Tanzania Internet Service Providers: Packages

Status
Not open for further replies.
Kama bado upo Dar na nakumbuka tuliwahi kukutana then tunaweza kuwasiliana via email nami nikakuunganisha na mtu wa ndani Zantel akakupa device flani hivi ukaunganisha kwenye Router yako ili kuweza kuunganisha pc zaidi ya 1 (hata 12 inafanya kazi).

Aidha, hapa kwangu nina Wireless na nimejaribu 30m from home bado inakuwa detected. Device ni nzuri na inafanya kazi, wao hawajaitangaza nami walinipa ili niijaribu na kuwapa feedback. Inafanya kazi vizuri sana. Hutakuwa na haja ya kufunga nyaya kibao kwenye cafe yako, sanasana ni kufanya wireless connection ofisini kwako na ndani ya 3hrs service inakuwa ishaanza.

Gharama wameshusha... I have to contact them ili nikwambie bei ikoje kwa 20GB, that's my package na haifiki hata Tshs 450,000/=

Uzuri wa device ile ni kuwa hata hizi modem za VodaCom na SimbaNet inafanya kazi nazo...

Ahsante mkuu


Ahsante sana mkuu,

Nitakutafuta nikikamilisha mipango yote na kuconfirm sehemu nitakapoweka hiyo project. Niko mkoani kwa sasa nadhani by september nitakuwa nimerudi dar permanently.
 
The most effective time kutangaza biashara ni sasa (kama wanavyofanya VODA), wakati ambapo watu wengi wako alert kupata taarifa za bei poa kufuatia mkonga kuwa tayari.

Sina time na matangazo ya providers wasiokuwa kwenye mkonga.
Makampuni yaliyo kwenye mkonga tayari, package zao lazima utakuta humo speed mfano 1MB, 2MB, nakuendelea. Hebu tizama hii attachment hapo chini,
 

Attachments

  • KDN fiber info.doc
    242.5 KB · Views: 88
Kuikweli unatusaidia sana kufanya maamuzi ya kuweka connection, ila pia nakuomba utupe kidogo undani wa hii connection mpya ya FIBRE OPTIC, nimeisikia lakini sijafahamu kwa undani wake ikoje na ufanyaji kazi wake uko vipi?
 
Hii imeandikwa leo na Mike Mushi (eThinkTankTz newsgroup).
Hello Guys,
SimbaNET was connected to SEACOM few 2 hours ago.

Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Bi Maua Daftari alikuwepo kushudia uzinduzi huo.

SimbaNET imekuwa Kampuni Binafsi ya kwanza Tanzania kujiunga na Mkongo.​
 
Mkuu nashukuru kwa hii information, manake mda mwingi nimekuwa nikijiuliza niwe na ISP gani mzuri. Binafsi natumia TTCL broadband ishu ni pale connection inapopotea, nafikiri kuna nyakati nyaya zao zinaachia, ukiwaita ata kuwapigia simu ni kama ulivyosema, wapo slow sana! For back up nimekuwa na vodacom pia! Lakini ndo ivyo bei yake ipo juu kwa mtu wa kawaida kama mie. Tusubiri tuone huu mkonge mpya unaopita baharini utaleta nini, tunataraji bei kupungua na speed kuongeza, zaidi ya hapo itakuwa ni ndoto zetu
 
Mwenye habari za Voda Internet bomba tafadhali! Inabidi ninunue package leo!
 
Hii imeandikwa leo na Mike Mushi (eThinkTankTz newsgroup).
Hello Guys,
SimbaNET was connected to SEACOM few 2 hours ago.

Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Bi Maua Daftari alikuwepo kushudia uzinduzi huo.

SimbaNET imekuwa Kampuni Binafsi ya kwanza Tanzania kujiunga na Mkongo.


Ndio Mkuu Nimeiona
 
Natarajia kutumia laptop yangu kwa Internet huko Tanzania hivi karibuni. Kutokana na kuwepo kwa fibre optic cable, ni ISP yupi ambaye amejitokeza kutoa huduma nzuri kipesa na kihuduma? Naomba kupatiwa vilevile specs za usb dongles ambazo naweza kutumia huko Tanzania. Natanguliza shukrani.
 
dax max
nimefunguka macho wacha nijipange ktk mitandai yenye akilia...
ila my worry ni kwamba seeacom haijasaidia kitu kwani zaidi ya speed hakuna cost effective at all.
 
Nitainunua this week, tuonane basi mkuu mbona kimya sana wewe?

Halafu kama ni $42 kwa 2GB basi hao ndio watakuwa Cheapest ISP in Tanzania kwa sasa mkuu....
Mkuu umesema ukweli, Nimetumia Africa online, Cats net na wengine lakini bado wana matatizo yao, Ila TTCL ndio kiboko yao maana unaweza kujiuliza kuwa hawa jamaa huduma zao zipo vipi
 
Natarajia kutumia laptop yangu kwa Internet huko Tanzania hivi karibuni. Kutokana na kuwepo kwa fibre optic cable, ni ISP yupi ambaye amejitokeza kutoa huduma nzuri kipesa na kihuduma? Naomba kupatiwa vilevile specs za usb dongles ambazo naweza kutumia huko Tanzania. Natanguliza shukrani.
 
