Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,755
Hamisa-Remmy Ongala & Super Matimila
Orch marguis Intern....Kalubandika
Kama wewe ungenipenda ya nini kunidanganya bwana wewe ,kujibandika madaraka siyo yako bwana weeeeeeeeeeeeeeeeeewe
Nimesikia tetesi ...
Bongolendi -penzi haligawanyiki
bht naomba lyrics za huu muziki
Jamani nyimbo bora.. labda tuseme zilizovuma!
Jamani nyimbo bora.. labda tuseme zilizovuma!
Jamani nyimbo bora.. labda tuseme zilizovuma!
Balanta....! unaweza shusha mistari hapa as well + ile kibao cha Monica........kukimbilia Zambia etc etc....?
Mkuu lyrics hizi hapa
1.Sauda
Sauda,Sauda oooh,Sauda dada
Tangu tuwe wapenzi tumependana kikweli pendo letu la moyoni,
Mioyo tusibadili wangu kipenzi dada tuepuke ushauri
Kwa mahasidi wa penzi ooh Sauda kwa mahasidi wa penzi mama ooh Sauda
Tangu tuwe wapenzi tumependana kikweli pendo letu la moyoni,
Mioyo tusibadili wangu kipenzi dada tuepuke ushauri
Kwa mahasidi wa penzi ooh Sauda kwa mahasidi wa penzi mama ooh Sauda
Sauda ooooh mama,Sauda ooooh mamaaa
Mv Mapenzi meli ya wapendwa nao,moyo kama bahari manahodha mimi na wewe
Mv Mapenzi meli ya wapendwa nao,moyo kama bahari manahodha mimi na wewe
(Gurumo) Duniani kuna mengi sawasawa na bahari,kuna papa na nyangumi tena wale wa hatri,hawapendi kuiona meli yetu baharini watafanya kila njia waifupishe safari
Mv Mapenzi meli ya wapendwa nao,moyo kama bahari manahodha mimi na wewe
Mv Mapenzi meli ya wapendwa nao,moyo kama bahari manahodha mimi na wewe
(Gurumo) Duniani kuna mengi sawasawa na bahari,kuna papa na nyangumi tena wale wa hatri,hawapendi kuiona meli yetu baharini watafanya kila njia waifupishe safari Sauda eeh
2.Kesi ya Khanga(Monica)-ZAITA Musica
Mama nipe nauli nikamfuate Monika ee,amekimbilia Zambia na treni ya mizigo ee,kisa cha kukimbia madeni yamemzidi doti kumi za khanga alizokopa hajalipa ee,anatafutwa na Polisi popote hapatikani,na mimi rafiki yake nipo nje kwa mdhamana ee,nililala rumande siku mbili kituoni,usumbufu nilioupata kwa kweli sina raha ee
Mama nipe nauli nikamfuate Monika ee,amekimbilia Zambia na treni ya mizigo ee,kisa cha kukimbia madeni yamemzidi doti kumi za khanga alizokopa hajalipa ee,anatafutwa na Polisi popote hapatikani,na mimi rafiki yake nipo nje kwa mdhamana ee,nililala rumande siku mbili kituoni,usumbufu nilioupata kwa kweli sina raha ee
Naona bora niende Zambia nikamtafute Monika,nimlete Daresalama apambane na kesi yake,e Monika eeh uko wapi
Naona bora niende Zambia nikamtafute Monika,nimlete Daresalama apambane na kesi yake,e Monika eeh uko wapi
Mahakamani wameshapanga siku ya kusikiliza kesi,asipokuja nitapelekwa jela kutumikia kifungo,ee Monika eeeh uko wapi ee,Monika eeh
Naona bora niende Zambia nikamtafute Monika,nimlete Daresalama apambane na kesi yake,e Monika eeh uko wapi
Naona bora niende Zambia nikamtafute Monika,nimlete Daresalama apambane na kesi yake,e Monika eeh uko wapi eeeeh
Mahakamani wameshapanga siku ya kusikiliza kesi,asipokuja nitapelekwa jela kutumikia kifungo,ee Monika eeeh uko wapi ee,Monika eeh
Naona bora niende Zambia nikamtafute Monika,nimlete Daresalama apambane na kesi yake,e Monika eeh uko wapi
Naona bora niende Zambia nikamtafute Monika,nimlete Daresalama apambane na kesi yake,e Monika eeh uko wapi eeeeh
Kuna tatizo nina liona hapa,sawa category ya "MAJINA YA KIKE" sawa ila swala ni,kunabaadhi ya nyimbo zilivuma sana 70's na nyingine 80's let 80's some early 90's na napenda ufahamu kwamba sisi pia ni vijana kwenye malika yetu kwa wakati wetu.
Sasa tuambie lika lipi haswa........?
yenye majina ya kike bwana.. kalubandika???
hata kama zilivuma miaka ya 50 lakini ni za Kiswahili.. labda tutatafuta santuri.. tayari ninazo kadhaa hapa.. tutafikia tupate 10 bora..
Balatanda naomba mistari kidogo kwenye huu muziki..