Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Dua, sijaangalia ni nani aliyesema, nimeangalia hoja alizotoa. Hakuna ushahidi aliotoa ambao unaondoa maelezo mengine na kubakia ukabila tu. Je ni undugu unaoendelea, je ni urafiki, je ni rushwa? Kuona majina ya watu wa kabila moja na kudai huo ni ukabila ni hitimisho la kihisia (emotional conclusion). We have to eliminate all the other factors before we conclude with authority that there is tribalism in TRA and other institutions. As long as the other factors are at work, madai ya ukabila have no basis in reality or fact and they remain to be just that, madai!!

Endapo itatokea kuwa kwenye mtaa fulani majambazi wamekuwa wakivunja mara nyingi na kuiba, na tukagundua baadaye kuwa wengi wanaoibiwa ni watu wa kipato cha chini, je tunaweza kuhitimisha kuwa wezi wanawalenga masikini? Kabla hatujasema hivyo, tukagundua kuwa kuna nyumba za masikini wengi ambao hazizunjwi mtaa huo huo na tulipofutilia tukadungua kuwa wenye nyumba hizo wameweka vitasa na makomeo ya uhakika na wanahakikisha kuwa kuna mtu nyumbani, je hilo halielezei kwanini nyumba zile nyingine huvunjwa? Sasa wale masikini wanovunjiwa nyumba kila siku watadai wanafanyiwa hivyo kwa sababu ni masikini au kwa sababu nyumba zao hazina ulinzi wa kutosha? Anayeta kuona ukabila anaweza kufanya hivyo, lakini ili aweze kutushawishi sisi wengin ni lazima aoneshe kisayansi kuwa hakuna maelezo mengine yanayoelezea hali hiyo.
 
well said mwanakijiji,you touch were i was thinking,...i like that..i support you kuwa TATIZO LA TANZANIA NI UNDUGUNIZATION aka USHKAJI...mimi nimeshuhudia unakuta bosi anaweza kuwa mchagga anaajiri watoto wa rafiki zake mhaya ,mgogo ets..au mara nyingi nimewaunganishia watu kazi kwa sababu nawafahamu ...lakini sio homeboys ...
tatizo lingine ni ABUSE OF POWER wengi wanawapa watu kazi watu wasio kuwa kabila lao BUT just because ana uhusiano wa kamapenzi na DADA hata kama ni nyumba ndogo....
nataka nikuhakikishie bw mswahili kuwa ukabila tanzania unapotea ..watu siku hizi hawaulizani kabila ila wanaulizana UNAMFAHAMU?...Sasa itategemea mnafahamiana vipi..siku hizi nataka nikuambie kuwa watanzania tumeoana sana kiasi unaweza ukasema mtu sio MCHAGGA Lakini ukifuatalia unakuta MAMA MCHAGGA..au unakuta binti wa kihaya anaitwa KOMBA ...siku hizi huwezi kujua kabila la mtu kwa kuangalia UBINI wake,nafikiri kwa hapo mwalimu alifahulu..
hata kina khamis abdul wapo kilimajaro na bukoba ...sio lazima wawe waswahili
HATA muheshimiwa rais alivyochagua baraza tukubali hakufanya undugu wala ukabila lakini ukweli ni kuwa ametumia KUJUANA au USHKAJI...

SULUHISHO:NAOMBA TUKUBALIANE WANA BODI KWA KAULI MOJA KUWA TATIZO LA TANZANIA YA LEO NI KUJUANA NA WALA SI UKABILA
 
MJJ & PM,

That is why in one of my earlier post I asked whether the problem is tribalism or nepotism/cronyism. To me I would like to agree with you guys that the problem is more of nepotism/cronyism than tribalism.
 
Kama ni kweli hivyo mnavyosema mnaweza kunipa jibu muafaka kwa nini barabara ya kwenda Lindi Mtwara kama alivyosema Mswahili ilipewa bajeti ndogo na ile iendayo Kilimanjaro kupewa bajeti mara kumi na saba zaidi na kuleta utata bungeni. Utaita huu nao ni Kujuana au Undugu?
 
dua fungu la ule msaada wa barabara za kili ,ulikuwa ni msaada wa mfadhili ambaye alielekeza specifically pesa ziende wapi,..hata wafadhili wana priority zao..kwa mfano hizo pesa zili cover pia kuboresha barabara kuelekea hifadhi ya kilimanjaro kupitia njia ya machame na marangu...pia kipindi hicho hicho barabara ya arusha to ngoro ngoro ikajengwa kwa kiwango cha lami....nafikiri kama sikosei hata ile ya kupita serengeti imefanyiwa ENVIRONMENTAL IMPACT ASSESSMENT...unajua wazungu wako very sensitive kusaidia maeneo ambayo pia na wao wanayatumia ,sasa kwenye vivutio vya utalii ni kati ya sehemu hizo...na hata siku moja huwezi kukata pesa ya kupeleka maji nzega kutuka lake victoria upeleke masaini...hiyo ilikuwa zamani na ikatuletea sifa mbaya ,,sasa hivi project management zinashirikisha wafadhili kuanzia hazina....
NIKUPE MFANO WA MILLENIUM GOAL mfuko wa wamarekani kwa nchi masikini ,juzi tu wamekuja hapa na wanafungua ofisi pale hazina ili kusimamia pesa zao zitumike kwa malengo waliyoweka.
 
Nafikiri Mnaikosa point ya Mswahili...
tatizo la mswahili sio wale wanaoibiwa.. kwa mfano wa mwanakijiji - maskini! ...
Huyu jamaa anasema ikiwa hao majambazi wote ni toka Kenya.. ... ambao wamekuja jazana kutokana na mmoja wao kupewa makazi. Mtanisamehe wakenya...
sasa kilio chetu kisiwe kukubali kweli Ukbabila pamoja na kwamba majambazi hawa ni Wakenya ila tunapowashughulikia pia tusianze kusema tunafanya Ukabila kuwafukuza Wakenya!...some mesures lazima yawepo kuhakikisha wizi unakomeshwa badala ya kubishana nani muathirika! it doesn't matter!
Swala la vitasa hiyo ni mila ya Mtanzania kulala madirisha wazi.. utamaduni wa kufunga milango ktk dunia hii ya Utandawazi ni mpya itachukua muda tuweze kuzoea.

Kwa hiyo hapa mswahili anazungumzia majambazi na nyie mnatazama upande mwingine wa wa athirika baada ya mswahili kuzungumzia waathirika kwa makundi yake.
 
PM

Unaweza kunipa jina la mfadhili wa hiyo na alitoa kiasi gani?
 
Lakini mbona sehemu za Utalii hazipo nyingi Kilimanjaro zaidi ya Arusha, Mara, Manyara na sehemu za kati?
Nawachemsha!
 
Umesahau Morogoro na Selous ambayo ni kubwa sana, pia wafadhili wanapata taarifa ya mahitaji yetu kabla hawajatoa commitment yao. kazi kubwa tunayo.
 
kichuguu said:
(b) Wanaosema kuwa hakuna ukabila nadhani wanasema kuwa siyo instutionalized ukabila kama ilivyo nchi nyingine. Nadhani si vizuri kuuita ukabila, badala yake tungesema ni upendeleo tu kwa vile ingawa kweli upendeleo huo uko skewed kwenye kabila fulani lakini ni kujuana ndiko kunakotumika bila kujali kabila la mtu. Akitokea mnyamwezi mmoja anayejuana sana na Kitilya tangu mashuleni kwao akamtaka Kitilya amsaidie mwanawe halafu kukawa na mchagga ambaye hajuani kabisa na Kitilya, ni wazi kuwa yule mnyamwezi atapata hiyo kazi iwapo anazo sifa zinazohitajika. Vile vile wanosema kuwa wachaga anapata kazi hizo kutokana na elimu yao pia wanasema ukweli. Ni kwa kesi chache sana ambapo utamkuta mchaga anafanya kazi ambayo hana utaalamu nayo, kwa mfano yule jamaa wa B.Sc (Ed) alivyopewa kazi iliyokuwa inahitaji B.Comm or equivalent.


phillemon mikael said:
well said mwanakijiji,you touch were i was thinking,...i like that..i support you kuwa TATIZO LA TANZANIA NI UNDUGUNIZATION aka USHKAJI...mimi nimeshuhudia unakuta bosi anaweza kuwa mchagga anaajiri watoto wa rafiki zake mhaya ,mgogo ets..au mara nyingi nimewaunganishia watu kazi kwa sababu nawafahamu ...lakini sio homeboys ...
tatizo lingine ni ABUSE OF POWER wengi wanawapa watu kazi watu wasio kuwa kabila lao BUT just because ana uhusiano wa kamapenzi na DADA hata kama ni nyumba ndogo....
nataka nikuhakikishie bw mswahili kuwa ukabila tanzania unapotea ..watu siku hizi hawaulizani kabila ila wanaulizana UNAMFAHAMU?...Sasa itategemea mnafahamiana vipi..siku hizi nataka nikuambie kuwa watanzania tumeoana sana kiasi unaweza ukasema mtu sio MCHAGGA Lakini ukifuatalia unakuta MAMA MCHAGGA..au unakuta binti wa kihaya anaitwa KOMBA ...siku hizi huwezi kujua kabila la mtu kwa kuangalia UBINI wake,nafikiri kwa hapo mwalimu alifahulu..
hata kina khamis abdul wapo kilimajaro na bukoba ...sio lazima wawe waswahili
HATA muheshimiwa rais alivyochagua baraza tukubali hakufanya undugu wala ukabila lakini ukweli ni kuwa ametumia KUJUANA au USHKAJI...

Tatizo letu ni kutokuwa na taratibu nzuri za kusimamia ajira za kitaalamu serikalini. Ndiyo maana kwenye mjadala wa Katiba niliwahi kusema kuwa tuunde tume huru ya kusimamia utumishi serikalini ambayo haitakuwa inaingiliwa na wanasiasa. Tume hii ime broad vya kustosha kiasi kuwa vitu kama upendeleo wa kujuana hautaweza kaupata nafasi.
 
that was A EUROPEAN UNION ,and JAPANESE GRANT,mkandara kilimanjaro kivutio kukubwa ni MLIMA ..SO pamoja na mambo mengine uboreshaji wa miundombinu ya haya maeneo ambapo hata wizara ya maliasili enzi ya mama meghji walishirikishwa na kwa kili walilenga kurahisisha usafiri kwa kuboreshanbarabara mbili za kufika kwenye mageti ya mlima upande wa machame na ule wa marangu ....sasa kutoka marangu hadi rombo serikali iliomba xtra funding ili kulink na mpaka wa HOLILI ambao pia ni kianzio kizuri cha kodi kwa serikali''
kwa upande wa dar es salaam ,barabara iliyonufaika katika mpango wa utalii ni ile ya bagamoyo road to kunduchi and bahari beach zone na ile ya bagamoyo to white sands zone hotels...
 
PM

Kama ni EU na Japan basi huu ni uongo wa hali ya juu kwa sababu hata siku moja EU hawachagui wanachotaka kwa vile sio taifa moja huwa wanaangalia Programme zenu. Japan ndio usiseme kabisa hawana interest hizo na wao sio wanaoongoza kwa Utalii bongo.

Mfano mzuri nikupe nchi zinazotoa pesa kama hizo i.e. KFW ya Ujerumani wao walitoa pesa za kujenga barabara ya Mombo - Lushoto kwa sababu wajerumani wa kwanza kuja Bongo walikupenda sana kule, kwa hiyo ndugu hizo pesa sio kweli zilitolewa kwa masharti. HUU NI MCHEZO UNAOFANYIKA HAPO BONGO. Mfano mwingine ni Mwanga water master Plan unafahamu nani anatoka huko. Usitufunge kamba hapa.
 
sellous ni game reserve[the largest in the world] sio national park...so shughuli kubwa pale ni nature tourism,hunting katika baadhi ya maeneo ets..kuna ugomvi na WANAMAZINGIRA katika kufanya shuguli za barabara pale ,wana argue kuwa activities za aina ile zinaweza kuharibu FLORA and FAUNA ,or to scare animals ,wanamazingira hawataki ...kama pia wanavyovutana kujenga barabara na airports SERENGETI ambako wanaogopa wanaweza kuwatisha wanyama wakakimbilia kenya.....
 
sasa DUA unabisha nini,sema basi wewe nani aliyetoa PESA...mimi nimesema kile ninachofahamu..tena japan walitujengea kipande cha arusha to makuyuni ,karatu [ngorongoro]..tena pesa wakapitishia kampuni ya KONOIKE ambao ndio waliojenga barabara,,,..sasa unataka kubisha tu!!!! MIMI kama kitu sifahamu sichangii...na kama nikikosea nikiona facts nakubali.siwezi kudanganya purposely!!! wajerumani pia wapo european union ila wao binafsi ni wachangiaji wakubwa wa WWF[WORLD WILDLIFE FOUNDATION..ambao interest yao kubwa ni tackling of animal pouching[anti pouching],kati ya mengi wanayosaidia,,,
 
Nafikiri umechanganya hapa angalia facts zako tena, nani ana-dictate programme etc. Kwa sababu EU mara nyingi wanafuata programme za nchi, japan vilevile.
 
Jamani ebu nitoeni Ushamba hapa!

Hivi game reserve na national park ni vitu viwili tofauti?..
navyofahamu mimi tofauti ni kuwa land inamilikiwa na national kwa kulinda mazingira fulani i.e manyama, na games reserve iko specific kwa wildlife na inaweza kuwa ya mtu binafsi..otherwise lugha ni moja tu. Kisha tunapotazama sellous nadhani ina kila haki ya kutazamwa zaidi kuliko hizo national park nyinginezo maanake nchi kibao ktk hizi national park hakuna wala hairuhusiwi ujenzi wowote wa kisasa ndani ya hizi mbuga!
 
Mzeee Mswahili,

Heshiima yako mkuuu, kama kawaida na vitu vyako vya uhakika, katika dunia hiii ya uwazi tunahitaji sauti kama yako!