Nimewasiliana na Customer Care VodaCom Tanzania kuhusu gharama za USB Modem internet na wameniambia ni TSh 259.60/MB (non-package rate)! Nimetembelea mitandao mingine kama Zantel, Zain na TTCL gharama zao ni relatively low! Kwa mfano package za Zantel sio zaidi ya TSh 28/MB ukilinganisha na bundle rate ya TSh 180/MB (highest rate) kwa upande wa VodaCom na lowest rate ni TSh 90/MB. Kwa upande wa Zain, TSh 250/MB (non-package rate)! TTCL Mobile (non-package) ni TSh 160/MB wakati TTCL Broadband ni TSh 75/MB (The CHEAPEST, I think)!
 
Nimewasiliana na Customer Care VodaCom Tanzania kuhusu gharama za USB Modem internet na wameniambia ni TSh 259.60/MB (non-package rate)!

Nimetembelea mitandao mingine kama Zantel, Zain na TTCL gharama zao ni relatively low! Kwa mfano package za Zantel sio zaidi ya TSh 28/MB ukilinganisha na bundle rate ya TSh 180/MB (highest rate) kwa upande wa VodaCom na lowest rate ni TSh 90/MB. Kwa upande wa Zain, TSh 250/MB (non-package rate)! TTCL Mobile (non-package) ni TSh 160/MB wakati TTCL Broadband ni TSh 75/MB (The CHEAPEST, I think)!
Karibu mkuu,

Pole, hizi zote mimi nimezijaribu (si kutembelea tu), wote aghali tu.

Pongezi ziwaendee Zain, Blackberry naona wameongeza offer, nimepata sms mwezi uliopita kuwa Tshs 35,000 nloweka itakuwa ni kwa siku 60 (miezi miwili), ni habari njema.

ISP wengine ni aghali sana na bado speed ovyo! TTCL natumia services zao, bei bado ni kubwa, speed ni nzuri kiasi chake (si nilivyotarajia).

Zantel bado natumia services zao, bei wamepunguza SANA... 3GB kwa Tshs 86,000/= na speed ni nzuri ya kuridhisha kabisa.

Nashauri mtu unapoenda kwa ISP basi nunua bundle na si zile za kukwangua vocha na kuliwa tuuuu
 
Hi Maxence Melo,
Binafsi nakubaliana na wewe kuhusu urahisi wa huduma ya Data kwamba huduma inayotolewa na TTCL/Broadband ni the cheapest. Tatizo tu ni kwamba once ipo kwenye Fixed Network coverage yake ni kwa ajili ya watu wa mijini tu.

Pia kama wageweza kuangalia huduma ya TTCL Mobile hali ingekuwa bora sana kwani wakati huduma hii inaanza ilikuwa ni Tshs 90 per MB baada ya hapo ikapanda mpaka kuwa 250 sasa wameshusha hadi 160 per MB, rate zao mpya nimezitoa kama reference kama inavyoonyesha kwenye website yao http://www.ttcl.co.tz

New BroadBand Package Tarriffs effective from 1st October 2009

Package Size

Price per month (Tshs)(VAT inclusive)
Time
Broadband -1GB
30,000
Per Month
Broadband – 2GB
60,000
Per Month
Broadband – 4GB
100,000
Per Month
Broadband – 10GB
200,000
Per Month
Broadband – 20GB
360,000
Per Month
Broadband –40GB
450,000
Per Month
Broadband – 100GB
1,000,000
Per Month

The Retail Price for Broadband Standard (Non-package) is Tsh 75 per MB
 
Nitainunua this week, tuonane basi mkuu mbona kimya sana wewe?

Halafu kama ni $42 kwa 2GB basi hao ndio watakuwa Cheapest ISP in Tanzania kwa sasa mkuu....


nASHUKURU MKUU KWA KUNIPA ELIMU NZURI SASA MIMI NITUMIE IPI?????? MIMI MLALAHOI NAISHI WILAYA YA TEMEKE
 
nASHUKURU MKUU KWA KUNIPA ELIMU NZURI SASA MIMI NITUMIE IPI?????? MIMI MLALAHOI NAISHI WILAYA YA TEMEKE
Kaka umerudi Tz lini?

Jayfour_King, natumia 40GB ya TTCL na naridhika na speed kusema ukweli. Tatizo ni urasimu uliowajaa wafanyakazi wa TTCL, unaweza kumzaba mtu kibao kwa huduma za kusuasua.

Ninayo Zantel 10GB pia, ni so cheap kusema ukweli. Angalia packages za TTCL kisha fikiria Zantel kwa 3GB at Tshs 86,000/= na speed ya Zantel ni nzuri kwa sasa baada ya kuunganishwa na mkonga.

Ni hayo tu kwa sasa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom