Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

dua fungu la ule msaada wa barabara za kili ,ulikuwa ni msaada wa mfadhili ambaye alielekeza specifically pesa ziende wapi,..hata wafadhili wana priority zao..kwa mfano hizo pesa zili cover pia kuboresha barabara kuelekea hifadhi ya kilimanjaro kupitia njia ya machame na marangu...pia kipindi hicho hicho barabara ya arusha to ngoro ngoro ikajengwa kwa kiwango cha lami....nafikiri kama sikosei hata ile ya kupita serengeti imefanyiwa ENVIRONMENTAL IMPACT ASSESSMENT...unajua wazungu wako very sensitive kusaidia maeneo ambayo pia na wao wanayatumia ,sasa kwenye vivutio vya utalii ni kati ya sehemu hizo...na hata siku moja huwezi kukata pesa ya kupeleka maji nzega kutuka lake victoria upeleke masaini...hiyo ilikuwa zamani na ikatuletea sifa mbaya ,,sasa hivi project management zinashirikisha wafadhili kuanzia hazina....
NIKUPE MFANO WA MILLENIUM GOAL mfuko wa wamarekani kwa nchi masikini ,juzi tu wamekuja hapa na wanafungua ofisi pale hazina ili kusimamia pesa zao zitumike kwa malengo waliyoweka.



PH

Mjomba mimi naweza kukusahihisha mambo mengi tu uliyosema hapo juu na yote ni katika kuweka FACTS sawa

Ninafanya kazi na organisation ambayo inatoamikopo katika nchi nyingi zinazoendelea na naweza kukuhakikishia kuwa huwa tuna tatizo kubwa sana katika baadhi ya nchi na hususwa za Africa kama kenya, Zimbabwe,Nigeria,Ghana,Zabaia,Uganda,Sudan na bila kuisahau Tanzania katika suala zima la kupunguza umasikini kuna UKABILA wa hali ya juuu katika proposals zao na hii inatokana na hao wanaowakilisha reports zao kuhusu miradi gani ifanyiwe kazi. Nitakupa mfano mdogo back in 90's Kenya kulikuwa na malalamiko makubwa kuhusu miradi mingi kwenda Rift Valley na Western Kenya kama Nyanza na Kakamega ili hali watu wanakufa na njaa Trukana na Marsabit vile vile mikoa ya Pwani iliachwa na ikapelekea movement ya jamaa wa COAST kutaka kujitenga na ikaundwa tume....kumbe baada ya uchunguzi kufanyika ikaja gundulika kuwa kulikuwa na Wakikuyu wanawapiga bao wajaluo ambako wao nao waliona isiwe tabu kwani wanao vigogo wao ambako walitaka investments ziende na kwao...

Si kweli kuwa wazungu ndio wenye kuweka priority bali ni nchi mwanachama kama Tanzania ambayo huwa tunahitaji tupate mikakati yao ya kupunguza umasikini na hapo ndipo jamaa wa Mipango wanawasilisha miyo Poverty Reduction Strategy Papers (PRSPs) na kusema ukweli ni kuwa mikoa mingi inayopewa kipaumbele mfano wa kurekebisha infrastructure Tanzania ni mikoa ya Kaskazini LAKINI SIYO KUTOKANA NA PRESHA ZA WAZUNGU kama ulivyosema bali

Vile vile umekosea kusema kuwa MILLENIUM DEVELOPMENT GOALS ni mfuko wa Wamerekani. Huuu ulikuwa ni mfuko ulioanzishwa na UNITED NATIONS kushirikisha member states zote za UN na kulikuwa na GOALS 8 ambazo walipeana kama njia za kumaliza umasikini na ofisi iliyofunguliwa DAR japo unaweza kufikiri iko independent lakini wako chini ya Country office ya UNDP


nimeona bora nikuweke sawa na hizo facts hapo juu
 
Mkandara,

nami nimekuwa naambiwa na hawa watu wa maliasili kuwa ktk game reserve activities za uwindaji hurusiwa na sio national park, watu wa utalii wanaweza kufafanua zaidi hilo.

