwenu na anavyeti feki.
philimon ina maana professor Malima nae alikuwa mchagga? unadai hatujasoma.
 
Unajua kuna kipindi mchagga mmmoja alikuwa katibu pale foreign, akajaza wachaggaa weeee ambao mpaka leo ni 75% pale, sasa ikawa kila akipeleka majina ya kuwa promoted kwa rais jaama alikuwa akiweka wachagga tu, ndipo waziri wake akaamua kupunguza majina na kuweka majina ya makabila mengine, wakati ule Mwalimu akiwa rais, yule waziri ananiambia kuwa yule katibu alienda kumshitaki kwa Mwalimu kuwa huyu waziri hafai maana ametoa majina niliyoyaweka,

Mwalimu akawaita wote wawili waeleza kesi yao, anasema huyu katibu mchagga alikuwa akitokwa na machozi mbele ya Mwalimu kwamba aliowaweka pamoja na kwamba ni Wachagga wenziwe ndio wanaofaaa, na hawa kina Bernad Muganda, Mwasakafyuka, Bandora, Salim, na Diria ambao yule waziri alikuwa amewaongeza walikuwa hawafai, anasema toka siku ile yeye na yule katibu mkuuu hawaelewani kabisaaa,

Ndugu zetu acheni hizo ndio maana sera ya majimbo inaogopewa sana, na the fact kwamba inatoka huko kwenu!
 
mswahili unafikiri kila mtu ni mchagga...anyway ukisoma post zangu utagundua kuwa mimi huwa simkubali mtu kwa kuangalia kabila...ndio maana hapo juu nikakuambia kuwa ushahidi wa kazi wa mkullo unaonekana kuliko wa dau ambaye hata kama atakuwa na mafanikio ni yakwenye maKARATASI tu....

ndio maana nkakuambia inaonekana wewe unachojua ni udini na ukabila tu...hao kina mahd abood nA mwinyimvua nilikuwa siwajui lakini those are bygones ,sasa tuwahimize vijana wa leo bila kuzingatia dini kusoma...kupata phd ukiwa na miaka 29 ,ni jambo la kawaida sana hakuna la ajabu hapo,siku hizi watu wenye phd wapo wengi kiasi kuwa wengine hawapendi kuitwa DR...

huyu dau inaonekana anafanya sana kampeni za chini chini,..nakubali kuwa ni msomi mzuri tangu akiwa kule bandari...but sidhani kama anahitaji kuwa affiliated kwenye hoja za udini au ukabila ili kupanda cheo ...hapa kati kati alikuwa tipped kuwa GAVANA WA CENTRAL BANK...

nakushauri uache chuki za kikabila na direct attacks,ukiendelea hivi utabakia kulalamika kila siku ,,..lazima kama mtu anakuzidi ukubali na uweke mkakati wa kujitahidi....muelekeo unaotoa ndio umedumaza elimu kwa baadhi ya jamii kwa kuamini kuwa wanaonewa ,,,,
 
kwani waziri wa fedha ni mramba?pale sasa hivi wapo zakia amdan meghji [waziri],mustapha mkullo[naibu],na abdisallaam issa khatib[naibu] hao pia ni wachagga..hao si ndio wamemuweka kittlya pale...na wakiamua kufanya maamuzi bila kuangalia merits wanaweza ...lakini hawafanyi hivyo kwa kuwa wanaelewa umuhimu wa profffessionalsm...ina maana pia wanajua kuwa bakhresssa anaonewa ...you cant be serious..kwa level ya ssb ana access na president 24 hrs...
huko airport unamuongelea nani ? eng.tesha na temu? na eng mama muyaga elizabeth pia ni mchagga? na naibu waziri anayesimamia viwanja si maua daftari ....guys people keeps there posts on merit.
mengine nimeyasoma ,it seems it is a collective or organised attack on certain tribes and that is the problem....mamamia!!!!!!!
 
Mswahili,'
Karibu tena. Asante kwa facts ulizomwaga. Lakini unajua uwongo ukirudiwa mara kwa mara watu wanaanza kuamini. Freeman Mbowe hakuajiriwa na Mtei benki kuu. Aliajiriwa na Charles Nyirabu (RIP). Hii nilishawahi kuisema. Wakati huo Mtei alikuwa Washington DC kama Mkurugenzi wa Benki ya Dunia. Facts are facts. Asante.
 
Phllemon mikael,
Ndugu zangu nafikiri itakuwa jambo zuri sana ikiwa tutajibu hoja kwa hoja!..Mswahili kayasema yake ktk kifungu chaajira zinazotokea Human resources ya TRA, Bandari na sehemu nyinginezo kutokana na mtu mmoja tu -Mwajiri wa sehemu hizo. Nadhani hapa hoja ipo wazi na vizuri ikiwa tutamjibu kulingana na hoja yake... Je, kweli waajiriwa wa sehemu hizo hukutana na vipengele vya Ukabila... maanake ktk CV yako kama jina na ubini ni moja ya sababu sidhani kama kuna haja ya kuendelea kutetea hali kuna hatari kubwa ya kuwa na tabaka hizi.
Naamini kabisa kukataa maradhi ama kutokubali kuwepo kwa gonjwa linaloambukiza ni moja ya kueneka gonjwa hilo zaidi ya mipaka yake. Lishughulikiwe ipaswavyo kabla halijasambaa!

Jasusi,
Kuhusu Freeman huyu mswahili ana lake nadhani personal! kwa sababu sisi tunaemjua Freeman tunafahamu lini alianza uhusiano na mtoto wa Mtei. tena wakati yuko benki kuu alianza na kitu cha uhakika Carlo Nyimbo kisha mchezo ukaisha na akaanguka na kitu kingine malkia Serah Kida ambaye alikuwa naye hadi mwishoni mwa 1980s kama sikosei.
Sasa haya ya Mtei nadhani katumia hesabu za Mkapa 2+2=22.
 
Hakuna kitu kinachofurahia kama kuuchonga ukweli. Mswahili kwa kutumia takwimu na orodha ya majina ameonesha kuwa kuna Ukabila. Bahati mbaya watu wameanza kuamini sababu ya kuona majina ya watu wa kabila moja! Kinachosikitisha zaidi ni kuwa badala ya kujiuliza kama huo ni ukabila au kitu kingine tunakubali maelezo hayo na tunaanza kuamini kuwa kuna ukabila.

Nilivyoonesha kwenye jibu la kwanza kabisa kuwa madai ya ukabila hajajaanza leo. Miaka 30 iliyopita kuna watu walianza kusema maneno hayo hivyo kwanza tukubali kuwa kuna watu ambao hawajabadili maono yao licha ya muda kupita na hakuna kitu kinachoweza kufanyika kinaweza kuwabadili mawazo yao.

a. Hivi watu wote hao waliotajwa wangeamua kubadili majina yao na kuweka mwisho majina ya "Ndomba, Likuli, Bayo, Salum, Haji, Zoba" n.k itabadili madai hayo? Kwa mfano wachagga wote kuanzia sasa waanze kuomba kazi kwa kuficha ubini wao itaondoa wao kupewa nafasi za kazi?

b. Katika majina yote yaliyotajwa na Mswahili na wengine humu ni wangapi kati ya watu hao wanajuana? Je viongozi hao wachagga ambao wameajiri watu chini yao (huko Human Resource) ni wangapi walikuwa wanafahamiana na waajiriwa hao? Kabla sijarukia na kusema ukabila nataka nifahamu kwanza je wangapi kati yao wanafahamiana? Je Kittilya anafahamiana na Lymo, Macha, au Mrema? Je anafahimiana na Mkullo, Ngosha n.k ambao nao aliwaajiri? Nioneshe kwanza kuwa hawa wote hawafahamiani au kujuana kwanza ndio unioneshe ukabila!