I do not care kama wewe ndiye Tafit, Mlalahoi, Mtaliii, Chinga, au Ole, this time you have a point!
 
Philimon mikael.

unachekesha sana kama ulikuwa huwajui Mohammed Abood na ali Mwinyimvua. kwenye madai yako ya ulidai wachagga wamesoma sana uhasibu.na fani hii watu wengine hawapo, hao niliowataja walishika nafasi ya uhasibu mkuu wa serikali lakini huwajui. naona huna haja hata ya kubishana. nisije kuwa natoa data kwa muuza mbege.

nimekupa vitengo vyote vya TRA na majina ya hao wachagga wenzako bado unaleta madai yasio na kichwa wala miguu.

DR. Dau unadai kazi yake iko kwenye makaratasi umefanya utafiti? huyu bwana hakuanza leo wala jana nenda chuo kikuu cha Dar-es-salaam uliza alikuwa nani? toka first year alikuwa best student ni yeye na DR. kawambwa mbona hatukona wachagga wako kumpita darasani? na kuonyesha chuki zako kwa huyu mswahili unaona hata taabu kumtaja KAMA dr. jee angekuwa kittlya ana phd ungeacha kumwita dr.?

lakini mithali ni mswahili huyu dr.Dau roho yako inakuuma sana.

unaleta uvumi kuwa anapiga kampeni yeye si mwana siasa ni mtaalam. na hahitaji kupiga kampeni kwani yeye ni mtoto wa mjini kuzaliwa mjini ni sawa na form six ya machame au holili,
DR.Dau kacheza Yanga kids chini ya kocha victor akiwa na kina pondamali, mkweche, Adolph n.k mtu huyu hahitajii kampeni kuzaliwa kwake mjini tayari ni kampeni.

labda wewe na akina mushi inabidi mtuvamie watu wa mjini hadi kwenye sekta zetu za mipira ili kutafuta umaarufu, mmetuulia mashirika ya umma na sasa mnatufuata hadi kwenye mipira ndio utaona akina peter mushi kwenye mipira au TFF huko hamkuwepo.

kifupi bwana mikael huwezi kujifananisha na DR.Dau kwa elimu. ufanisi n.k na dua lako ni kama dua la mwewe halimpati dr.Dau hata kama atakuwa gavana wa benki wewe unaumia nini? ulitaka awe tesha au mtei? au ndio maana hadi magazeti yetu ya kichagga yanampiga vita hyu bwana mna wasiwasi atakuwa gavana hivyo wizi wenu BOT utakwama kama NSSF?

kinachozungumzwa hapa ni ukabila uliopo TRA kama una hoja jibu na si kuleta majibu ya bar.

nenda NSSF ukaone rekodi safi za DR.Dau na uliza kwenye menejimenti yake kama kuna wazaramu wangapi?

huyu bwana kachukua phd ana miaka 29 jee vipi kitilya alichukua akiwa na umri huo? hata rekodi hii safi ya shule unapinga bwana mikael? huku ukijitia kuwa wachagga shule mmeipa nafasi?unashindwa hata kuelewa mtu kachukua phd ana 29 tu unaona kitu cha kawaida?angekuwa massawe au mbando? kifupi mnyonge mnyongeni ila mpeni sifa yake.

inaonekana wewe ni kundi la kina Barongo.


Mwanakijiji.

naona kama unajikanyaga kwa kujaribu kupinga tu huku hujui kama kujuana na undugunaizesheni ndio huo huo ukabila.

suala hili la TRA lilipelekwa bungeni sikulipeleka mimi mswahili ni watu waliofanya utafiti na kupata data za kulipeleka huko na kuendelea kulifumbia macho si suluhu kuna baadhi ya taasisi ukiomba kazi lazima unaulizwa jinsi gani utatumia equal opportunity policies ktk kazi yako? TRA kuna kilio cha uchagga kushika hatamu jamani acheni masihara na hata aliyeanzisha topic hii alijua itawakwaza akina mikael phillimon.

mwanakijiji kama una zaidi fuatilia bungeni ukaone vigezo vilivyotumika kulipeleka huko hili suala. mie nimeleta baadhi ya data kulianika jambo hili sasa kuniambia lete hili na lile wakati data hizi ziko bungeni na pia najua tayari umelalia huko. wewe si mwandishi fanya hiyo assignment au wahoji wafanyakazi wa TRA wasio wachagga waulize utapata jibu.umeambiwa mdogowake Lauwo ni kidato cha sita kapewa kitengo kizuri tofauti na elimu yake na hao walisoma kama Benny walipewa kazi zisizolingana na elimu yao tena porini. huyu Benny si muislam wala mswahili ni mtu wa mbeya lakini bado namtetea kuwa hakufanyiwa haki na TRA sasa bwana mikael kunibatiza udini na ukabila wangu vimetokea wapi?
 
Back
Top Bottom