pm + Dua

Barabara za kuzunguka Mlima i.e. Marangu-Tarakea-Kamwanga awali ulikuwa mradi mmoja, wafadhili wakaja na zao kulingana na pesa watazo tupa na kuchagua vipande, serikali ikalazima kuigawa na kuwa Marangu-Mkuu (Mwika Kilacha inclusive)-NORAD, Mkuu-Tarakea-BADEA na Tarakea Kamwanga ni GOT. mawasiliano yanaendelea kati ya EU na GOT kufadhili ile barabara toka Hai mpaka lango jingine la kupandia Mlima. CBA sna EIAs zote zilizofanyika zaonyesha kuwa miradi yote hiyo inalipa, credits to Meghji, Mramba na Magufuli. Pm umesema kweli barabara ya mwika kilacha automatically ilifaidika kuingizwa kwani nayo ilionekana ni kiunganishi kizuri na Holili (TZ)/Taveta(Kenya).

Back to the mada.
Ukabila unaozungunzwa hapani experience/perception binafsi za watu. mfano leo nikienda kuomba kazi, nikakutana na wenzangu watano (jumla tukawa sita), nafasi iliyo wazi ni moja. Bwana mkubwa wa ile sehemu tunayoomba kazi lets say ni Mhaya na miongoni wa wasailiwa yumo mhaya. impression nitayokuwa nayo mwanzoni ni kuwa wote tulioitwa ni competent, kwa hiyo yeyote aweza chukuliwa NOW akichukuliwa mhaya picha ya kwanza itayokuja akilini mwa wengi wetu itakuwa "kwa kuwa ni mhaya mwenzake".....regardless ya kwamba Bwana mkubwa mhaya anajuana naye au hamjui. sasa je tuuite huo UKABILA?? YES & NO!

NO, why
1. wote tuko competent na mmoja wetu lazima apate regardless of his/her kabila
2. There is a possibility ya ambaye si mhaya kuchukuliwa
3. Ni haramu kumtuhumu mtu aliyepata kihalali riziki yake

YES, why
1. %ge kubwa ya panel ikiwa ni wahaya, kutakuwa na ka-roho fulani ka'yule ni wa kwetu" trust me, makabila mengine hayana aibu
2. Nguvu/influence ya bwana mkubwa na uhaya wa huo bwana mkubwa

Serikalini haya mambo yako saana both KUJUANA na UKABILA, yote hii haina budi KUPIGWA VITA.

NB: nimetumia Wahaya kwa kuwa ni moja ya kabila lilosemwa. so ktk maelezo yangu waweza ku-substitute na Mchagga au Mnyakyusa vile vile. sina bifu na kabila lolote.

Ni rahisi sana kwa mtu ku-judge, inakuwaje watu waliosomea mambo ya tax wasipate ajira na mtu mwenye BSc/BA (Ed) apewe nafasi inayohusu taxes??, huyu bw/bi anatakiwa aende kufundisha, vinginevyo abadilishe fani aende akasomee kwanza ndio aajiriwe kama ajira itakuwepo wakati huo "under competitive selection" short of that ndio hizo speculations za ukabila na kujuana zina-emerge.

Naunga mkono, kuwe na kamati huru ya ajira, na ikiwezakana tutumie consultants e.g KPMG, PriceWaterHouse (wasiingiliwe though), especially katika hizi Authorities za serikali zilizo na uwezo wa kuajiri bila kupitia utumishi. Through my experience kamti ya uajiri ya UTUMISHI are doing a very good Job!!
 
that was A EUROPEAN UNION ,and JAPANESE GRANT,mkandara kilimanjaro kivutio kukubwa ni MLIMA ..SO pamoja na mambo mengine uboreshaji wa miundombinu ya haya maeneo ambapo hata wizara ya maliasili enzi ya mama meghji walishirikishwa na kwa kili walilenga kurahisisha usafiri kwa kuboreshanbarabara mbili za kufika kwenye mageti ya mlima upande wa machame na ule wa marangu ....sasa kutoka marangu hadi rombo serikali iliomba xtra funding ili kulink na mpaka wa HOLILI ambao pia ni kianzio kizuri cha kodi kwa serikali''
kwa upande wa dar es salaam ,barabara iliyonufaika katika mpango wa utalii ni ile ya bagamoyo road to kunduchi and bahari beach zone na ile ya bagamoyo to white sands zone hotels...



Hoja yako iko weak kwa sababu DODOMA,TANGA na MTWARA kote huko kuna WAGOGO,WADIGO na WAMAKONDE wanatoa KODI zao na wanastahili same investments kama zinayoenda sehemu yoyote ile TANZANIA
 
Mzee Es

heshima yako mkuu Mimi ni Ole na sio Mswahili au Tafit, Mlalahoi, Mtaliii or Chinga. I am just Ole.
 
Nashukuru mkuu ES

Hawa watu mjini wametukuta na sasa wanataka kutufanya wajinga, mwinyi kama wewe kumbuka enzi hizo kuna timu ya mpira kama Nungu au cosmopolitan utamuona mikael kiongozi wa timu? hata Fat yetu kulikuwa na waswahili wenzetu utakutana na kina el-mamry,mnonji, abubakar mwilima, mohamed kassanda, n.k
sasa wamevamia hadi starehe zetu za mipira ndio utaona akina dismas ndumbalu wanagombea TFF. yaani wametuulia mashirika yetu ya umma na sasa hadi kwenye mipira wanatuvamia. huyu mikael anamjua mzee Tabu Mangara? shiraz shariff?

DUA.

huo uongo wao umefika kikomo hakuna wafadhili wanaotoka masharti selous ndio mbuga kubwa duniani.
na huo ndio ulikuwa ujanja wa msuya cleopa kudanganya watu
 
sellous ni game reserve[the largest in the world] sio national park...so shughuli kubwa pale ni nature tourism,hunting katika baadhi ya maeneo ets..kuna ugomvi na WANAMAZINGIRA katika kufanya shuguli za barabara pale ,wana argue kuwa activities za aina ile zinaweza kuharibu FLORA and FAUNA ,or to scare animals ,wanamazingira hawataki ...kama pia wanavyovutana kujenga barabara na airports SERENGETI ambako wanaogopa wanaweza kuwatisha wanyama wakakimbilia kenya.....



I detest hawa wanamazingira wanaokuja Africa kutuambia miradi gani tufanye na ipi tusifanye

Unakumbula walivyoleta tafrani kuhusu MRADI WA KAMBA (NADHANI ILIKUWA MAFIA)?

These people should concentrate na nchi zao..imagine UK govt wants to upgrade its NUclear Trident at £70 billion halafu sisi kuwa na mradi wowote wa kutuingizia Riski watu wetu ishakuwa tabu

The bottom line to me these GAP year students that come to Africa as environmentalists should shove off back to where they are from

I have enough of green peace objecting every single DAM proect in Africa based on their illogocal conclusions eti tutaharibu mazingira...HALAFU TUISHI GIZA?
 
Labda turudi mwanzoni naona kuna watu walimiss definition yangu ya "Ukabila" Ndugu zangu, ukabila siyo kuhusiana na watu wa kabila moja, kufanya kazi pamoja na watu wa kabila lako au kuajiriwa na mtu wa kabila lako!! Ama sivyo, Mnyakyusa akienda mahali na kukuta bosi ni mnyakyusa ni bora asiombe kazi kwa kuogopa Ukabila!!! Na kwa mtindo huo Mkerewe akienda mahali akakuta bosi ni Mkerewe, Mweka Hazina ni Mkerewe na nafasi ya HR anayoomba yeye iko wazi, basi asiombe kazi!!! Hii ni hatari ndugu zangu. Ukabila ni hisia ya ubora na kustahili ya watu wa kabila fulani, hisia hii inatokana na watu wa kabila kuamini kuwa wao ni bora zaidi, wamejaliwa zaidi, na wana nafasi zaidi hivyo wanastahili zaidi. Ni hisia ya kutukuza kabila lako na kudharau, kukandamiza makabila mengine. Huu ndio ukabila ninaoelewa mimi.... Unless mtu anipe definition nyingine ya ukabila ama sivyo bila kuwa na maana tunayokubaliana tutaendelea kugongana mawazo.
 
sasa DUA unabisha nini,sema basi wewe nani aliyetoa PESA...mimi nimesema kile ninachofahamu..tena japan walitujengea kipande cha arusha to makuyuni ,karatu [ngorongoro]..tena pesa wakapitishia kampuni ya KONOIKE ambao ndio waliojenga barabara,,,..sasa unataka kubisha tu!!!! MIMI kama kitu sifahamu sichangii...na kama nikikosea nikiona facts nakubali.siwezi kudanganya purposely!!! wajerumani pia wapo european union ila wao binafsi ni wachangiaji wakubwa wa WWF[WORLD WILDLIFE FOUNDATION..ambao interest yao kubwa ni tackling of animal pouching[anti pouching],kati ya mengi wanayosaidia,,,



WWF, GREEPEACE na wengineo hao wote ni waharibifu na hawana INTERESTS ZA WAAFRICA

sisi huwa tunawaifa ni ma ECO-IMPERIALISTS

hawana lolote hawa
 
=phillemon mikael;21480 kuhusu NSSF naona hakuna tofauti kati ya dau na mkullo au mattaka...tena sanasana DAU bado hajafanya vivid investment kulinganisha na enzi ya kina mkullo au mattaka [hata mkimsema ..jamaa ni kichwa ]....ila aendelee kujitahidi ..na nafikiri ni mtu anayetumia sana propaganda chini chini..natambua ni PAN AFRICA mzuri na mtoto wa mjini ,,,but we want more results...


KWA HUMU NDANI TUNAKWENDA NA DATA hebu naomba utupatie DATA kiduchu tu:


Dr DAU aliingia NSSF lini?

Alikuta makusanyo pale NSSF chini ya MKULO yalikuwa kiasi gani?

Sasa hivi yako kiasi gani?

Je Kulikuwa na investments za kiasi gani?

Sasa hivi investments zimefikia kiasi gani?

Na ni Propaganda zipi anazitumia kuendesha shirika kubwa la wanachi la NSSF?

Na imekuwaje ameweza kusurvive pale muda wote huo tangu MKAPA amuweke pale?

Na ikiwa unaweza kuniconvince katika hayo then nitakuwa mtu wa kwanza kuanzisha "MWANAKIJIJI STYLE" kampeni zakumuondoa pale NSSF
 
Mwanakijiji,

watu wanzungumza experience zao na ku-conclude. YES it maybe Ukabila au kujuana and at the same time it may NOT be Ukabila au Kujuana. Definition yako ya Ukabila in-FIT kabisa na experience/mazingira waliyokutana nayo akina mswahili et al huko makazini.

hakuna anayesema ukiwa Mkwere leo uogope kumuona/kumuelzea shida yako JK kwakuwa ni mkwere NO. It is obvious haya makabila huko authorities yamesheheni and it is obvious TATIZO hilo la Ukabila/Kujuana lipo kutokana na experience za watu mbali mbali.

Mi nasema midhali TATIZO LIPO? then halina budi kutafutiwa ufumbuzi. JF lets bring our good brains together and come out with ideas to solve this irascible situation.
 
Mkandara,


Naunga mkono, kuwe na kamati huru ya ajira, na ikiwezakana tutumie consultants e.g KPMG, PriceWaterHouse (wasiingiliwe though), especially katika hizi Authorities za serikali zilizo na uwezo wa kuajiri bila kupitia utumishi. Through my experience kamti ya uajiri ya UTUMISHI are doing a very good Job!!



Tatizo hao KPMG na PWC ni sawa na ARTHUR ANDERSON na sina imani nao tangu issue ya ENRON na WORLDCOM

lete wengine lakini siyo hao uliowataja hapo juu
 
Ukabila upo kila kona ya serikali sasa kama kuna wengine mmeupa majina tofauti thats fine lakini upo ni kawaida Africa kwa hilo kutokea
 
Mzeee Ole,

Heshima yako mkuu, kumradhi unajua utamu wa kukata ishues, haya mzee tukate issues bro! Kumkoma nyani giladi!