c. Zaidi ya yote, naomba mtu anioneshe kuwa kwenye nafasi ambazo zinahitaji elimu kuna mchagga, mnyakyusa, au mhaya ambaye ameajiriwa ambaye hana elimu hiyo. Na hapa sizungumzii nafasi za kisiasa au kuteuliwa. Nazungumzia nafasi za kikazi. Kama kuna mchagga ambaye hana elimu naye amepewa kuongoza kitengo au idara ambayo hana ujuzi nayo badala ya kuuliza kama ni ukabila, kwanini tusiulize kwanini apewe nafasi hiyo, je anafahamiana na bosi?

d. Hivi tatizo kubwa Tanzania ni ukabila au undugunization? Mfano wa mama Mkapa je hao wote "waliopewa nafasi" ni kwa sababu ni wachagga au kwa vile ni ndugu? Hebu tuangalie maneno ya Mswahili:

"kamishina wa ushuru na forodha George Lauwo amempa kazi mdogo wake mr Lauwo "
alimpa hiyo nafasi kwa vile ni mchagga au ni ndugu yake?

chukulia mfano daktari wa mkapa alikuwa dr.Maro mchagga na ni ndugu wa mama Mkapa
Je alipewa nafasi hiyo kwa vile ni mchagga au kwa vile ni ndugu ya mama Mkapa? Kama kilichoangaliwa ni uchagga kwa nini wasimpe Dr. Minja ambaye anaqualification kama za dr. Maro?

mpiga picha wa Mkapa na sasa Rais Kikwete ni mchagga na ndugu wa mama mkapa freddy Maro
Je alipewa nafasi hiyo kwa vile ni mchagga au kwa sababu ni ndugu ya mama Mkapa? mbona wapo wapiga picha wengi tu kama Mroki Mroki?


TRA GENERAL COMMISSIONER ni Kittlya Harry huyu ni mchagga na ndio mkuu wa TRA NI mchagga aliyebebwa na Mramba basil mchagga mwenzake.
Je Kittlya alipewa nafasi hiyo kwa vile ni Mchagga au kwa vile anafahamiana na vigogo wengine wa serikali akiwemo Mramba? Mbona hawakumpa nafasi hiyo Tarimo ambaye ingawa ni mfanyabiashara mkubwa lakini hafahamiani sana na Vingunge?

nakupa zaidi RRO wa airport alikuwa Kimaro ambaye ni mchagga,

RRO long room alikuwa sabuni nae kilimanjaro, ukienda officer in charge majahazi alikuwepo Lyimo nae mchagga akaja Mushi nae mchagga, na ukienda RRO BANDARINI alikuwepo mzee Maleko mchagga bandari iko chini yake kabla yake alikuwepo Foyi nae mchagga,RRO wharf alikuwepo Kisaka mchagga ambaye sasa ni deputy commissioner,hawa ndio watendaji wanaopitisha ushuru.
Je, hawa wote, (i) hawana elimu inayowafanya wastahili nafasi hizo? (ii) wanafahamiana na nani? (iii)nioneshei kuwa watu hawa wote walirushwa nafasi hizo yaani hawakuanzia chini na hivyo waliwapita watu wa makabila na mengine na kupewa nafasi hizo

Human resource & adminstration yupo mtu wa kilimanjaro hapo ajira haendi kwingine. halafu fuatilia watendaji wa chini ya hawa policy makers.

fuatilia RRO/MANAGERS, fuatilia officers in charges wa long room(Dar),na boarders, then utapata jibu vipi kilimanjaro walivyothibiti idara hii nyeti.

nakupa zaidi RRO wa airport alikuwa Kimaro ambaye ni mchagga,

RRO long room alikuwa sabuni nae kilimanjaro, ukienda officer in charge majahazi alikuwepo Lyimo nae mchagga akaja Mushi nae mchagga, na ukienda RRO BANDARINI alikuwepo mzee Maleko mchagga bandari iko chini yake kabla yake alikuwepo Foyi nae mchagga,RRO wharf alikuwepo Kisaka mchagga ambaye sasa ni deputy commissioner,hawa ndio watendaji wanaopitisha ushuru.