Mzee Mswahili,

Heshima tena mbele, mkuuu mwaga mwanangu tumechoka na watindiga hawa meno nje kama wanacheka kumbe wamenuna! Hao enzi za Cosmo na Magram hawakuwepo, lazima tuteee tafu yetu Zaramo, waarabu wenyewe hawakutuchukua utumwa sasa itakuwa hawa watindiga!
 
Mzeee Ole,

Heshima yako mkuu, kumradhi unajua utamu wa kukata ishues, haya mzee tukate issues bro! Kumkoma nyani giladi!

Mzee Mswahili,

Heshima tena mbele, mkuuu mwaga mwanangu tumechoka na watindiga hawa meno nje kama wanacheka kumbe wamenuna! Hao enzi za Cosmo na Magram hawakuwepo, lazima tuteee tafu yetu Zaramo, waarabu wenyewe hawakutuchukua utumwa sasa itakuwa hawa watindiga!

Kumbe Mzee ES ni mkali kweli kweli; sikujua kuwa una uchungu sana na ukabila wa kizaramo. Sasa sijui tuelekee wapi kama watu tunaowategemea kutupa mawazo mapya nao ndio hao hao kama wewe. Nikipata nafasi nitarudia tena makala zako kuhusu Kikwete na Ditopile kwa vile hueda ulikuwa ukiziandika na mwelelekeo wa Uzaramo.

Kwa bahati mbaya ukabila umepitwa na wakati sehemu yoyote duniani. Nchi zenye keundekeza ukabila haziendelei chochote, na ndiyo maana utakuta kwenye nchi zote za magharibi ambazo ndizo za dunia ya kwanza, swala la uhamiaji ni kubwa sana.
 
phillimon.
.... ina maana professor Malima nae alikuwa mchagga? unadai hatujasoma.


tanzania tumekuwa na matatizo mengi sana tangu tupate Uhuru. Mojawapo lilikuwa ni lile la kuwapa watu madaraka ambayo hawayawezi.

Professor Malima alipopata skolaship ya kwenda marekani kusoma kati ya mwaka 1964 na 66 hivi wakati huo akiwa katibu mtendaji wa TANU wilaya fulani mkoa wa pwani, hakuna aliejua kuwa atakuja kuwa mzigo sana kwa nchi. Aliporudi alipewa kazi ya katibu Mkuu wizara ya mipango chini ya Waziri Professor Abdurlahmani Babu ambaye mara moja aliona weakness yake na kumkataa. Ndipo Nyerere alipoamua kumpa kazi ya kufundisha Chuo kikuu ambapo alipata uprofessor kutokana na mshahara aliotoka nao serikalini wa katibu mkuu wa wizara. Huyu mtu hakuwa professor on merit. Niliwahi kusoma review iliyoandikwa na Professor Shivji kuhusu profesorial inaugural lecture ya Malima iliyokuwa ikiitwa kitu kama " The Political Economy of Devaluation in Developing Countries "; Shivji alionyesha kuwa this guy was really bogus. Unfortunately professor Malima hakuwahi kuandika technical paper yoyote kudhihirisha umahiri wake kama mtaalamu wa uchumi, alichoacha ni technical reports kadhaa zisizokuwa na maana yoyote na ambazo hakuna hata moja ilyowahi kuwa cited.

Kama kuna waziri wa fedha aliyewahi kuvurunda pale nchini basi ni huyu bwana. Tumekuwa na mawaziri akina Jamal, Mtei, Msuya, Malima, Kibona, Kikwete, Mramba, na yule Professor wa minofu ya samaki simkumbuki jina lake. Wote walivurunda kwa namna fulani isipokuwa labda Mtei, Jamal na Kibona; hata hivyo nadhani Malima alitia fora kwa kuvurunda.
 
wanabodi,
Tuachane na Ukabila maanake tafsiri yake ngumu sana. sasa naona tumefikia kwa Wazaramo kudai pwani... hatari tupu.

Hata tukitazama kipengele hiki cha katiba kinachosema:-
(3) Raia yoyote wa Jamhuri ya Muungano hatakuwa na haki,
hadhi au cheo maalum kwa misingi ya nasaba, jadi au urithi
wake.
(4) Ni marufuku kwa sheria yoyote kutoa haki, hadhi au cheo
maalum kwa raia yeyote wa Jamhuri ya Muungano kwa misingi
ya nasaba, jadi au urithi.
(5) Ili watu wote waweze kufaidi haki na uhuru vilivyotajwa na
Katiba hii kila mtu ana wajibu wa kutenda na kuendesha shughuli
zake kwa namna ambayo haitaingilia haki na uhuru wa watu
wengine au maslahi ya umma.
Sasa kama mtu ataweka watu wake na kusema wana elimu na ujuzi kwa kazi hiyo hapo tayari kisha tengua maelezo yote ya katiba na hakuna kipimo cha kuhalalisha sheria ya katiba hiyo. Kisha imeacha tobo kibao za Ukabila na udini kwa sababu ambazo sizifahamu maanake sheria lazima izuie kila tobo ambayo inaweza kujitokeza.
Na kibaya zaidi ni kwamba tunakubali vitu hivi hali kuna watu 100 wenye ujuzi na uwezo kama hao ndugu zake huyo kiongozi. Pili, ukitazama maelezo ya mswahili utakuta kwamba sio mtu mmoja tu katika taasisi anayezungmziwa. Ni karibu nusu nzima ya watendaji kazi waliopata ajira pale kuwa kabila fulani!.. hapa wandugu napata taabu kidogo, ingekuwa wakati ule wa Uhuru ningeelewa na hata Nyerere alipokuwa akitoa sababu zake zilileta maana lakini sio leo. Elimu gani ambayo utawakuta makabila fulani peke yake wenye uwezo?... Jamani tukubali kuna baadhi ya watu (magugu) ambayo yanatakiwa kuondolewa. nchi haina Ukabila ila kuna uwezekano ukashamiri ikiwa tutapuuza.
Kichuguu,​
Kwa taarifa niliyoipata inasemekana kuwa Prof. Malima alipinga uuzaji wa IPTL au TTCL (mojawapo) na ndio sababu hasa ya yeye kuondolewa baada ya IMF kugunduia kuwa ndiye alimshauri Mwinyi kutokubali deal. Walipomwondoa deal likakubali. haya maneno kweli?..
 
mswahili you just propagating coons of the tycoons like the commies"
nataka nikueleweshe kuwa nchi hii bado hatuna cha kujivunia kwa elimu ya juu.,,so kujisifu kwa wasomi wa miaka hiyo ni kupoteza muda tuwahimize vijana wa leo kusoma kule al haramain ,,kinondoni ,jangwani ets
alafu kaka siwezi kuona ngumun kuwaita dau na kawambwa dr kwa sababu phd still sio big deal ,kwa mtu aliyeanza shule na miaka saba ni sawa na kawaida kupata phd na miaka 28/29....no big deal ,kwenye ukoo wetu kila familia kuna phd wawili hadi watatu sio hao wakutafuta kwa mawani na kuwapigia debe..haTA BOT siku hizi robo wana phd kiasi hawaitani tene dr,it becomes too monotonous ....
kuhusu utoto wa mjini kama kuwa kibali cha kupaa ..i wish you and him luck...but i am afraid kama mpiga debe wake ni wewe unamuharibia ,na humsaidii .you know hakuna atakayekubali kiongozi anayefagilia udini na kujenga ...kwa pesa za wachangiaji[ukisikia eeeh ,umenielewa],sasa unamfananuisha dau na yule mdini malima ambaye kabla hajafarii alishahamia chama kingine kinachopendelea udini NRA chini ya aboubakary ulotu...
dua ,
sikujijibu kwenye game reserve ,nilikua natoa explanation too..however kuna tofauti hata za kimamlaka kwani game rerve zinaangaliwa moja kwa moja na wizara wakati national park zipo chini ya TANAPA
 
Kichuguu,[/LEFT]
Kwa taarifa niliyoipata inasemekana kuwa Prof. Malima alipinga uuzaji wa IPTL au TTCL (mojawapo) na ndio sababu hasa ya yeye kuondolewa baada ya IMF kugunduia kuwa ndiye alimshauri Mwinyi kutokubali deal. Walipomwondoa deal likakubali. haya maneno kweli?..


Hili swala la IPTL au TTCL sidhani kama ni kweli kwa sababu ni jambo lililojitokeza late sana. Inawezekana Malima alishiriki katika majadiliano na hakuwa amekubaliana na deal hilo kweli; sina uhakika.

Jambo ninalofahamu kabisa ni kuwa Malima aliondolewa Wizara ya fedha kwa sababu ya utendaji mbovu ikiwa ni pamoja kutoa mishamaha ya kodi kwa washikaji wake na wale wa Mustahiki Meya Kitwana Kondo wakati huo. Jambo jingine lilikuwa ni kuhusu usimamiaji wa pesa zilizokuwa zimetolewa na IMF zitumike kukopesha wafanya biashara wa ku-import bidhaa nchini. Pesa hizo zilitakiwa zirudishwe lakini Malima alizitoa kama zawadi na hadi leo haieleweki kama kweli pesa hizo zilirudishwa. Ni Kutokana na Uzembe wa malima ndipo lilipotolewa shinikizo la kuanzishwa hii TRA ya leo.

Kuna tetesi kuwa alikuwa amefungua account binafsi kwa jina la waziri wa fedha wa Tanzania ambayo ilikuwa inapokea pasent fulani ya mikopo na misaada ya serikali. Alipoondolewa uwaziri tu nao wajanja huko majuu wakasimasisha account hiyo na kuhamishia pesa zote kwenye account ya serikali bila yeye kujua. Sasa wakati Malima alikwenda kuchota pesa kidogo kwa ajili ya kumwachia Adam pocket money akakuta account inasema kuwa yeye siyo waziri kwa hiyo haruhusiwi kutoa pesa kwenye account hiyo. Alipata shock ambayo unasemekana kuwa ilichangia katika kuchukua maisha yake. Hizi ni tetesi ambazo zinaweza kuwa siyo sahihi kwa vile sikupata kuzithibitisha, inawezekana kuna anayezijua vizuri zaidi kwenye forum hii.
 
mkandara wrote:Kwa taarifa niliyoipata inasemekana kuwa Prof. Malima alipinga uuzaji wa IPTL au TTCL (mojawapo) na ndio sababu hasa ya yeye kuondolewa baada ya IMF kugunduia kuwa ndiye alimshauri Mwinyi kutokubali deal. Walipomwondoa deal likakubali. haya maneno kweli?..

Mkandara,
Prof.Malima aliondolewa kutokana na mapendekezo ya Tume ya Mohamed Aboud. Tume hiyo iliundwa na Raisi Mwinyi kuchunguza, pamoja na mambo mengine, udhaifu wa serikali ktk kukusanya kodi.

Rufiji wrote:
Mimi naomba nieleweshwe , huyu mangi alikuwa ni mangi wa wachaga gani ? kwa sababu kwa ninavyojua mimi kuna wachaga wengi kama machame, marangu , rombo , kibosho hawa wote wanaitwa wachaga ila wana tofauti kubwa sana kwani hawazungumzi lugha moja !

Sasa mimi nashindwa kuelewa wanabodi wanapotaka kulabel kama kuna kitu kimoja collectively kinachoitwa wachaga. Hawa watu sio kuwa hawazungumzi lugha moja bali pia hawapendani wao kwa wao . Mfano ni marufuku kwa mmachame na mkibosho kuoana ...najua ni vitu vya zamani but trust me vitu hivi bado vina exist.

Rufiji,
siyo hayo uliyoyaeleza kwa umahiri mkubwa hapo juu. Naona hapa kunakulazimisha hoja kiasi cha kuwaweka Wachaga na Wapare ktk kundi moja la "Wakilimanjaro." Hawa watu hawawezi kuwa na mkakati wa pamoja[joint strategy] hata siku moja. Zaidi, Wapare walikuwa upande wa Tanga mpaka baada ya majimbo kuvunjwa!!
 
Back
Top Bottom