na documents zote za bandari Dar lazima zinapitia kwa head declaration officer(HDO) MR. MCHIRA huyu nae kilimanjaro,

officer in charge wa container terminal bandari dar,ni mr. steven mchagga,
officer in charge border ya Tunduma ni mr, Niko ni mchagga na ukienda border ya Namanga kuna mr. Mosi nae mchagga,

Kwa mtu ambaye macho yake hayajafunzwa anaweza kushtuka akikabiliwa na data kama hizi, na kujikuta akikubali bila kuhoji kuwa kuna ukabila. Kabla miye sijashawishika naomba Bw. Mswahili atufanyie mambo yafuatayo.

a. Leta orodha ya vitengo vyote vya TRA na utupe viongozi wake wa juu wa vitengo hivyo makao makuu

b. Leta orodha ya mipaka yetu (Mipaka ya TZ na Uganda, TZ na Malawi, TZ na Rwanda, TZ na Burundi, TZ na Kenya na bandari zote ) na viongozi wake na makabila yao

Sasa, kabla hatujaenda mbali lazimi nikiri jambo moja kuwa nitakuwa mwongo na mzandiki kama sitakiri kuwa wapo Watanzania ambao wanatanguliza ukabila katika mambo fulani fulani na anga hizo siyo za Wachagga peke yao! kuna wasukuma wanaoependelea wasukuma wenzao, wandengereko wanaopendelea wandengereko wenzao n.k Watu wenye hisia hizo haiwajilishi kama ni wachagga au la, unless Mswahili aniambie kuwa katika ya binadamu wote waishio Tanzania wenye hisia ya Ukabila ni Wachagga peke yao!

Zaidi ya yote, wakati wengine wanaona ukabila katika hayo yote mimi bado naona kufahamiana na kujuana zaidi. Na ukiliangalia hili utaona kuwa watu wengi bila kujali makabila yao wameajiriwa kwa vile wanajuana na mzee fulani au familia fulani. Una nafasi kubwa ya kuajiriwa mahali fulani Tanzania ukiwa unajuana na watu wa humo kuliko ukiwa mtu wa kabila la mmoja wa wawili wa viongozi wa humo! Ni wangapi hapa tumepata nafasi kwa sababu wazee wetu au rafiki zetu wametuunganisha na marafiki zao!? Kwangu mimi tazio la undugunization ndio linalotishia maendeleo ya nchi yetu zaidi kuliko huu ukabila hewa!!! Bado sijashawishika kuwa kuna ukabila Tanzania kwa kiwango ambacho Mswahili na wengine wanataka tuamini!! Ni rahisi kudai ukabila kuliku undugunization, kwani ukabila unawahusu watu wa kundi fulani, na undugu unaweza kuwa unatuhusu sisi!!!!!!
 
Mwanakijiji,
tatizo langu sio kuamini kuwepo kwa Ukabila nchini ila kama nilivyosema Majambazi bado wapo hata kama nchi itadai kukomesha Ujambazi...
Na Ubaguzi wa aina yeyote bado utaendelea kuwepo duniani muhimu ni kundelea kuupiga vita.
Kukataa kwamba hauwezi kuwepo hapo ndipo naposema ni kujidanganya. Ni kweli kwamba mtu mmoja ama kundi la watu wachache haliwezi kuunda hitimisho la nchi nzima... Na ndio maana nakubali kuwa Tanzania hakuna Ukabila kwa tafsiri ndefu ya Ukabila ktk nchi isipokuwa kuna hivi vijidimbwi vya mbu ama magugu yanayojiotesha ktk shamba la kahawa ambayo hata Yesu alitaka yang'olewe, magugu ambayo yanaweza hata kuota juu ya jiwe.
 
Nafikiri tufanyie kazi yale yaliyosemwa na wala si kuangalia aliyetoa hoja ni Mswahili. Je kuna ukweli katika aliyoyasema? Je kuna wengine wamekutwa na haya? Tukumbuke lisemwalo lipo ......................................... Data zipo nyingi lakini ni za ukweli au ni ubabaishaji?
 
Back
Top Bottom